WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Sunday, October 29, 2017

MIAKA MIWILI YA JPM : NI MAGEUZI MAKUBWA

Na Ibrahim malinda

IKIWA jana Oktoba 25, imetimia miaka miwili, tangu watanzania wapige kura za Uchaguzi Mkuu na kuchagua Rais, wabunge na Madiwani ambapo Dk. John Magufuli alichaguliwa kuwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mageuzi makubwa yameelezwa kufanyika katika sekta mbalimbali za kimaendeleo kwa kipindi cha miaka miwili ya uongozi wake imeelezwa.

Mageuzi hayo ni pamoja na kufanikisha elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi sekondari, ambapo hivi sasa wanafunzi wanagharamiwa kila kitu na serikali kuanzia ada za shule, mitihani, chakula, jambo ambalo kwa miaka zaidi ya 20, halikuwepo.

Kuwezekana kwa jambo hilo, kumemfanya Dk. Magufuli kuwa mmoja wa viongozi hodari walioweza kutimiza ahadi zao ndani ya muda mfupi na hata kutoa taswira kubwa ya mabadiliko ya maendeleo ambayo kwa namna moja au nyingine walikuwa hakuna.

Taarifa ilizozipata gazeti hili, zilieleza kuwa elimu bora imekuwa mkombozi na hata kufanya kila mzazi kupunguziwa majukumu ya masomo kwa watoto, ambao awali ilikuwa mtihani mkubwa kwa wananchi kushindwa kumudu gharama za masomo.

Mmoja wa mwananchi aliyezungumza na gazeti hili, Joseph Yona, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Tawi la Bokorani, lililopo Temeke, alisema kuwezekana kwa elimu bure ni msaada tosha kwa wananchi, ambao kwa muda mrefu walikuwa wanashindwa kusomesha watoto wao.

“Elimu ni nyenzo ya maendeleo, anapojitokeza kiongozi anaweka jitihada kubwa katika elimu ni msaada tosha. Naifurahia kura yangu niliyoipiga kwa kuwa imesaidia kupata kiongozi bora na mwenye malengo makubwa kwa nchi,’’alisema alipokuwa anazungumza na gazeti hili.

Jamvi la Habari, lilielezwa kuwa ununuzi wa ndege sita mpya , ni uamuzi ambao unatajwa ni wa kihistoria, ambapo kwa muda mrefu nchi ilikosa ndege zake na hata kuhatarisha ustawi wa Shirika la Ndege Tanzania(ATCL), ambalo lilikuwa linaelekea kuzimu.

Kuzinduka kwa shirika la ndege ni moja ya hatua kubwa ya kukuza mapato kwa taifa lolote, hivyo inaelezwa uwepo wa ndege hizo ni hatua kubwa ya kimaendeleo, ambayo kila mtanzania anapaswa kufurahia maendeleo hayo, ambayo yamekuwa makubwa sana.

Akizungumzia fursa za uwepo wa ndege hizo, mfanyabiashara Yusuph Rashid alisema nchi kuwa na ndege zake ni hatua kubwa, hivyo kila mtanzania anapaswa kuona hii ni ufahari mkubwa ambao nchi itapata maendeleo makubwa.

“Leo hii soko la ndege ya Afrika kwa nchi za Afrika limetekwa na Kenya, pamoja na Ethiopia, hivyo nasi lazima tuwe na uhakika wa ndege zetu kwa vile Tanzania inaouwezo mkubwa wa kuwa na mashirika makubwa ya ndege, ambayo kwa namna moja au nyingine tunaouwezo huo,’’alisema.

Taarifa zaidi ilieleza kuwa ujenzi wa reli ya kisasa kwa kiwango cha stardand gauge kutoka Dar es Salaam hadi, Mwanza na Kigoma ni hatua moja kubwa ya kimaendeleo, ambapo kwa zaidi ya miaka 100 reli mpya ya kisasa ilikuwa hakuna, hivyo uwepo wa reli hiyo ni hatua moja kubwa ya kimaendeleo.

Ujenzi wa Barabara za Juu Ubungo na makutano ya Tazara, ni fursa kubwa ya ujenzi wa uchumi imara, ambayo Rais Dk. Magufuli amenuia kuiletea sifa kubwa nchi, kutokana na uwepo wa maendeleo hayo ni hatua moja kubwa ya kimaendeleo kwa nchi kusonga mbele.

Jamvi la Habari linaeleza kuwa uwepo wa mabadiliko makubwa ya kisheria katika sekta ya madini na nchi kuanza kunufaika na mabadiliko hayo, ni hatua kubwa ya kimaendeleo na hata kila mmoja kuona kuwa ufahari mkubwa wa ulinzi wa rasilimali za nchi kuwa zinalindwa kwa kiasi kikubwa.

Pia, inaelezwa katika kipindi cha miaka miwili Rais Dk. Magufuli ameweza kunipa heshima nchi kwa kuhakikisha tunalipwa zaidi ya Bilioni 700 na kampuni ya ACCACIA kutokana na kukwepa kodi.

Uwezekano wa jambo hilo ndio unafanya kuwepo kwa maendeleo makubwa ya nchi yanakuja ndani ya kipindi cha miaka mitano ya utawala wa Rais Magufuli kufanikiwa hasa kutokana na mapato ya kila mwezi kupanda maradufu.

Taarifa za Mamlaka ya Mapato(TRA), zinaeleza kuwa mapato ya nchi kila mwaka yanapanda ambapo sasa hivi kila mwezi toka utawala wa Dk. Magufuli, mapato yamefikia sh. Trilioni 1.3 tofauti na awali ilikuwa bilioni 900.

Ujenzi Bomba la Mafuta Kutoka Uganda Mpaka Tanga, ni mradi mkubwa unaotajwa kuwa na mafanikio makubwa kwenye utawala wa Rais Magufuli kwa kuwa utaweza kutengeneza ajira zaidi ya milioni mbili pamoja na kuipa mapato makubwa nchi.

Uwezekano wa mradi huo, ambao unatajwa kuwa moja ya miradi mikubwa kufanyika nchini, unazidi kueleza mafanikio ya utawala wa Rais Dk. Magufuli kuwa utakuwa salama na maendeleo makubwa kwa nchi.

Pia, inaelezwa udhibiti wa fedha za umma, unazidi kumpa heshima Rais Dk. Magufuli kutokana na aina ya utawala wake kuheshimu fedha za wananchi katika utekelezaji wa miradi mbali mbali nchini.

Jamvi la Habari lilielezwa kuwa ifikapo 2020 zaidi ya asilimia 95, mijini na vijini kutakuwa na uhakika wa maji safi na salama kutokana na utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa fedha za ndani pamoja na wahisani waliolizika na utawala imara wa Rais Dk. Magufuli.

Katika kipindi cha miaka miwili ya Rais Dk. Magufuli huduma mbalimbali za afya zimeboreshwa ikiwemo ununuzi wa vifaa tiba na huduma kama, MRI, CT-SCAN zanunuliwa kwa mafanikio makubwa.

Pia Rais Magufuli amefanikiwa kudhibiti upotevu wa Mapato Bandarin pamoja na kufanikiwa kuimarisha miundombinu ya barabara sehemu mbali mbali ya nchi.

No comments:

Post a Comment