WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, January 17, 2018

KAYOMBO :UBUNGO TUTAJENGA SEKONDARI YA A-LEVEL KUTEKEZA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM.

ELIMU BURE KWA WOTE: TULIAHIDI TUMETEKELEZA.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg. John Lipesi Kayombo akiwaonyesha utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 wajumbe wa Kamati ya siasa Wilaya ya Ubungo inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo Ndg. Lucas Mgonja.

Mkurugenzi Kayombo kwa kushirikiana na watumishi wa Manispaa hiyo ameweza kujenga ukuta (fensi), vyoo na vyumba nane vya madarasa katika shule ya msingi Ubungo Plaza.

Kabla ya hapo shule hiyo ilikuwa haina uzio kitu ambacho kilikuwa ni hatarishi kwa wanafunzi wa jinsia zote.

Pia kulikuwa na uhaba wa vyoo ambapo kilikuwa ni chanzo kikubwa cha magonjwa.

Sambamba na hilo wanafunzi walikuwa wanasoma katika majengo chakavu swala ambalo ni hatarishi kwa maisha yao.

Habari njema ni kuwa Mkurugenzi Kayombo ameahidi kujenga shule ya Sekondari ya A - level katika eneo hilo.

Ujenzi wa sekondari hiyo ya kidato cha tano na sita utasaidia kurahisisha upatikanaji wa elimu katika manispaa hiyo na jambo ambalo litakuwa ni Mara ya kwa Manispaa hiyo tangu ianzishwe.

Jamvi la Hbari linampa Hongera Mkurugenzi Kayombo kwa kuendelea kutekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 kwa vitendo.

No comments:

Post a Comment