WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, August 24, 2017

Yingluck: Mahakama yatoa kibali waziri mkuu wa zamani Thailand akamatwe

Bangkok, Thailand, 25 August 2017. Mamia ya wafuasi wa Bi Yingluck walifika nje ya majengo ya mahakama ya juu Bangkok 

Mahakama ya Juu nchini Thailand imeahirisha kikao cha kutoa hukumu katika kesi ambapo waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo Yingluck Shinawatra ameshtakiwa makosa ya uhalifu ya kuzembea kazini.
Majaji hao wakiwa mjini Bangkok wametoa kibali cha kukamatwa kwake wakisema hawaamini alivyosema kwamba amekosa kufika mahakamani kwa sababu anaugua.
Mahakama imeahidi kutoa huku tarehe 27 Septemba.

Ijumaa, mawakili wa Bi Yingluck waliomba hukumu icheleweshwe na kuambia mahakama kwamba anaugua ugonjwa wa vertigo na hawangeweza kufika kortini.
Lakini taarifa rasmi ya Mahakama ya Juu imesema waendesha mashtaka "hawaamini mshtakiwa ni mgonjwa kwani hakuna cheti chochote cha matibabu kilichowasilishwa kwa mahakama, na kwamba hali yake ya afya si mbaya mno kiasi kwamba hawezi kufika kortini."
Mahakama imesema itatoa kibali cha kukamatwa kwake kwani anaweza kuikimbia nchi hiyo, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP.

Kadhalika, mahakama imetwaa dhamana ya $900,000 (£703,000) ambayo alikuwa ameiweka wakati wa kuanza kwa kesi hiyo.
Bi Yingluck, amekanusha makosa ya kuzembea kazini yanayohusiana na mradi wa mpunga wa gharama ya mabilioni ya dola.
Iwapo atapatikana na hatia, anaweza akafungwa jela na pia kupigwa marufuku kutoshiriki siasa maishani yake yote.

Bi Yingluck, ambaye alikuwa waziri mkuu wa kwanza mwanamke nchini Thailand mwaka 2011, aliondolewa madarakani mwaka 2015.
Kesi dhidi yake iliwasilishwa na serikali inayoungwa mkono na jeshi ambayo ilimuondoa mamlakani.
Lakini bado ni maarufu na anaungwa mkono sana.
Mamia ya wafuasi wake walikusanyika nje ya Mahakama ya Juu mjini Bangkok kabla ya kusomwa kwa hukumu dhidi yake, huku polisi wengi wakishika doria nje ya mahakama hiyo.
Mpango wa Bi Yingluck wa kulipia sehemu ya gharama ya mpunga ulikuwa sehemu ya ahadi zake kuu kwenye kampeni yake ya kutaka kuchaguliwa, na aliuzindua mwaka 2011 muda mfupi baada yake kuingia madarakani.

No comments:

Post a Comment