WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Monday, November 6, 2017

Utata upya kifo cha balozi wa Libya nchini

Na. Mwandishi Wetu, - JAMVI LA HABARI

Mwanaharakati Philipo Mwakibinga ambaye ni Mratibu wa taasisi ya watetezi wa rasilimali wasio na mipaka maarufu WARAMI ambae pia amepata kuwa Rais katika serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha Dodoma UDOM ameibuka na kuibua maswala mazito yanayohusiana na diplomasia ya kimataifa na uchunguzi wa kipolisi kuhusiana na kifo cha aliyekuwa balozi wa Libya nchini Tanzania Ismail Nwairat ambaye taarifa zilitolewa zikisema kuwa amejiua kwa kujipiga risasi akiwa ofisini kwake jijini Dar es salaam tarehe 2 juni 2014.

https://static.pulse.ng/img/news/origs5539360/7990482043-w980-h640/60ac8257ba7a13919eb88fb5172907d897ea4869.jpg 
 Fayez al-Sarraj, Waziri Mkuu wa Libya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mwakibinga ameitaka serikali kupitia jeshi la polisi na vyombo vingine vya dola kufanya uchunguzi wa kina ili kujiridhisha na kuondoa utata unaoonekana kuvikabili vichwa vya wananchi wengi wa Libya waliopo hapa nchini ambao yeye anafahamiana nao

‘’mimi nina marafiki zangu kadhaa wa ki Libya, tangu kutokea kwa tukio lile mpaka leo kila siku wanasononeka kuhusiana na kifo cha balozi wao, na mimi wananitumia kama sample ya mwananchi ambae taifa langu limeshindwa kulinda uhai wa mwana diplomasia wao’’. Anasema Mwakibinga

‘’wanasema haiwaingii akilini na hata mimi hainiingii akilini mtu mzima mwenye hadhi ya kuwa balozi ajipige risasi akiwa ofisini kwake mchana kweupe…kwa maslahi mapana ya taifa langu na heshima yake kimataifa naviomba vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa kina juu ya swala hili’’. Aliongeza mwanaharakati huyo

Marehemu balozi Ismail Nwairat ambaye alikuwa anakaimu nafasi hiyo aliripotiwa kupoteza uhai wake kwa kujipiga risasi ofisini kwake.
Balozi huyo ambaye alikuwa anasifika kwa kutoficha msimamo wake wa kupingana na serikali iliyoondolewa madarakani ya hayati Kanal Muamar Gadafi kwa mapinduzi ya umma kwa kuiita ya kidikteta isiyojali wala kuheshimu haki za binaadam, kifo chake kilizua sintofahamu miongoni mwa wadau wengi wa masuala ya kidiplomasia ya kimataifa.

Taarifa ya kifo cha balozi huyo kufariki zilisema kuwa balozi huyo alijipiga risasi ya kifuani upande wa kushoto akiwa ofisini kwake.
Taarifa iliyotolewa na  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ilisema kuwa,  ilipokea taarifa kutoka kwenye Ubalozi huo kuwa aliyekuwa Kaimu Balozi wa Libya,  Ismail Nwairat amefariki dunia  kwa kujipiga risasi.

Hata hivyo ubalozi wa Libya ulisema  kuwa,  kifo hicho kilitokea majira ya saa 7 mchana ofisini kwa Kaimu Balozi huyo katika jengo la Ubalozi wa Libya. Na ilitaarifiwa kuwa  Nwairat alijifungia ofisini na kujifyatulia risasi kifuani upande wa kushoto.

“Maafisa ubalozi walivunja mlango waliposikia mlipuko wa bunduki na kumkuta Kaimu Balozi Nwairat ameanguka chini, walimkimbiza hospitali ya AMI Oysterbay ambako alitangazwa kuwa alikwisha kufariki na Polisi walithibitisha kifo hicho” ilisema taarifa hiyo.

No comments:

Post a Comment