WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, August 3, 2017

MAALIM SEIF AKWAMA

·         Afukuza wabunge, Ashindwa
·         Katiba Cuf yambeba Lipumba
·         Msajili wa Vyama akaza Uzi, Amtaka Afate Utaratibu

Na Mwandishi Wetu.

Ni dhahiri sasa hali ya mambo inazidi kwenda kombo kwa upande wa katibu mkuu wa Chama cha wananchi Cuf Maalim Seif Sharif Hamad katika mgogoro wa kiuongozi unaoendelea baina yake na mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba, Jamvi la Habari linaweza kuthibisha.

Kitendo cha mwenyekiti wa chama hicho Prof. Lipumba kuwavua uanachama wabunge nane na madiwani wawili wa viti maalum kitendo kilichoonyesha kufuata taratibu zote za kisheria na katiba ya ndani ya chama hicho na hatimaye kubarikiwa na ofisi ya Bunge, Tume ya taifa ya Uchaguzi na msajili wa vyama vya siasa, kinaelezwa kumpagawisha katibu mkuu huyo na timu yake kiasi cha kuamua nayeye kuwavua uanachama wanachama wengine kadhaa akiwemo mbunge na naibu katibu mkuu anayekaimu majukumu ya katibu mkuu wa chama hicho kwa sasa kutokana nan kutokufika ofisini kwa Maalim Seif tangu mwezi septemba mwaka 2016 Magdalena sakaya na Maftah Nachuma ambaye pia ni mbunge wa mtwara mjini.

Katika barua yake kwa msajili wa vyama vya siasa, katibu mkuu huyo amemueleza msajili  huyo kuwa baraza kuu la uongozi la taifa lililokutana visiwani Zanzibar hivi karibuni kuwa wajumbe 43 kati ya 45 waliokutana visiwani humo wameridhia kuvuliwa kwao uanachama na kwamba anamfamisha msajili juu ya jambo hilo.

Katika kile kinachoitwa kufuata sheria na katiba ya chama hicho, msajili amemjibu kwa kumkumbusha kuwa yeye kama mlezi na mtunza kumbukumbu wa shughuli zote za vyama vyote vya siasa nchini, anafahamu kwamba ofisi ya katibu mkuu wa chama hicho imekaimishwa kwa Magdalena sakaya na kwamba  ofisi yake inahitaji kupokea kwanza taarifa ya kutenguliwa kwa azimio hilo lililomuweka madarakani sakaya.

Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili inazo zinasema kuwa kwa sasa kambi ya maalim seif imeshakata tama juu ya mgogoro huo baada ya kujitathmini na kujigundua kwamba katiba ya chama chao inampa nguvu mwenyekiti wa chama hicho Prof.Lipumba na hivyo kujilaumu kila kukicha.

‘’unajua mwanzoni Maalim na Julius (Mtatiro) hawakujua kwamba Prof angekuwa na nguvu kiasi hiki, ndio maana wakampuuza, lakini laity kama wangejua namna ya ushindani wanaokuja kukabiliana nao hasa wa kikatiba nadhani hali isingekuwa kama ilivyo hivi sasa’’. Alinukuliwa Saidi Makame wa Darajani Zanzibar
‘’tatizo Prof. analindwa na ibara ya 117 ya chama, sasa kila maalim na wenzetu kadhaa tukijaribu kutafuta namna ya kumpiku, linapokuja swala la kisheria na mahakamani ama kwa msajili huyu bwana anatushinda tu’’. Aliongeza mwanachama huyo wa chama hicho kikuu cha upinzani Zanzibar
Kadhalika, wakati hayo yanaendelea hivi karibuni mwenyekiti wa chama hicho alifanikiwa kusajili upya bodi ya wadhamini wa chama hicho baada ya ile ya awali kumaliza muda wake wa mujibu wa sheria jambo ambalo limezidisha pigo kwa timu ya maalim seif kwa sababu bodi ya wadhamini ya chama chochote cha siasa huwa moja tu inayosajiliwa na RITA na kwa mujibu wa katiba ya CUF bodi hiyo ndio mamlaka pekee inayoruhusiwa kufanya usimamizi wa jumla wa chama hicho ikiwemo kushtaki na kushtakiwa jambo linalohatarisha uwepo na uhalali wa kesi zilizofunguliwa na bodi ya awali dhidi ya Msajili wa vyama na Lipumba juu ya masuala kadhaa.

Aidha, kukwama huko kwa maalim Seif katika kile anachokiita mapambano ya kukinusuru chama hicho, kunamfanya sasa abadili mawazo na kujiandaa kuhamia chama kingine kikubwa cha upinzani hapa nchini chenye ngome yake kuu Tanzania bara.

Taarifa zaidi zinaonyesha kwamba mpaka sasa maalim na watu wake wameshakubali kuwa kisheria hawawezi kumshinda Prof. Lipumba na kwamba wamebakiwa na njia mbili pekee ama wahame kuhamia chama hicho kikubwa cha upinzani Tanzania bara ama waanzishe chama chao wenyewe kipya.

Mjadala unaoendelea hivi sasa baina ya wadau muhimu wa timu ya maalim Seif ni kwamba iwapo uamuzi utakuwa ni kuwa wanahama, je watahama na vyeo vyao walivyokuwa navyo wakiwa CUF kama hicho cha Katibu mkuu na vya baadhi ya vya wakurugenzi au watahamia na kuwa wanachama wa kawaida jambo ambalo wanahisi litawapunguzia nguvu ya kufanikisha agenda yao ya kuendelea kudai maslahi yao ya kisiasa yanayotokana nauchaguzi mkuu uliopita.

Taarifa hizo pia zinaeleza kuwa mpaka sasa majadiliano ya kina ya namna gani Maalim na timu yake watahamia chama hicho yameshaanza na yanaratibiwa vizuri na wanasiasa kadhaa mashughuli hapa nchini wakishirikiana na baadhi ya wafanyabiashara wenye vinasaba na chama hicho.

Ikiwa mwanasiasa huyo atahama chama hicho na kujiunga chama kingine kama njia ya kufikia lengo lake la kisiasa, kitakuwa ni kielelezo mahsusi cha kudhibitiwa na Prof. Lipumba katika kuijua na kuifahamu katiba ya chama hicho na pia ndio utakuwa mwisho wa ushirikiano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA.

Alipotafutwa na gazeti hili msajili wa vyama vya siasa Jaji Fransis Mutungi, ameendelea kusisitiza kwamba ofisi yake itaendelea kufanya kazi za kuvisimamia vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini kama sheria iliyoviasisi inavyosema na kuongeza kuwa kinachoendelea ndani ya Cuf ni matokeo ya utekelezaji wa katiba ya chama hicho ambacho wameitunga wenyewe.

‘’mimi ofisini kwangu ninasajili vyama baada ya kuzipitia katiba zao na kujiridhisha kuwa hazikiuki masharti ya sheria za nchi, nikizipokea na kujiridhisha siongezi wala kupunguza kitu chochote zaidi ya kuzisajili, na kama ujuavyo katiba ikishapitishwa kinachofuata ni kutekelezwa tu’’. Alisema Msajili Mutungi

‘’kwa hiyo Lugha nyepesi kabisa kuitumia ni kwamba mchawi wa Cuf si Mutungi wala nani, Mchawi wa Cuf ni katiba yao wenyewe, waifate katiba yao inavyoelekeza nina imani hakuna malalamiko yatakayotokea, lakini kama wataendelea kufanya mambo kwa hisia na utashi binafsi, basi haya wataendelea kulalamikiana daima’’. Aliongeza mtaalamu huyo wa maswala ya sheria

No comments:

Post a Comment