WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Monday, April 24, 2017

BREAKING NEWS: MSAJILI JAJI MUTUNGI AFUNGUKA VURUGU CUF



AZILAANI VURUGU HIZO NA KUZIKEMEA
AWATAKA CUF KUHESHIMU MAHAKAMA

Na. Mwandishi wetu.
Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, amelaani na kukemea vikali vurugu zilizotokea miongoni mwa wananchama na viongozi wa chama cha wananchi CUF zilizowahusisha pia baadhi ya waandishi wa habari walioitikia wito uliotolewa kwao.

 Msajili wa Vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi katika Picha ya Maktaba.
Taarifa iliyosainiwa na msajili huyo na kusambazwa kwa vyombo vya habari inasema kuwa msajili huyo anavitaka vyombo vya ulinzi na usalama katika nchi kulifanyia kazi tukio hilo ili wahusika wafahamike na kuchukuliwa hatua mara moja, ‘’ninaomba vyombo vya ulinzi na usalama katika nchi yetu kulifanyia kazi tuio hilo ili wahusika wafahamike na kuchukuliwa hatua za kisheria’’. Imesema taarifa hiyo,

Aidha msajili Mutungi amesema kuwa vurugu hizo zilionekana kuvunja Amani na utulivu na watu kuumizwa jambo ambalo ni tofauti na tunu za taifa za Amani na utulivu huku akiwaasa wanachama wa chama hicho kuwa pamoja na tofauti walizonazo kutulia kusubiri uamuzi wa mahakama kwa kuwa tayari suala hilo liko mahakamani.

‘’ni ukweli usiopingika kuwa suala la mgogoro wa uongozi katika chama cha CUF lipo mahakamani, lakini nikiwa msimamizi wa sheria ya vyama vya siasa na kutambuliwa na kutambuliwa na jamii na jamii kuwa ni mlezi wa vyama vya siasa, nimelazimika kuwasihi wadau wa siasa hususani wanachama wa chama cha CUF, kutambua kwamba kuwapo kwa shauri mahakamani siyo fursa ya kufanya vitendo vya uvunjifu wa Amani, kwani kwani jambo hili ni uvunjifu wa sheria na linaleta sura mbaya kwa jamii’’. Iliongeza sehemu ya taarifa hiyo.

Jaji Mutungi akiwa na Malim Seif

Hayo yamejili ikiwa juzi tarehe 22 mwezi huu wa nne, akiwa katika mkutano na waandishi wa habari uliotishwa na mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF wilaya ya Kinondoni bwana Juma Mkumbi ambaye pia ni mjumbe wa baraza kuu la uongozi la taifa la chama hicho anayedaiwa kumuunga mkono katibu mkuu wa maalim seif sharrif Hamad kuvamiwa na watu wasiojulikana wanaozaniwa kuwa ni wafuasi wa mwenyekiti wa chama hicho profesa Ibrahim Lipumba na kuvuruga mkutano huo uliofanyika katika hoteli ya VINA iliyopo Mabibo Farasi jijini Dar es salaam.

Katika tukio hilo watu kadhaa walijeruhiwa ikiwemo waandishi wa habari na mmoja wa waliovamia kiasi cha kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali mpaka alipookolewa na polisi na kupelekwa katika kituo cha polisi magomeni.