WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, August 17, 2017

MATUKIO: Watu 13 wauawa na mamia kujeruhiwa, Barcelona

Serikali ya Catalonia imesema watu 13 wamekufa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa baada ya gari la mizigo kugonga watu katika eneo la watalii la Las Ramblas, Barcelona.
Polisi nchini Uhispania wanasema kuwa watu kadhaa wamejeruhiw watoa huduma za dharura wakiwashauri watu kukaa mbali na eneo hilo.
Ripoti kutoka eneo hilo zinasema kuwa watu wanajificha ndani ya maduka yaliyo karibu.
 Shirika la hahari la Reuters linasema kuwa watoa huduma za dharura wameomba kusitishwa kwa huduma za usafiri wa mabasi na vituo vya treni.
Shirika la hahari la Reuters linasema kuwa watoa huduma za dharura wameomba kusitishwa kwa huduma za usafiri wa mabasi na kufungwa vituo vya treni.
Gazeti la El Pais lilisema kuwa dereva wa gari aliliendesha na kutoroka kwa miguu baada ya kuwagonga watu kadha.

"Watu kwenye ofisi yangu waliona gari likiendeshwa kwenda kwa umati wa watu huko Las Ramblas," alisema mtu moja anayefanya kazi sehemu hiyo.
"Niliona karibu watu wawili au watatu hivi wakilala chini


"Kuna magari kadha ya kubeba wagonjwa na polisi waliojihami wakiwa na bunduki kwa sasa," alisema.
Taarifa za kina kuhusu kisa hiki bado hazipo lakini magari yashatumiwa kugonga watu kwenye misururu ya mashambulizi barani Ulaya tangu mwezi Julai mwaka uliopita.

Sunday, August 6, 2017

Uhuru, Raila : Kila mmoja na imani ya Ushindi Kesho

 
Wafuasi wa chama cha Jubilee (kushoto) na wale wa muungano wa NASA wanahuduria mikutano ya mwisho ya kampeni zao katika uwanja wa Afraha, Nakuru, na Uhuru Park, Nairobi siku ya Jumamosi..

Wagombea wa urais nchini Kenya walikuwa na shughuli mbali mbali Jumapili zikiwa zimesalia siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu wa Jumanne. Kulingana na kanuni za tume ya uchaguzi na mipaka, IEBC, ni kinyume cha sheria kufanya shughuli zozote za kampeni saa 48 kabla ya zoezi la uchaguzi kuanza.
Rais Uhuru Kenyatta alijiunga na waumini kwenye makanisa mawili mjini Nairobi na kuwaomba Wakenya wa tabaka mbali mbali kudumisha amani wakati wa uchaguzi huo.
Kulingana na msemaji wa kampeni ya Kenyatta, baadaye mwanasiasa huyo alifanya mikutano kadhaa na viongozi wa chama chake na kuthibisha mawakala watakaowakilisha chama hicho katika vituo mbali mbali vya kupigia kura nchini kote.
Mapema Jumapili, Kenyatta aliwatakia Wakenya zoezi la upigaji kura lenye amani. "Uwe wa Imani ya kikriso, Kiislamu au yoyote nyingine, naomba tufanye uchaguzi kwa amani," alisema.
Raila na Uhuru wakati wa mikutano yao ya kampeni za mwisho.
Raila na Uhuru wakati wa mikutano yao ya kampeni za mwisho.
 
Naye mgombea kwa tikiti ya NASA, Raila Odinga, alikutana na baadhi ya wafuasi wake katika eneo la Karen na baadaye kufanya mikutano na viongozi wa mrengo wake na kutoa orodha ya maafisa wa kushughulikia kipindi cha mpito iwapo atashinda kwenye kinyang’anyiro hicho.
Viongozi hao wawili walifanya mikutano miwili ya mwisho siku ya Jumamosi ambayo ilihudhuriwa na maelfu ya watu. Odinga alikuwa kwenye bustani za Uhuru Park, mjini Nairobi, huku Kenyatta akiongoza mkutano wake katika uwanja wa Afraha Stadium, Nakuru, takriban kilomita 160 kutoka Nairobi.
Rais Uhuru Kenyatta ambaye anagombea urais kwa muhula wa pili alifanya mkutano wa mwisho wa kampeni siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Afraha Stadium, kaunti ya Nakuru. Aliongoza maombi na kuwataka Wakenya kupiga kura kwa amani.
Rais Uhuru Kenyatta ambaye anagombea urais kwa muhula wa pili alifanya mkutano wa mwisho wa kampeni siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Afraha Stadium, kaunti ya Nakuru. Aliongoza maombi na kuwataka Wakenya kupiga kura kwa amani.
 
Kenyatta aliongoza maombi ya amani na kuwataka Wakenya kujitokeza kwa wingi, huku Odinga pia akiwataka wafuasi wa NASA kupiga kura kwa amani.
“Naomba mtupe nafasi nyingine ili kuendelea na miradi tuliyoanzisha wakati wa muhula wetu wa kwanza,” alisema Kenyatta.
“Nawasihi pia muwachague wawaniaji wa nyadhifa zingine kwa tikiti ya Jubilee ili tuendeleze ajenda yetu katika bunge, kaunti na kwingineko,” aliongeza.
Mgombea mwenza wa Kenyatta, William Samoei Arap Ruto alisema waliamua kufanya mkutano wa mwisho mjini Nakuru kwa sababu “ndiko chama chetu cha Jubilee kilizaliwa.”
Naye Raila odinga, ambaye anawania urais kwa mara ya nne, aliambia halaiki ya wafuasi wake kwamba ako tayari kuchukua usukani. “Nimeona dalili kubwa za ushindi kwenye uchaguzi wa Jumanne,” alisema.
“Nawaalika nyote kwa karamu ya ushindi kwenye Ikulu siku ya Jumamosi,” aliongeza huku waliohudhuria wakishangilia.
Mgombea urais wa muungano wa National Super Alliance, Raila Odinga, ahutubia wafuasi wake katika bustani za Uhuru Park mjini Nairobi mnamo siku ya Jumamosi. Alisema yuko tayari kuhika usukani wa Kenya na kwamba ameona dalili kubwa za ushindi.
Mgombea urais wa muungano wa National Super Alliance, Raila Odinga, ahutubia wafuasi wake katika bustani za Uhuru Park mjini Nairobi mnamo siku ya Jumamosi. Alisema yuko tayari kuhika usukani wa Kenya na kwamba ameona dalili kubwa za ushindi.
 
Raila alisema iwapo NASA itaunda serikali, ufisadi utatokomezwa. “Nitaenda nchini Tanzania na kutafuta suluhisho la kimagufuli,” alisema, huku akiashiria kutumia mfano wa uongozi wa rais wa Tanzania, John Pombe Maufuli – ambaye ni rafiki yake wa siku nyingi – kama kigezo cha kupambana na ulaji rushwa.
Mgombea mwenza, Stephen Kalonzo Musyoka, alisema polisi hawasemai ukweli kuhus kifo cha aliyekuwa naibu mkurugenzi wa idara ya mawasiliano na teknolojia kwenye tume ya IEBC, Chis Msando, ambaye mwili wake ulipatikana katika chumba cha kuhifadhi miti cha City, wiki moja iliyopita, baada ya afisa huyo kuripotiwa kupotea siku mbili kabla ya hapo.
“Polisi wanawadanganya Wakenya kwamba wanafanya uchunguzi,’ alisema Musyoka.
Rais Kenyatta anawania urais kwa mara ya tatu baada ya kushindwa na Mwai Kibaki mnamo mwaka wa 2002 na kumshinda Raila Odinga manamo mwaka wa 2013 kwenye uchaguzi uliozua utata na msindi wake kuamriwa na mahakama kuu.
Tayari vifaa vya kupigia kura vimefika katika vingi vya vituo na serikali imetangaza kwamba itatumia maafisa 150,000 kulinda amani wakati wa zoezi hilo.
Wawaniaji wengine wa urais pamoja na wagombea wa nyadhifa mbali mbali pia walifanya mikutano katika maeneo tofauti tofauti na kuwarai wapiga kura kuwachagua. Jumamosi ilikuwa siku ya mwisho ya kufanya kampeni.
Licha ya hali ya wasiwasi kwamba uchaguzi huenda ukagubikwa na ghasia, wachambuzi wametaja kipindi cha kampeni za mwaka huu kama ambacho hakikuwa na visa vingi vya vurugu.

VOA

Kitanzi cha Maalim Seif ni Katiba ya CUF




Ibara ya 117 ya katiba ya CUF ndio mwiba kwake,

Inaelekeza kiongozi anayetaka kujiuzulu lazima akubaliwe na mamlaka iliyomchagua

Yeye na Mtatiro walimpuuza Lipumba, Sasa wanahaha kujinusuru

Mipango kumuangushia lawama msajili wa vyama ,serikali yazidi kugognga mwamba

Kila mahali waambiwa fuateni katiba yenu.

Na Ibrahim Malinda.


KUKWAMA  kwa majaribio kadhaa ya Katibu Mkuu wa chama cha wananchi( CUF) Maalim Seif Sharif Hamad dhidi ya Mwenyekiti wake Profesa Ibrahim Lipumba na viongozi wake waandamizi aliowateua na wengine kuteuliwa na vyombo vya maamuzi vya chama hicho kunatokana na katiba ya chama hicho, imezidi kubainika.

Hivi karibuni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Maalim Seif alipata pigo baada ya kukwama kwa  jaribio lake la kuwavua uanachama wanachama kadhaa wa chama hicho akiwemo Magdalena Sakaya ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara na Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Taifa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kaliua, Mkoani Tabora sambamba na Maftah Nachuma ambaye ni mbunge wa Mtwara Mjini.

Sambamba na jaribio hilo kukwama, wiki chache zilizopita Wakala wa Usajili, Ufilisi na Uthamini(RITA) iliridhia usajili wa wajumbe wapya wa bodi ya wadhamini baada ya kuisha kwa muda wa bodi ya awali ya udhamini wa chama hicho.

Jambo hilo linathibitisha kumuondoa Maalim Seif katika nafasi ya kushinda imani ya wananchama wa CUF baada ya kuenea kwa tetesi kwamba bodi mpya ya wadhamini imeunda na wanachama wanaomuunga mkono Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Lipumba.

Kitendo cha kutambuliwa kwa bodi mpya ya wadhamini wa CUF, kinatoa taswira kuwa kuna uwezekano wa kufutwa kwa mashtaka yote yaliyofunguliwa na bodi ya awali ya udhamini, bodi ambayo kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, ndio imepewa mamlaka ya kushtaki na kushtakiwa kwa niaba ya chama cha CUF.

Aidha maung’uniko ya muda mrefu ya katibu mkuu huyo wa chama hicho kuwa kurudi kwenye kiti kwa mwenyekiti wake Lipumba kunatokana na kubebwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini inayoongozwa na jaji Fransis Mutungi yameonekana kukosa mashiko.

Hali hiyo, inatokana na Lipumba baada ya kujua kwamba katiba ya chama hicho inamruhusu kutengua uamuzi wake kutokana na kutokukubaliwa kwa ombi lake na mamlaka iliyomchagua.
Taarifa zaidi zinasema kwamba kuzembea kwa katibu mkuu huyo kuchukua uamuzi wa kuitisha mkutano mkuu wa chama hicho haraka mara tu baada ya kupokea barua ya Lipumba ya kujiuzulu  ambapo mkutano huo ungepiga kura ya siri ya kuridhia ombi hilo na hatimaye Lipumba kuwa ameondoka rasmi kwa kufuata matakwa ya katiba ndiko kumesababisha mtanziko unaendelea hivi sasa.

‘’Katiba ilimtaka katibu mkuu kuitisha mkutano mkuu maalum kwa ajili ya kujadili na kupiga kura juu ya barua ya Profesa lakini Maalim hakuitisha, hiyo hata ule mkutano wa Agosti 21 pale ubungo plaza haukuwa na lengo la kujadili barua ya Profesa bali ni kuchagua tu Mwenyekiti ambapo kina Taslima walikuwa wanagombea, lakini tulipokataa kwa nguvu ndio ikachomekwa hiyo agenda na hata hivyo hatukufikia hatua ya kupiga kura’’. Anasema mjumbe mmoja wa mkutano mkuu wa chama hicho kutokea viwani Zanzibar tunayemuhifadhi jina lake kwa sasa.

Kwa kifupi  Ibara ya 117(2) ya katiba ya CUF inataka ili kiongozi ahesabike amejiuzulu ni lazima mamlaka iliyomchagua ikubali ombi lake, ambapo kwa Profesa Lipumba mamlaka hiyo ni Mkutano mkuu wa chama hicho ambao haujaridhia ombi hilo . Hata hivyo Maalim Seif na timu yake wanaukwepa ukweli huo wa katiba yao na kueneza propaganda dhidi ya Msajili na Serikali.

Ibara hiyo ya 117 kifungu kidogo cha (2) inasomeka kama ifuatavyo  ‘’Kiongozi atajiuzulu kwa kuandika barua na kuweka saini yake kwa katibu wa mamlaka iliyomchagua au kumteua na kiongozi  huyo atahesabiwa kuwa amejiuzulu ikifika tarehe aliyoiainisha katika barua yake kuwa atajiuzulu pindipo akikubaliwa na mamlaka iliyomchagua au iliyomteua, au kama hakuainisha tarehe ya kujiuzulu kwake basi atahesabiwa amejiuzulu mara baada ya katibu wa mamlaka iliyomteua au kumchagua kupokea barua hiyo na mamlaka iliyomchagua au kumteua kukubali ’’.

Hivi karibuni gazeti hili liliripoti kuwa hali ya mambo inazidi kwenda kombo kwa upande wa Maalim Seif katika mgogoro wa kiuongozi unaoendelea baina yake na mwenyekiti wa Taifa wa Lipumba.

Kitendo cha Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Lipumba kuwavua uanachama wabunge nane na madiwani wawili wa viti maalum kitendo kilichoonyesha kufuata taratibu zote za kisheria na katiba ya ndani ya chama hicho na hatimaye kubarikiwa na ofisi ya Bunge, Tume ya taifa ya Uchaguzi na msajili wa vyama vya siasa.

Taarifa zaidi inaelezwa kinaelezwa kumpagawisha Katibu Mkuu huyo na timu yake kiasi cha kuamua na yeye kuwavua uanachama wanachama wengine kadhaa akiwemo mbunge na Naibu Katibu Mkuu anayekaimu majukumu ya Katibu Mkuu wa chama hicho kwa sasa kutokana na kutokufika ofisini kwa Maalim Seif tangu mwezi Septemba, 2016.

Mmoja wa wanaharakati wa siasa nchini, Joseph Zabron, alisema huu ndio wakati wa Maalim Seif kukaa mezani na Profesa Lipumba kuyamaliza mambo yote kwa kuwa chama imara ni maelewano na si kuanza kutoa shutuma kwa vyombo vya dola.

“Hili suala ukilitizama kwa umakini si Msajili wa Vyama, Bunge wala Tume au Mahakama unaweza ukasema inaingilia CUF zaidi ya Katiba yao wenyewe na ndio maana wao wenyewe wamekwenda mahakamani kukatia rufaa maamuzi ya msajili, lakini maamuzi halali hayakatiwi rufaa,’’alisema.

Kadhalika, wakati hayo yanaendelea hivi karibuni Mwenyekiti wa Chama hicho alifanikiwa kusajili upya bodi ya wadhamini wa chama hicho baada ya ile ya awali kumaliza muda wake wa mujibu wa sheria jambo ambalo limezidisha pigo kwa timu ya maalim seif kwa sababu bodi ya wadhamini ya chama chochote cha siasa huwa moja tu inayosajiliwa na RITA na kwa mujibu wa katiba ya CUF bodi hiyo ndio mamlaka pekee inayoruhusiwa kufanya usimamizi wa jumla wa chama hicho ikiwemo kushtaki na kushtakiwa jambo linalohatarisha uwepo na uhalali wa kesi zilizofunguliwa na bodi ya awali dhidi ya Msajili wa vyama na Lipumba juu ya masuala kadhaa.

Aidha, kukwama huko kwa maalim Seif katika kile anachokiita mapambano ya kukinusuru chama hicho, kunamfanya sasa abadili mawazo na kujiandaa kuhamia chama kingine kikubwa cha upinzani hapa nchini chenye ngome yake kuu Tanzania bara.

Taarifa zaidi zinaonyesha kwamba mpaka sasa maalim na watu wake wameshakubali kuwa kisheria hawawezi kumshinda Prof. Lipumba na kwamba wamebakiwa na njia mbili pekee ama wahame kuhamia chama hicho kikubwa cha upinzani Tanzania bara ama waanzishe chama chao wenyewe kipya.

Mjadala unaoendelea hivi sasa baina ya wadau muhimu wa timu ya maalim Seif ni kwamba iwapo uamuzi utakuwa ni kuwa wanahama, je watahama na vyeo vyao walivyokuwa navyo wakiwa CUF kama hicho cha Katibu mkuu na vya baadhi ya vya wakurugenzi au watahamia na kuwa wanachama wa kawaida jambo ambalo wanahisi litawapunguzia nguvu ya kufanikisha agenda yao ya kuendelea kudai maslahi yao ya kisiasa yanayotokana nauchaguzi mkuu uliopita.

Taarifa hizo pia zinaeleza kuwa mpaka sasa majadiliano ya kina ya namna gani Maalim na timu yake watahamia chama hicho yameshaanza na yanaratibiwa vizuri na wanasiasa kadhaa mashughuli hapa nchini wakishirikiana na baadhi ya wafanyabiashara wenye vinasaba na chama hicho.

Ikiwa mwanasiasa huyo atahama chama hicho na kujiunga chama kingine kama njia ya kufikia lengo lake la kisiasa, kitakuwa ni kielelezo mahsusi cha kudhibitiwa na Prof. Lipumba katika kuijua na kuifahamu katiba ya chama hicho na pia ndio utakuwa mwisho wa ushirikiano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA.

Alipotafutwa na gazeti hili msajili wa vyama vya siasa Jaji Fransis Mutungi, ameendelea kusisitiza kwamba ofisi yake itaendelea kufanya kazi za kuvisimamia vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini kama sheria iliyoviasisi inavyosema na kuongeza kuwa kinachoendelea ndani ya Cuf ni matokeo ya utekelezaji wa katiba ya chama hicho ambacho wameitunga wenyewe.

‘’mimi ofisini kwangu ninasajili vyama baada ya kuzipitia katiba zao na kujiridhisha kuwa hazikiuki masharti ya sheria za nchi, nikizipokea na kujiridhisha siongezi wala kupunguza kitu chochote zaidi ya kuzisajili, na kama ujuavyo katiba ikishapitishwa kinachofuata ni kutekelezwa tu’’. Alisema Msajili Mutungi

‘’kwa hiyo Lugha nyepesi kabisa kuitumia ni kwamba mchawi wa Cuf si Mutungi wala nani, Mchawi wa Cuf ni katiba yao wenyewe, waifate katiba yao inavyoelekeza nina imani hakuna malalamiko yatakayotokea, lakini kama wataendelea kufanya mambo kwa hisia na utashi binafsi, basi haya wataendelea kulalamikiana daima’’. Aliongeza mtaalamu huyo wa maswala ya sheria.

Friday, August 4, 2017

BILIONI 600 ZAMPELEKA NEYMAR PARIS St-GERMAIN

Neymar: Paris St-Germain wamnunua nyota wa Barcelona kwa rekodi ya dunia ya euro 222m

Neymar

Paris St-Germain wamekamilisha kumnunua mshambuliaji wa Brazil, Neymar, kwa ada iliyoweka rekodi mpya ya ununuzi wa mchezaji ya euro 222m (£200m) kutoka Barcelona.
Ununuzi huo wa mchezaji huyo wa miaka 25 umevunja rekodi ya awali iliyowekwa Paul Pogba aliporejea Manchester United kutoka Juventus kwa £89m Agosti 2016.

Atakuwa analipwa euro 45m (£40.7m) kwa mwaka - euro 865,000 (£782,000) kila wiki - kabla ya kutozwa ushuru katika mkataba wake wa kwanza wa miaka mitano. Hiyo ni jumla ya £400m.
Neymar amesema amejiunga na "mojawapo ya klabu zenye ndoto kuu zaidi Ulaya".
"Ndoto kuu ya Paris St-Germain ilinivutia kujiunga na klabu hiyo, pamoja na kujitoleza kwao na nguvu zinazotokana na hili," amesema.

"Najihisi niko tayari kuanza kazi. Kuanzia leo, nitafanya kila niwezalo kuwasaidia wachezaji wenzangu wapya."

Klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Ufaransa imepanga kuwa na kikao na wanahabari mwendo wa saa 12:30 BST Ijumaa (saa nane unusu Afrika Mashariki).
Neymar baadaye atatambulishwa rasmi kwa mashabiki wa PSG Jumamosi wakati wa mechi yao ya kwanza kabisa ya msimu mpya, ambayo itakuwa nyumbani uwanja wa Parc des Princes dhidi ya Amiens.
Neymar alikuwa amefika kituo cha mazooezi cha Barcelona Jumatano akiandamana na babake na mwakilishi wake na kufahamisha klabu hiyo ya Uhispania kwamba angetaka kuondoka.
Alipewa ruhusa na meneja wa Barca Ernesto Valverde kwenda "kupanga mustakabali wake".
Nchini Uhispania, kifungu cha kumwachilia mchezaji kutoka kwa mkataba wake kinaweza tu kufunguliwa kwa mchezaji kulipa pesa yeye binafsi.

Neymar alipofika na pesa Alhamisi kulipa hata hivyo, maafisa wa La Liga walikataa malipo hayo.
Kulitokea majibizano kati ya maafisa wa La Liga na wasimamizi wa Ligue 1.
La Liga wanaamini PSG huenda wanakiuka sheria za uchezaji haki kifedha (FFP) kwa kumnunua mchezaji huyo wa Brazil.

Baada ya kushindwa kulipa pesa hizo kwa La Liga, wawakilishi wa Neymar walilipa euro 222m (£200m) katika afisi za Barca badala yake.
Neymar alijiunga na Barca mwaka 2013 na akashinda mataji mawili ya La Liga na moja la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

PSG wameorodheshwa wa 11 kwa thamani duniani na Forbes lakini ni mara yao ya kwanza kwao kuvunja rekodi ya dunia katika kumnunua mchezaji.

Neymar ni nani?

  • Alizaliwa Mogi das Cruzes, viungani mwa Sao Paulo, 5 Februari 1992
  • Alianza uchezaji wake Santos kwa kutia saini mkataba wa kulipwa Januari 2009
  • Amesalia kuwa mfungaji mabao mengi zaidi Santos baada ya enzi ya Pele ambapo aliwafungia mabao138 mechi 229.
  • Alihusishwa na kuhamia Real Madrid, Chelsea na Manchester United kabla ya kuchukuliwa na Barcelona Juni 2013 akiwa na miaka 21.
  • Alichezea Barca mechi yake ya kwanza dhidi ya Levante Agosti 2013 na akawafungia mabao 105 na kusaidia ufungaji wa mengine 80 katika mechi 186 alizochezea klabu hiyo ya Catalona.
  • Alichezea timu ya taifa mara ya kwanza akiwa na miaka18 na amefunga mabao 52 katika mechi 77 alizochezea Brazil

Thursday, August 3, 2017

Wanyarwanda wanapiga kura kuchagua Rais wao Leo

https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/15B44/production/_97200988_1ef3c25d-0299-49b4-a74a-543ba0b4061f.jpg
Raia nchini Rwanda wanamchagua kiongozi mkuu wa Rwanda katika uchaguzi mkuu Ijumaa, ambao unatarajiwa na wengi kumuongezea muhula mwingine madarakani rais Paul Kagame.
Frank Habineza wa chama cha Green Party na Philippe Mpayimana, ambaye ni mgombea huru pia wanawania urais katika uchaguzi huu.
Lakini wapinzani hao wote hawatarajiwi kumpa ushindani mkubwa Kagame ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2000.
Kuna hisia tofuati kuhusu utawala wake Kagame nje ya nchi hiyo.
Lakini uungwaji mkono mkubwa anaopata ndani ya Rwanda, unamhakikishia ushindi mkubwa katika uchaguzi huu.
Ameutaja uchaguzi huo kama mpangilio usio budi kufanyika.
Anasifiwa kwa kukuza uchumi wa taifa hilo.
Lakini wakosoaji wanamshutumu kwa kukandamiza upinzani na kuzuiwa uhuru wa kisiasa nchini.
Wagombea wengine wanasema wafuasi wao wamenyanyaswa lakini chama tawala kina kana tuhuma hizo.
Katiba ya Rwanda ilikarabatiwa mnamo mwaka 2015, na kumpa rais Kagame nafasi ya kushinda muhula mwingine wa miaka 7 na mihula mingine miwili ya ziada ya miaka mitano kila mmoja.
Kwa hivyo, ana nafasi ya kusalia madarakani hadi mwaka 2034.

MAALIM SEIF AKWAMA

·         Afukuza wabunge, Ashindwa
·         Katiba Cuf yambeba Lipumba
·         Msajili wa Vyama akaza Uzi, Amtaka Afate Utaratibu

Na Mwandishi Wetu.

Ni dhahiri sasa hali ya mambo inazidi kwenda kombo kwa upande wa katibu mkuu wa Chama cha wananchi Cuf Maalim Seif Sharif Hamad katika mgogoro wa kiuongozi unaoendelea baina yake na mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba, Jamvi la Habari linaweza kuthibisha.

Kitendo cha mwenyekiti wa chama hicho Prof. Lipumba kuwavua uanachama wabunge nane na madiwani wawili wa viti maalum kitendo kilichoonyesha kufuata taratibu zote za kisheria na katiba ya ndani ya chama hicho na hatimaye kubarikiwa na ofisi ya Bunge, Tume ya taifa ya Uchaguzi na msajili wa vyama vya siasa, kinaelezwa kumpagawisha katibu mkuu huyo na timu yake kiasi cha kuamua nayeye kuwavua uanachama wanachama wengine kadhaa akiwemo mbunge na naibu katibu mkuu anayekaimu majukumu ya katibu mkuu wa chama hicho kwa sasa kutokana nan kutokufika ofisini kwa Maalim Seif tangu mwezi septemba mwaka 2016 Magdalena sakaya na Maftah Nachuma ambaye pia ni mbunge wa mtwara mjini.

Katika barua yake kwa msajili wa vyama vya siasa, katibu mkuu huyo amemueleza msajili  huyo kuwa baraza kuu la uongozi la taifa lililokutana visiwani Zanzibar hivi karibuni kuwa wajumbe 43 kati ya 45 waliokutana visiwani humo wameridhia kuvuliwa kwao uanachama na kwamba anamfamisha msajili juu ya jambo hilo.

Katika kile kinachoitwa kufuata sheria na katiba ya chama hicho, msajili amemjibu kwa kumkumbusha kuwa yeye kama mlezi na mtunza kumbukumbu wa shughuli zote za vyama vyote vya siasa nchini, anafahamu kwamba ofisi ya katibu mkuu wa chama hicho imekaimishwa kwa Magdalena sakaya na kwamba  ofisi yake inahitaji kupokea kwanza taarifa ya kutenguliwa kwa azimio hilo lililomuweka madarakani sakaya.

Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili inazo zinasema kuwa kwa sasa kambi ya maalim seif imeshakata tama juu ya mgogoro huo baada ya kujitathmini na kujigundua kwamba katiba ya chama chao inampa nguvu mwenyekiti wa chama hicho Prof.Lipumba na hivyo kujilaumu kila kukicha.

‘’unajua mwanzoni Maalim na Julius (Mtatiro) hawakujua kwamba Prof angekuwa na nguvu kiasi hiki, ndio maana wakampuuza, lakini laity kama wangejua namna ya ushindani wanaokuja kukabiliana nao hasa wa kikatiba nadhani hali isingekuwa kama ilivyo hivi sasa’’. Alinukuliwa Saidi Makame wa Darajani Zanzibar
‘’tatizo Prof. analindwa na ibara ya 117 ya chama, sasa kila maalim na wenzetu kadhaa tukijaribu kutafuta namna ya kumpiku, linapokuja swala la kisheria na mahakamani ama kwa msajili huyu bwana anatushinda tu’’. Aliongeza mwanachama huyo wa chama hicho kikuu cha upinzani Zanzibar
Kadhalika, wakati hayo yanaendelea hivi karibuni mwenyekiti wa chama hicho alifanikiwa kusajili upya bodi ya wadhamini wa chama hicho baada ya ile ya awali kumaliza muda wake wa mujibu wa sheria jambo ambalo limezidisha pigo kwa timu ya maalim seif kwa sababu bodi ya wadhamini ya chama chochote cha siasa huwa moja tu inayosajiliwa na RITA na kwa mujibu wa katiba ya CUF bodi hiyo ndio mamlaka pekee inayoruhusiwa kufanya usimamizi wa jumla wa chama hicho ikiwemo kushtaki na kushtakiwa jambo linalohatarisha uwepo na uhalali wa kesi zilizofunguliwa na bodi ya awali dhidi ya Msajili wa vyama na Lipumba juu ya masuala kadhaa.

Aidha, kukwama huko kwa maalim Seif katika kile anachokiita mapambano ya kukinusuru chama hicho, kunamfanya sasa abadili mawazo na kujiandaa kuhamia chama kingine kikubwa cha upinzani hapa nchini chenye ngome yake kuu Tanzania bara.

Taarifa zaidi zinaonyesha kwamba mpaka sasa maalim na watu wake wameshakubali kuwa kisheria hawawezi kumshinda Prof. Lipumba na kwamba wamebakiwa na njia mbili pekee ama wahame kuhamia chama hicho kikubwa cha upinzani Tanzania bara ama waanzishe chama chao wenyewe kipya.

Mjadala unaoendelea hivi sasa baina ya wadau muhimu wa timu ya maalim Seif ni kwamba iwapo uamuzi utakuwa ni kuwa wanahama, je watahama na vyeo vyao walivyokuwa navyo wakiwa CUF kama hicho cha Katibu mkuu na vya baadhi ya vya wakurugenzi au watahamia na kuwa wanachama wa kawaida jambo ambalo wanahisi litawapunguzia nguvu ya kufanikisha agenda yao ya kuendelea kudai maslahi yao ya kisiasa yanayotokana nauchaguzi mkuu uliopita.

Taarifa hizo pia zinaeleza kuwa mpaka sasa majadiliano ya kina ya namna gani Maalim na timu yake watahamia chama hicho yameshaanza na yanaratibiwa vizuri na wanasiasa kadhaa mashughuli hapa nchini wakishirikiana na baadhi ya wafanyabiashara wenye vinasaba na chama hicho.

Ikiwa mwanasiasa huyo atahama chama hicho na kujiunga chama kingine kama njia ya kufikia lengo lake la kisiasa, kitakuwa ni kielelezo mahsusi cha kudhibitiwa na Prof. Lipumba katika kuijua na kuifahamu katiba ya chama hicho na pia ndio utakuwa mwisho wa ushirikiano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA.

Alipotafutwa na gazeti hili msajili wa vyama vya siasa Jaji Fransis Mutungi, ameendelea kusisitiza kwamba ofisi yake itaendelea kufanya kazi za kuvisimamia vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini kama sheria iliyoviasisi inavyosema na kuongeza kuwa kinachoendelea ndani ya Cuf ni matokeo ya utekelezaji wa katiba ya chama hicho ambacho wameitunga wenyewe.

‘’mimi ofisini kwangu ninasajili vyama baada ya kuzipitia katiba zao na kujiridhisha kuwa hazikiuki masharti ya sheria za nchi, nikizipokea na kujiridhisha siongezi wala kupunguza kitu chochote zaidi ya kuzisajili, na kama ujuavyo katiba ikishapitishwa kinachofuata ni kutekelezwa tu’’. Alisema Msajili Mutungi

‘’kwa hiyo Lugha nyepesi kabisa kuitumia ni kwamba mchawi wa Cuf si Mutungi wala nani, Mchawi wa Cuf ni katiba yao wenyewe, waifate katiba yao inavyoelekeza nina imani hakuna malalamiko yatakayotokea, lakini kama wataendelea kufanya mambo kwa hisia na utashi binafsi, basi haya wataendelea kulalamikiana daima’’. Aliongeza mtaalamu huyo wa maswala ya sheria

Wednesday, August 2, 2017

HABIBU MCHANGE : TUMWAMINI NANI, CHADEMA AU ZITTO KABWE

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjWoB6pXyiTI5hN11Z86w-g110eWfHggGcwxRd44E5k3HS78-sH12cGy0YkZOhhy2f9wyqmWSFa5K-l_PilvdVcKfqUmkMAlsSaof0l8tYBQIyrAp9ZWoWQbjfU1wISvxP_pIPjnpiy9Es/s1600/bomola.jpg Habibu Mchange.
Na. Habibu Mchange

Kwa kipindi cha siku kadhaa sasa tumekuwa tukishuhudia maneno makali kutoka kwa wanachama na viongozi wa Chama cha CHADEMA kwenda kwa kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO ndugu Zitto Kabwe.

Njia mbalimbali zimetumika kufikisha mashambulizi hayo huku mitandao ya kijamii ikishika hatamu sambamba na makala za magazetini wakimuita Zitto kabwe ni Msaliti, wengine Kinyonga na wengine Mamluki huku Leo nikisoma makala nyingine ikimuita Zitto Kabwe ni Uyoga kwamba uyoga unaweza kutumiwa kama chakula na kadharika sumu.

Licha ya wanachama na viongozi hawa kujisahau pengine kuwa Zitto sio mwanachama wa chama chao na kwamba yeye ni mwanachama wa chama kingine kinachojitegemea chenye Sera, katiba na miongozo yake, lakini ni Dhahiri Viongozi na wanachama wa CHADEMA hawawezi kumsahau Zitto Kabwe.

Kama kuna jambo CHADEMA na viongozi wake nahisi linawauma na kuwanyima usingizi, basi kuendelea kuwepo kwa mwanasiasa huyu waliyemfukuza chama chao kwa matusi na kejeli nyingi mwaka 2015 mwanzoni.

Naam, ukisoma makala na maandiko yanayomshambulia Zitto kisa tu kakosoa kauli ya mwanasheria wa chama cha CHADEMA Tundu Lissu kuhusu kutaka nchi inyimwe misaada na ushirikiano wa kimataifa, hauna utakachojifunza dhidi ya Chuki dhahiri za wanachadema kwa Zitto.

Kwa Lugha nyepesi tu unaweza ukasema CHADEMA na wafuasi wake wanatamani sana Madini yanayotemwa na Zitto Kabwe wa ACT WAZALENDO yangekuwa yanatemwa Hata kwa asilimia 20 na mmoja kati ya wabunge wao, ndio maana Hata Zitto afanye jema lipi, CHADEMA wao wataacha kulijadili alilolifanya watamvaa Zitto, huu ni udhaifu wa kiwango kikubwa sana.

CHADEMA wameumia sana Zitto kumsifia Rais Dkt Magufuli pale Jukwaani Kigoma, imewauma kwa sababu Hawakujua kuwa Zitto hakumsifia tu Rais Magufuli, Bali pia Zitto amempongeza kwa dhati kiongozi wa nchi anayepeleka mbele maendeleo ya wana kigoma.

Wamekasirika kwanini Zitto aliwahi kuukosoa utawala wa Rais Magufuli hapo nyuma halafu juzi eti amempongeza na kuona kwamba Zitto ni kigeugeu, walitamani Zitto aendelee kukosoa tu na kupinga hata maeneo dhahiri, ama wamesahau kwamba chama alichopo Zitto kwa sasa sio kazi yake kupinga kila kitu, na ndio maana wameamua kujitanabaisha na Slogan ya Taifa kwanza wakimaanisha kuwa wao maslahi ya nchi kwao ni kitu cha msingi kuliko chochote.

Wamesahau kwamba moja kati ya vichagizo vya Zitto na chama chake ni Kuupinga ujinga popote ulipo bila kujali chama cha anayefanya huo ujinga?. Ni vigumu sana kumuelewa Zitto kama haujui mpaka unaingia kwenye chama cha siasa unataka nini zaidi ya kupinga.

TUWAAMINI CHADEMA?...

Kwa msingi wa hoja zao kuwa Zitto ni kigeugeu na kwamba haaminiki Leo anaweza akapinga jambo na kesho akageuka, nadhani CHADEMA ndio wanaongoza kwa kuwa na sifa hiyo.

Kama hiyo ndio Hoja, basi Kwa sasa, CHADEMA ndio chama ambacho hakipaswi na hakiwezi kuaminiwa Mara 1000 zaidi kulinganisha na Zitto alivyo.

Nitatoa mifano Michache.

Mwaka 2013/2014, Freeman Mbowe akiwa kiongozi wa upinzani na mbunge wa Hai, aliwaongoza wabunge wenzake kupinga bajeti ya wizara ya Ujenzi iliyokuwa ikiongozwa na Dkt. Magufuli, mbowe aliipinga bajeti hiyo na kupiga kura ya hapana pale Bungeni, na kusema hawezi kuunga mkono serikali ya CCM.

Mungu si Athumani, mwaka huo huo Dkt Magufuli akaenda jimboni kwa Mbowe Hai, kisha au kabla alikwenda jimboni Rombo kwa Joseph Selasini, huwezi amini aisee,

Sifa alizozipolomosha Mbowe kwa Magufuli na Kikwete (aliyekuwa Rais) hazifikii hata Robo ya zile alizozitoa Zitto Kigoma, ndio maana ilimbidi mpaka Magufuli achukue link ya YouTube na kwenda nayo Bungeni katika bajeti iliyofata na kuwaambia wabunge na watanzani jinsi serikali ya CCM inavyochapa kazi kiasi cha kusifiwa hadharani na Freeman Mbowe. - NANI Tumuamini sasa, CHADEMA au Zitto?.

Naongeza, Kabla ya tarehe 15-09-2007, msamiati wa neno FISADI haukuwa maarufu hapa nchini Tanzania.

Unamjua aliyeuibua sawa sawa?.

Ni CHADEMA kupitia Tundu Lissu,

Ndio, Tundu Lissu akiwa Mwanachadema na mwanasheria machachali, tarehe 15-00-2007 pale viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es salaam, akishirikiana na Mbowe, na viongozi wengine wa upinzani akiwemo Dkt. Slaa, Maalim Seif , Mbatia na Wengine. Lissu alisoma Orodha ya Watanzania kumi na moja wanaolifilisi Taifa hili la Tanzania, tena akasema watu hawa hawanastaha ya kuitwa jina lingine zaidi ya MAFISADI, Lissu akasoma Orodha ya Mafisadi akisindikizwa na vifungu kibao vya Sheria.

Katika Timu ya watu 11 waliotajwa na Lissu kama mafisadi wanaoliumiza Taifa mtu NAMBA 9 aliyetajwa na Lissu na CHADEMA ni *EDWARD LOWASSA* Kwamba kwa mujibu wa Lissu na CHADEMA LOWASSA ni miongoni mwa Wafilisi 11 wa nchi hii, Leo LOWASSA yuko wapi, na Lissu yuko wapi na anasemaje?. - Tuwaamini CHADEMA ?.

Naongeza, Mwaka 2011/2012 kule Arumeru palikuwa na Uchaguzi wa Marudio, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA ambaye pia ni Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema, alisimama Jukwaani na Kuwashukuru wananchi kuwa walimzomea Mzee LOWASSA. Nitayarejea baadhi ya maneno yake

*"Jana mmemzomea LOWASSA, ni Heshima kubwa kwa Mungu Kumzomea Mwizi, LOWASSA ni FISADI*" Huyo ni God bless lema wa CHADEMA , Leo LOWASSA yuko wapi na Lema yuko wapi?, anasema nini?..- TUWAAMINI CHADEMA?.

Niongeze?... Msigwa alimtukana LOWASSA, akasema atakayemnadi na kumshabikia LOWASSA akapimwe akili yake, nani alimnadi LOWASSA 2015, ni Zitto au Msigwa?. - Tuwaamini CHADEMA ?

Mwaka 2010 katika kampeni za Uchaguzi mkuu Moja kati ya Sera za CHADEMA ilikuwa ni kurudisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa na kugeuzwa maghala, CHADEMA wakasema watavirudidha kwa wananchi, Mbowe akasema lazima virudi, Leo mwaka 2017 Mbowe yule yule anasema serikali imekosea kutoa tamko la kuvirudisha viwanda vile vile walivuotaka kuvirudisha wao mwaka 2010. Tuwaamini CHADEMA?...

Mwaka 2010 mpaka 2013 mwanzoni, CUF waliitwa CCM B na CHADEMA, Nccr wakaitwa Washirika wa CCM, miezi michache mbele CCM B na washirika wa CCM wakaungana wakaitwa UKAWA. tuimini CHADEMA?

Mifano iko mingi mingi mingi sana.

USHAURI

nawashauri viongozi na wanachama wa CHADEMA waachane na Zitto, wajenge CHADEMA yao, wamuache Zitto na ugeu geu wake na chama chake, watu makini wanafahamu kwamba CHADEMA ni kikundi cha watu wasaka madaraka tu na sio chama cha siasa.

Chama makini chochote cha siasa hakivunji wala kukiuka misingi yake iliyojiwekea,

Chama makini cha siasa hakiwezi badili Gia angani, lakini kikundi cha wasaka madaraka kinaweza Fanya lolote lile ilimradi tu kipate madaraka.

Wamuache Magufuli afanye kazi ya kuleta maendeleo aliyoahidi, maendeleo hayana chama, maendeleo hayana dini maendeleo hayana Kabila.

Kama Zitto alimpinga Magufuli Jana, sio kigezo cha kpongeza Leo kama amefanya vizuri na wala sio kizingizi cha kutokumkosoa kesho akifanya vibaya, hiyo ndio huitwa siasa ya masuala.

Ndio maana LOWASSA hamsimangi Lissu aliyemwita Fisadi namba Tisa hapa nchini,

Ndio maana LOWASSA hamsimangi Lema aliyekesha akimtukana katika mikutano ya kisiasa

Ndio maana LOWASSA hamsimangi msigwa, hamsimangi Mbowe aliyemkejeli kuwa ni dhaifu na baadae kumpokea wala hamsimangi yeyote, anafanya siasa zenye kukipigania anachokiamini atakipata ama anataraji kukipata.

Vijana, viongozi na wanachama wa CHADEMA kuhangaika na kina Zitto, Kitila mkumbo na Anna Mgwira ni kujidharirisha kwa kuonyesha kiwango kidogo cha uelewa wa masuala ya siasa.

Nawapongeza sana baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA wanaojikita kila uchao kuhangaika kutafuta suluhu ya changamoto za wananchi wao kama MEYA Boniface Jacob, John Mnyika, David Silinde Mwita Waitara nakadharika.

Muhimu kujua ni kwamba Zama zimebadilika, siasa zimebadilika, siasa za Leo si sawa na siasa za miaka mitano iliyopita.

Siasa za Leo zinahitaji wanasiasa wanaoleta majawabu kwa wananchi wao kuliko kutukanana kila uchao. Mmeshatukanana imetosha sasa wapeni majawabu wananchi.

Ndimi,
Habibu Mchange
0762178678
Mwananchi wa kawaida.