WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, January 11, 2018

MKURUGENZI KAYOMBO WA UBUNGO AKABIDHIWA MADARASA YA KIMATAIFA


 
Katika kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha mapinduzi CCM, na kuunga mkono juhudi na jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyejipambanua kuwasimamia na kuwatetea watanzania wanyonge,
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, John L. Kayombo Aliyesimama

Moja ya Madarasa yaliyopokelewa leo ambayo yametengenezwa pamoja na madawati na miundombinu muhimu ya kusomea wanafunzi.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Mheshimiwa John Lipesi Kayombo, sambamba na mkuu wa wilaya hiyo Mheshimiwa Kisare leo wamepokea madarasa mawili yaliyojengwa na wadau wa maendeleo wanaifanya shughuli zao katika manispaa hiyo ya ubungo madarasa yaliyojengwa katika shule ya Sekondari Urafiki iliyopo kata ya Ubungo

madarasa hayo mawili yaliyojengwa kwa ustadi wa aina yake yamejengwa baada ya kukubaliwa kwa maombi ya Mkurugenzi huyo kwa kampuni ya Tanzania Steel Pipes LTD ya jijini hapa na kwamba sehemu kubwa ya madarasa hayo yamejengwa kwa chuma

‘’wakati nateuliwa kuwa mkurugenzi nilifanya ziara kwenye shule hii nilikuta hapa kuna madarasa matano yamechakaa kabisa hayapaswi kutumiwa na wanafunzi wetu, niliagiza mara moja yavunjwe na tutafute pesa kwa ajili ya kujenga madarasa mengine matano mapya…kwa neema ya Mwenyezi Mungu tulikutana na hawa watu wa viwanda tukazungumza nao nikawaomba watujengee madarasa mawili’’. Alisema Mkurugenzi Kayombo wakati akimkaribisha mkuu wa wilaya ya Ubungo kutoa hotuba ya kuopokea madarasa hayo


‘’niseme tu mheshimiwa mkuu wa wilaya, tutayatunza madarasa haya, ni madarasa ya mfano hayapo wilaya ya ubungo na mkoa wa Dar es salaam hayapo, hapo hapa Urafiki Sekondari’’. Alipngeza Kayombo

kabla ya ujenzi wa madarasa hayo shule hiyo ilikuwa na madarasa matano mabovu yanayohitaji maboresho ambapo baada ya kukamilika kwa madarasa hayo mawili, hivi sasa taratibu za kizabuni kukamilisha ujenzi wa madarasa mengine matatu zimefikia hatua za mwisho na mpaka kufikia mwezi mei mwaka huu inatarajiwa madarasa yote kuwa yamekamilika.




taarifa zaidi kuhusu madarasa hayo tutawaletea.

No comments:

Post a Comment