WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, January 17, 2018

ZIFAHAMU FAIDA MBALIMBALI ZA FENESI KATIKA MWILI WAKO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh_CmEdJWjpld8xQfRzwDXKNQo-EURqf7lOdb3hyphenhyphen9c-W7-srTWcUMkP4tEAiNn4oxO76cM-O484_yIXcF4okipP9X1ghKvSGYDYphY0Wa98m3B0AyJd868VKiYtJM5bQ0H7oEjRFky8H-ux/s320/unnamed.pngJ

Huenda umewahi kuliona na kulipita tu ama kutovutiwa na ladha yake ama kukereka na utomvu wake baada ya kula


Habari mbaya kwako ni kwamba umekosa kitu adimu na maridhawa sana......Hili ni moja ya matunda yanayochukuliwa kama MFALME WA MATUNDA (The King of Fruits) kwa kuwa na karibu vitamin vyote muhimu yaani A, B1, B2 na C..



Na sehemu zinazotumika ni majani, matunda, utomvu, mizizi na magamba. Na mfenesi unaweza kukua hadi kufikia kimo cha mita 20.........na nakusihi sana kuanzia leo ujitahidi kula walau punje tatu tu na ukiweza hata mbegu zake kwa kadri ya mada hii



Leo nimejikuta tu nafukunyua tunda hili baada ya kulikuta mahali fulani na jinsi watu walivyokuwa wanatua kilich cha thamani ndipo nilipoanza kugoogle nikakuta faida na hata hilo jina la lugha ya malkia huitwa Jackfruit




Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomithilika. Licha ya sifa hii, tunda hili linatajwa kuwa na faida lukuki endapo litaliwa na mwanadamu.



Hakuna anayejua vizuri asili ya mafenesi lakini inaaminika asili yake ni katika misitu ya mvua nyingi ya Magharibi ya ghats (western ghats). Lakini kwa sasa inalimwa katika nchi za india, Burma, Sri lanka, China, Malaya, East in indies, Qeens land, Maturities, Hawaii, Suriname, Brazil, Kenya, Uganda na Tanzania, Na nchini Tanzania hulimwa Pemba, Unguja, Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Tanga na Mbeya(Kyela) nk.




Kwanza, linatajwa kuwa na virutubisho kadha wa kadha vyenye kazi mbalimbali mwilini. Baadhi ya virutubisho hivyo ni pamoja na vitamini za aina mbalimbali, madini, protini, mafuta, uwanga na nyuzinyuz (fiber) ambazo husaidia kwenye mfumo wa mmeng'enyo na kuchagiza tatizo la kupata haja (constipation) na linasaidia pia kuzuiwa kuvimbiwa.



Fenesi pia linatajwa kuwa chanzo kizuri cha nishati kisichokuwa na lehemu (cholesterol). Si hivyo tu, bali pia ni chakula chenye virutubisho vya kuondosha sumu mwilini vinavyoweza kuukinga mwili dhidi ya saratani na magonjwa mengine kadha wa kadha,



Sukari ya Fenesi ni dawa ya sukari sumu mwilini kwa kuwa linasharabiwa taratibu mwilini na kufyonza sukari sumu na hii husaidia pia katika kuhibiti shinikizo la damu mwilini ( Jackfruit is more slowly absorbed into the bloodstream, which prevents sugar crashes, sugar cravings, and mood swings, They are well known because of its high potassium content. This helps the blood vessels relax and maintains proper blood pressure.)

kutoka michuzi Blog ambapo tunaambiwa habari hii imeandaliwa na ​ Geofrey Chambua ​kutoka vyanzo mbalimbali

No comments:

Post a Comment