WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, November 1, 2017

NYALANDU AZIDI KUNANGWA

Akumbushwa alivyoitwa waziri mzigo
·         wazee Singida wamtoa thamani
·         atuhumiwa kumkimbia kigwangala Ufisadi maliasili
·         yabainika hana cha kupoteza kibunge, kifamilia


Na Ibrahim Malinda

Baadhi ya wazee wa heshima mkoni Singida anakotokea ambako pia anatokea Lazaro Nyalandu ambaye amejivua uanachama wa chama cha mapinduzi hivi karibuni wamewata watanzania hasa wakazi wa mkoa huo kumpuuza mbunge huyo wa zamani kwa kusema kuwa kitendo chake alichokifanya si cha kiungwana na wala hakina uwezo wa kufanywa na watu wa asili ya mkoa huo
Mmoja wa wazee hao Shabani Mughwai amesema kuwa kama kweli Nyalandu alikuwa anataka kujiondoa na kubalki na heshima kwa wana singida kamwe asingeweza kwenda kufanyia tukio hilo mkoani arusha hata kama ni nchi moja.

‘’sasa yeye amekuwa mbunge wetu zaidi ya miaka 20, kilichomfanya ashindwe kujiuzulu akiwa hapa na kutueleza yaliyomsibu ili tujue nini cha kumsaidia kama wazee wake ni kipi..hana busara hata kidogo na ndio maana akaenda kujiuzulu akiwa arusha, tena hotelini lakini kama angekuwa na busara angekuja kujiuzulu hapa sasa tunaelewa kwanini katibu mkuu wake Kinana alimwita waziri mzigo’’, anasema Mughwai

 ‘’tunasikia kwamba ana uraia wa nchi mbili, kwamba yeye nusu mtanzania na nusu mtu wan chi nyingine, pengine ndio maana ameamua kutudharau sisi kwa sababu hana cha kupoteza hapa nchini na hata asipokuwa mwakilishi wetu bado ana uhakika wa kusafiri na kuishi nje ya nchi hata kama nchi yetu ikiingia kwenye machafuko.. tena mpaka watoto wake tunajua kuwa nao hawajazaliwa Tanzania. Tunamuombea mungu kwa hilo lakini tunamtaka asitufarakanishe’’. Aliongeza mzee huyo

Aiza mmoja wa ndugu wa karibu wa mbunge huyo wa zamani ambaye ameomba kutotajwa gazetini kwanza amesema kuwa mbunge huyo hastahili kupongezwa eti kaacha ulaji wa kujiuzulu ubunge badala yake hakuwa na cha kupoteza kwani tayari alishakopa mpaka sehemu ya kiinua mgongo chake
‘’Lazaro hakubakisha kitu, alikopea mshahara, posho , marupurupu mpaka na kiinua mgongo, kwa hiyo hakuna chochote anachopoteza zaidi ya kulitia hasara taifa kumlipia deni lake katika mabenki’’. Alsema

Juzi gazeti hili liliripoti kuwa aliyekuwa waziri wa Maliasili na Utalii aliyehudumu katika serikali ya awamu ya nne, Lazaro Nyalandu ambaye pia ni mwanachama wa muda mrefu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),  amejivua uanachama wa chama hicho na hivyo kupoteza nafasi zake zote ikiwemo ubunge wa Singida Kaskazini na Ujumbe wa Halmashauri Kuu(NEC) ya CCM.

Kitendo cha kujiondoa CCM kimeenda sambamba na kutoa rai kwa viongozi na wanachama wa CHADEMA kuwataka wafikirie kama itafaa kumpokea katika chama hicho ili aendeleze kile alichokiita kuendeleza Demokrasia na utawala wa sheria.

JAMVI LA HABARI limejulishwa kwamba Nyalandu hakuwa na namna zaidi ya kujiuzulu na kuhama chama kama sehemu ya kinga yake baada ya kujiona dhahiri kwamba haendani na kasi, dhamira, malengo , utashi na misimamo ya Rais na Mwenyekiti wa CCM Dk. John Pombe Magufuli ambaye mara zote amekuwa akitangaza hadharani kuwa hana mswalia mtume na aina yoyote ya viongozi wabadhirifu, wajanja wajanja na walioshiriki kulitia hasara taifa kwa namna yoyote ile.

Aidha, kitendo cha Nyalandu tangazo la kufuta vibali vyote vya uwindaji na kwamba serikali haitamchekea mtu yeyote hata kama alikuwa Waziri inasema kuwa ni miongoni mwa viashiria vya Nyalandu kuachia ngazi na kukimbilia Chadema.

Hivi karibuni CCM imekuwa ikisisitiza utaratibu wa kujiendesha chenyewe bila kutegemea ufadhili wa wanachama na wafanyabiashara na kusisitiza kutokuwepo kwa viongozi wenye vyeo zaidi ya kimoja na kuondoa kili kilichokuwa kikijengeka kama Umungu mtu ndani ya chama.

Taarifa zaidi zinasema kwamba kuondoka kwa nyalandu kunachagizwa na ukweli kwamba umri wake bado ni mdogo na ameshakaa jimboni kwake kwa zaidi ya vipindi vinne na hakuna jambo lolote la msingi aliloweza kulifanya kwa wananchi anaowaongoza na kujiona kuwa ameshachuja kisiasa hivyo kuamua kwake kuhama chama kutamsaidia kurudisha mvuto alioupoteza jimboni humo.

"Kaka asikudanganye mtu, Lazaro huku kwetu zama zake zilishapita, na hata mwaka juzi ni heshima tu ya yeye kugombea Urais ndio iliyomfanya ashinde ubunge, lakini 2020 hata angegombea udiwani kama Mimi asingeshinda, amechuja mno". Alisema Diwani mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa.

"" unajua siasa ni mahesabu, sasa huyu bwana kila akipiga hesabu zake anaona hazilipi na zisingelipa kweli. Angefanyaje zaidi ya kuhama na Rais wetu hataki utani na wawakilishi wa aina yake?"". aliongeza

Diwani huyo aliongeza zaidi kuwa ni kwa sababu tu Nyalandu hana aibu, lakini kama angekuwa na aibu asingeweza kujipeleka Chadema chama ambacho kimekuwa kikimtuhumu kila uchao kipindi akiwa waziri kuwa anahusika na ubadhilifu katika sekta hiyo.

"Unakumbuka maneno ya Peter Msigwa kuwa Nyalandu anafadhili ujangili na ubadhirifu katika vitalu?, sasa kwa tabia ya Chadema na unafiki wao nao watamsafisha kama walivyomsafisha Edward Lowassa, . Nyalandu alitakiwa atoe majibu ya tuhuma za Msigwa kwanza kabla hajapokelewa". Aliongeza

Alipoulizwa na Gazeti hili atoe maoni yake juu ya kitendo cha Nyalandu, Mwanaharakati na Mwenyekiti wa CCM tawi la mtoni Bokorani, Joseph Yona alisema kuwa watu aina ya Nyalandu ni wa kuwaogopa kama ukoma

"Mtu yeyote mwenye akili timamu kama mimi na wewe ataelewa kuwa Nyalandu anahangaikia tumbo lake, CCM aliyoihudumu kama waziri ndio ile ile anayoilaumu leo na kutangaza kuihama, tofauti ni kuwa kipindi anahudumu alikuwa anaiona inafaa na ina maana, Leo hayupo serikalini anaiona haina tena thamani, huyu ni mganga njaa tu hana lolote". Alisema 

" ningemuona mwanaume wa kweli kama angehama kabla ya Rais kukamilisha uteuzi wa mara ya pili wa baraza lake la mawaziri, lakini kasikilizia weee, kaona hayumo na imebaki miaka michache na uwezekano wa kupata nafasi hana amejidai kuhama, awadanganye hao hao Chadema waliozoea mizoga ya kisiasa sio sisi timamu". Aliongeza Yona

Aidha, katika mitandao ya kijamii kumekuwa na mijadala mikubwa kuzungumzia kuhama kwa waziri huyo wa zamani huku taarifa zikielezwa kuwa wiki iliyopita Waziri wa Maliasili na Utalii, Dr. Hamisi Kigwangalla, akizungumza na wadau wa Wizara yake alisema kuwa baadhi ya mawaziri na wabunge wa awamu ya nne wangepaswa kuwa jela kwa ufisadi na ushiriki wao kwenye ujangili. Leo Nyalandu amekimbia. Ifuatayo ni historia ya kashfa moja ya Nyalandu. 

Kampuni ya Kimarekani ya Friedkin Conservation Fund (FCF) ambayo inamiliki kampuni tanzu za uwindaji wa kitalii za Mwiba Holdings Ltd, Tanzania Game Trackers Safaris (TGTS) ni miongoni mwa watuhumiwa wa ujangili
Uchunguzi unaonesha kumekuwapo matukio kadhaa ya wafanyakazi wa Mwiba kukamatwa wakiwa wameua wanyamapori na kukutwa na nyara za Serikali.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii vimesema mara zote kesi zinazoihusu kampuni hizo zimekwama kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni urafiki wao wa karibu na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Nyalandu.

Urafiki wa Nyalandu na wamiliki wa kampuni hizo ulikuwa mkubwa kiasi cha kumpatia moja ya helikopta zake aitumie kwenye mbio za kuwania urais, kabla ya kushindwa na kujielekeza kwenye ubunge.

Helikopta ya kampuni hiyo ndiyo aliyoitumia wakati wote wa kampeni zake za ubunge
Nyalandu alimwamuru Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa wakati huo, Paul Sarakikya, kutoa Leseni ya Rais kwa familia ya Tom Friedkin (mmiliki wa kampuni hizi) kuwinda wanyamapori 700 katika vitalu vinane na eneo la wazi la Makao. Leseni hizo zilitolewa bure bila kulipiwa hata senti.

Miongoni mwa wanyamapori waliokuwa kwenye orodha ya kuuawa ni tembo walio katika hatari ya kutoweka.

Pia Nyalandu alikiuka sheria kwa kupuuza ukomo wa idadi ya vitalu vitano kwa kampuni moja. TGTS imemilikishwa vitalu vinane pamoja na eneo la wazi; hali ambayo ni ukiukwaji wa kifungu cha 38(7) cha Sheria ya Wanyamapori.

Kampuni hiyo pia ilipewa vitalu na Nyalandu kinyemela, ilhali sheria ikiagiza kuwa kitalu kinapobaki wazi sharti kitangazwe kwanza na waombaji washindanishwe katika mfumo na utaratibu ulio wa haki na uwazi [Kanuni ya Uwindaji wa Kitalii 18(1).

Pamoja na kutoa Leseni ya Rais, Wamarekani hao walileta watoto wadogo, chini ya umri wa miaka 18 kuwinda; jambo ambalo ni kinyume cha kifungu cha 43(3) cha Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009.

FCF na kampuni tanzu imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama (Makao Ranch).

Kampuni ya Mwiba Holdings Ltd chini ya TGTS Ltd ambazo zinamilikiwa na Friedkin Conservation Fund (FCF) imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama.

Hata baada ya kumalizika Mkataba wake na JUHIWAPOMA, kampuni ya Mwiba Holdings Ltd iling’ang’ania na kuendelea kukalia eneo la Makao WMA kwa mabavu na kinyume cha sheria.

No comments:

Post a Comment