WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Monday, July 17, 2017

BREAKING NEWS:- MSAJILI JAJI MUTUNGI ASHUSHA RUNGU ZITO KWA VYAMA VYA SIASA

  • sasa Ripoti ya CAG Kuwakaanga
  • vyatakiwa kutaja vyanzo vya mapato vya nje na ndani
  • waliofuja Ruzuku kukiona cha moto
  • TCD nayo kueleza matumizi ya gawio la Serikali

Na. Mwandishi Wetu

Upepo wa kusimamia Rasilimali za nchi, kubana matumizi na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha zinazotokana na kodi ya watanzania sasa umezidi kushika kasi katika ofisi ya msajili wa vyama vya siasa inayoongozwa na Jaji Fransis Mutungi.

uchunguzi uliofanywa na JAMVI LA HABARI, unaonyesha kwamba Tayari Msajili wa vyama vya siasa amevilima barua vyama vyote vya siasa hapa nchini vinavyopokea ruzuku na kuvipatia maelekezo kadhaa ya utekelezaji haraka iwezekanavyo.

Chanzo chetu cha siri kilichopo ndani ya chama kimoja cha siasa kikubwa hapa nchini kimedokeza kuwa tayari wao kama chama wameshasikia tetesi za kupewa maelekezo ya kiusimamizi wa fedha na kwamba kwa sasa wanasubiri barua rasmi kutoka ofisi hiyo.

"Mpaka sasa hatujapokea barua bado lakini tumesikia chinichini kwamba tunawindwa". Kimenukuliwa chanzo chetu hicho

Taarifa za uhakika zinasema kuwa moja ya mambo ambayo msajili na ofisi yake wanataka vyama vya siasa vifanye haraka iwezekanavyo ni pamoja na utekelezaji wa maelekezo aliyowapa awali ya kuvitaka vyama hivyo kutengenisha akaunti za kupokea fedha za ruzuku na michango ama vyanzo vingine ili kudhibiti matumizi ya ruzuku ambazo ni fedha zinazotokana na kodi za watanzania.

Aidha Msajili anadaiwa kuvielekeza vyama vyote vya siasa kuweka hadharani vyanzo vyao vyote halali vya mapato tofauti na ruzuku na kuwafahamisha wanachama wao jambo ambalo linapongezwa kuwa ni njia sahihi kudhibiti matumizi ya fedha haramu katika vyama vya siasa 

" unajua vyama vya siasa ni taasisi za umma, lakini vimekuwa vikipokea mamilioni ya fedha safi na chafu bila kutoa taarifa na kujikuta vikitumika kuhalalisha fedha haramu". Anasema  Saidi Kambi wa Chuo cha  Diplomasia alipoulizwa kuhusu jambo hilo.

Mwaka 2013 Ofisi ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG ilisema kwamba vyama vyote vya siasa havikaguliwi japo vinapokea fedha za ruzuku na kuzua mjadala uliopelekea vyama hivyo kuanza kukaguliwa.

Sheria namna saba  ya uanzishwaji wa vyama vya siasa ya mwaka 1992 inamtaja msajili wa vyama vya siasa kama msajili, mlezi na mtunza kumbukumbu wa vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini na aliyepewa mamlaka ya kuvipatia ruzuku kwa mujibu wa sheria na hata kuvifuta vyama hivyo iwapo havitakidhi matakwa ya kisheria ya kuanzishwa kwao.
 
mbali na vyama vya siasa, pia kituo cha demokrasia Tanzania kinachoundwa na viongozi wa vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni TCD (Tanzania Center for Democracy) ni miongoni wa taasisi zitakazokumbwa na mchakato huu.

Kitendo cha msajili Mutungi kuanzisha mchakato huu wa ukaguzi wa fedha za vyama vya siasa kimekuja wakati tayari kukiwa na Malalamiko kadhaa ya baadhi ya viongozi na wanachama wa vyama kuhusu ufujaji wa fedha zinazotokana na ruzuku ikiwemo kulipana mishahara na madeni hewa baina ya viongozi jambo ambalo haliruhusiwi kisheria.

Jamvi la Habari litaendelea kuwajuza kila hatua kuhusiana na jambo hili muhimu.

No comments:

Post a Comment