WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, January 17, 2018

MAAJABU : Apasuka koo kwa kujaribu kuzuia kupiga chafya

Madaktari wa upasuaji wakimuhudumia mgonjwaMadaktari wameonya kwamba kuzuia kupiga chafya kwa kufunga pua na mdomo kunaweza kukusababishia madhara makubwa.
Hii inajiri baada ya madaktari mjini Leicester kumtibu mtu mwenye umri wa miaka 34 ambaye alipusuka koo kwa kujaribu kujizuia kupiga chafya.
Huku kukiwa hakuna nafasi ya hewa ya chafya hiyo kutoka, ililazimika kupasua tishu laini.
Licha ya kwamba kisa hicho sio cha kawaida, madaktari wameonya kwamba watu wengine wanafaa kujua kuhusu hatari hiyo.
Kuzuia kupiga chafya kunaweza kuharibu masikio mbali na kuathiri ubongo wameonya katika jarida la BMJ.

Mtu huyo anasema kuwa alihisi kuwashwa katika koo yake baada ya chafya hiyo na muda mchache baadaye akaanza kuhisi uchungu na akaanza kushindwa kula na kuzungumza.

Wakati madaktari walipomchunguza waligundua kwamba alikuwa ana uvimbe katika koo na shingo yake.
Picha za X ray zilizopigwa zilibaini kwamba kuna hewa inayotoka kupitia tushu laini zilizopasuka kupitia shingo yake.
Mtu huyo alilazimika kulishwa kwa kutumia paipu kwa siku saba mfululilizo ili kutoa fursa kwa tishu hizo kupona.
Baada ya kulazwa hospitalini kwa juma moja, mtu huyo alienda nyumbani ambapo alipona.

KAYOMBO :UBUNGO TUTAJENGA SEKONDARI YA A-LEVEL KUTEKEZA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM.

ELIMU BURE KWA WOTE: TULIAHIDI TUMETEKELEZA.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg. John Lipesi Kayombo akiwaonyesha utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 wajumbe wa Kamati ya siasa Wilaya ya Ubungo inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo Ndg. Lucas Mgonja.

Mkurugenzi Kayombo kwa kushirikiana na watumishi wa Manispaa hiyo ameweza kujenga ukuta (fensi), vyoo na vyumba nane vya madarasa katika shule ya msingi Ubungo Plaza.

Kabla ya hapo shule hiyo ilikuwa haina uzio kitu ambacho kilikuwa ni hatarishi kwa wanafunzi wa jinsia zote.

Pia kulikuwa na uhaba wa vyoo ambapo kilikuwa ni chanzo kikubwa cha magonjwa.

Sambamba na hilo wanafunzi walikuwa wanasoma katika majengo chakavu swala ambalo ni hatarishi kwa maisha yao.

Habari njema ni kuwa Mkurugenzi Kayombo ameahidi kujenga shule ya Sekondari ya A - level katika eneo hilo.

Ujenzi wa sekondari hiyo ya kidato cha tano na sita utasaidia kurahisisha upatikanaji wa elimu katika manispaa hiyo na jambo ambalo litakuwa ni Mara ya kwa Manispaa hiyo tangu ianzishwe.

Jamvi la Hbari linampa Hongera Mkurugenzi Kayombo kwa kuendelea kutekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 kwa vitendo.

ZIFAHAMU FAIDA MBALIMBALI ZA FENESI KATIKA MWILI WAKO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh_CmEdJWjpld8xQfRzwDXKNQo-EURqf7lOdb3hyphenhyphen9c-W7-srTWcUMkP4tEAiNn4oxO76cM-O484_yIXcF4okipP9X1ghKvSGYDYphY0Wa98m3B0AyJd868VKiYtJM5bQ0H7oEjRFky8H-ux/s320/unnamed.pngJ

Huenda umewahi kuliona na kulipita tu ama kutovutiwa na ladha yake ama kukereka na utomvu wake baada ya kula


Habari mbaya kwako ni kwamba umekosa kitu adimu na maridhawa sana......Hili ni moja ya matunda yanayochukuliwa kama MFALME WA MATUNDA (The King of Fruits) kwa kuwa na karibu vitamin vyote muhimu yaani A, B1, B2 na C..



Na sehemu zinazotumika ni majani, matunda, utomvu, mizizi na magamba. Na mfenesi unaweza kukua hadi kufikia kimo cha mita 20.........na nakusihi sana kuanzia leo ujitahidi kula walau punje tatu tu na ukiweza hata mbegu zake kwa kadri ya mada hii



Leo nimejikuta tu nafukunyua tunda hili baada ya kulikuta mahali fulani na jinsi watu walivyokuwa wanatua kilich cha thamani ndipo nilipoanza kugoogle nikakuta faida na hata hilo jina la lugha ya malkia huitwa Jackfruit




Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomithilika. Licha ya sifa hii, tunda hili linatajwa kuwa na faida lukuki endapo litaliwa na mwanadamu.



Hakuna anayejua vizuri asili ya mafenesi lakini inaaminika asili yake ni katika misitu ya mvua nyingi ya Magharibi ya ghats (western ghats). Lakini kwa sasa inalimwa katika nchi za india, Burma, Sri lanka, China, Malaya, East in indies, Qeens land, Maturities, Hawaii, Suriname, Brazil, Kenya, Uganda na Tanzania, Na nchini Tanzania hulimwa Pemba, Unguja, Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Tanga na Mbeya(Kyela) nk.




Kwanza, linatajwa kuwa na virutubisho kadha wa kadha vyenye kazi mbalimbali mwilini. Baadhi ya virutubisho hivyo ni pamoja na vitamini za aina mbalimbali, madini, protini, mafuta, uwanga na nyuzinyuz (fiber) ambazo husaidia kwenye mfumo wa mmeng'enyo na kuchagiza tatizo la kupata haja (constipation) na linasaidia pia kuzuiwa kuvimbiwa.



Fenesi pia linatajwa kuwa chanzo kizuri cha nishati kisichokuwa na lehemu (cholesterol). Si hivyo tu, bali pia ni chakula chenye virutubisho vya kuondosha sumu mwilini vinavyoweza kuukinga mwili dhidi ya saratani na magonjwa mengine kadha wa kadha,



Sukari ya Fenesi ni dawa ya sukari sumu mwilini kwa kuwa linasharabiwa taratibu mwilini na kufyonza sukari sumu na hii husaidia pia katika kuhibiti shinikizo la damu mwilini ( Jackfruit is more slowly absorbed into the bloodstream, which prevents sugar crashes, sugar cravings, and mood swings, They are well known because of its high potassium content. This helps the blood vessels relax and maintains proper blood pressure.)

kutoka michuzi Blog ambapo tunaambiwa habari hii imeandaliwa na ​ Geofrey Chambua ​kutoka vyanzo mbalimbali

Thursday, January 11, 2018

MKURUGENZI KAYOMBO WA UBUNGO AKABIDHIWA MADARASA YA KIMATAIFA


 
Katika kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha mapinduzi CCM, na kuunga mkono juhudi na jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyejipambanua kuwasimamia na kuwatetea watanzania wanyonge,
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, John L. Kayombo Aliyesimama

Moja ya Madarasa yaliyopokelewa leo ambayo yametengenezwa pamoja na madawati na miundombinu muhimu ya kusomea wanafunzi.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Mheshimiwa John Lipesi Kayombo, sambamba na mkuu wa wilaya hiyo Mheshimiwa Kisare leo wamepokea madarasa mawili yaliyojengwa na wadau wa maendeleo wanaifanya shughuli zao katika manispaa hiyo ya ubungo madarasa yaliyojengwa katika shule ya Sekondari Urafiki iliyopo kata ya Ubungo

madarasa hayo mawili yaliyojengwa kwa ustadi wa aina yake yamejengwa baada ya kukubaliwa kwa maombi ya Mkurugenzi huyo kwa kampuni ya Tanzania Steel Pipes LTD ya jijini hapa na kwamba sehemu kubwa ya madarasa hayo yamejengwa kwa chuma

‘’wakati nateuliwa kuwa mkurugenzi nilifanya ziara kwenye shule hii nilikuta hapa kuna madarasa matano yamechakaa kabisa hayapaswi kutumiwa na wanafunzi wetu, niliagiza mara moja yavunjwe na tutafute pesa kwa ajili ya kujenga madarasa mengine matano mapya…kwa neema ya Mwenyezi Mungu tulikutana na hawa watu wa viwanda tukazungumza nao nikawaomba watujengee madarasa mawili’’. Alisema Mkurugenzi Kayombo wakati akimkaribisha mkuu wa wilaya ya Ubungo kutoa hotuba ya kuopokea madarasa hayo


‘’niseme tu mheshimiwa mkuu wa wilaya, tutayatunza madarasa haya, ni madarasa ya mfano hayapo wilaya ya ubungo na mkoa wa Dar es salaam hayapo, hapo hapa Urafiki Sekondari’’. Alipngeza Kayombo

kabla ya ujenzi wa madarasa hayo shule hiyo ilikuwa na madarasa matano mabovu yanayohitaji maboresho ambapo baada ya kukamilika kwa madarasa hayo mawili, hivi sasa taratibu za kizabuni kukamilisha ujenzi wa madarasa mengine matatu zimefikia hatua za mwisho na mpaka kufikia mwezi mei mwaka huu inatarajiwa madarasa yote kuwa yamekamilika.




taarifa zaidi kuhusu madarasa hayo tutawaletea.