WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Friday, September 30, 2016

DIAMOND PLATNUMZ AIPASHA MAKAVU SERIKALI YA MAGUFULI

 http://expressng.com/wp-content/uploads/2015/09/diamond-platnumz111.png
Diambond Platnumz.
Msanii Diamond Platnumz ambaye ameshiriki kukifanyia kampeni chama cha mapinduzi katika chaguzi mbili mfululizo, wiki hii amefunguka kuhusiana na serikali ya chama hicho na kuitaka isijisahau hasa kuwasahau watu walioshiriki kuhakikisha inakaa madarakani na kuboresha miundombinu ya maeneo mbalimbali na kuacha kupendelea maeneo maalum tu jijini Dar es salaam.

Akihojiwa katika kipindi cha kijamii cha The weekend chat show cha Clouds Tv, Diamond Platnumz msanii maarufu nchini Tanzania ameonyesha kusikitishwa kwake na kitendo cha serikali kushindwa kutengeneza barabara za maeneo ya wanaoishi watu wa kawaida kama temeke, tandale na kwake madale tegeta na badala yake wanaendelea kutengeneza kila siku maeneo yanayosemekana kuwa ni daraja la kwanza na kuwasahau watanzania wengine.

''unajua mtu umeshiriki kuhamasisha watu ili chama fulani kishinde, lakini mwisho wa siku mambo yanayokuhusu hayatiliwi uzito, inazinguaga sana''. alisema msanii huyo.

''unajua mimi ninapoishi tegeta kule barabara mbovu sana, kila siku wanaweka udongo wanatoa wanaweka wanatoa, tunaharibu shock ups tu, ukizingatia tumeshiriki kunadi chama kuwashawishi watu wachague halafu mambo yatakuwa mazuri lakini hamna, inazingua sana kwa hiyi kama ningekuwa waziri wa miundombinu ningehakikisha barabara zinatengemaa maeneo yote''. aliongea msanii huyo

MAANDALIZI YA UPANDAJI MITI YAZIDI KUPAMBA MOTO

MULIKA TV SHOW. KARIAKOO MARKET/ LIFAHAMU SOKO KUU LA KARIAKOO MULIKA KA...



kipindi cha Mulika kinachoandaliwa na TETERE MEDIA kinazidi kukupa
uhondo wa kufahamu na kuyamulika mambo mbali mbali kwa undani. safari
hii wametuwekea tena SOKO KUU LA KARIAKOO soko maarufu kuliko masoko
yote Tanzania.



hebu pata nafasi ya kutazama soko hili
ili uweze kujua limeanza lini, limeanzishwa na nani, limebuniwa na nani
na kwanini linaitwa soko la kariakoo.


KAGAME AMZIDI KETE MAGUFULI

siku chache baada ya Tanzania kuzindua ndege zake mbili za Bombadier Q400

Rwanda yanunua ndege ya kisasa ya Airbus yenye uwezo wa kubeba abiria 244

 http://america.aljazeera.com/content/ajam/articles/2015/12/16/paul-kagame-rwandas-president-for-life/jcr:content/mainpar/adaptiveimage/src.adapt.960.high.kagame_thumb.1450275953330.jpg     Rais wa Rwanda Paul Kagame

http://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/0010/production/_91461000_4.jpg 

Shirika la ndege la Rwanda, Rwandair, limezidisha ushindani katika uchukuzi wa ndege Afrika Mashariki na Kati kwa kununua ndege aina ya Airbus A300-200.
Ndege hiyo itawezesha shirika hilo kufika masoko ya Ulaya na bara Asia.
Ndege hiyo ilizinduliwa kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wa kimataifa wa Kanombe, Kigali.

 Mkuu wa shirika la Rwandair John Mirenge amewaambia waandishi wa habari kuwa ndege hiyo yenye nafasi ya abiria 244 ndiyo ya kwanza katika ukanda huu na ina teknolojia ya kisasa na ya hali ya juu.

"Ukiwa angani ndani ya ndege hii unaweza kupiga simu, kupata ujumbe wako wa simu, ujumbe wa barua pepe, ujumbe wa WhatsApp na mawasiliano mengine. Haya hayakuwepo katika ndege nyingine tulizo nazo," amesema.
"Hata katika ukanda huu na kwingineko barani afrika hakuna shirika lenye ndege iliyo na uwezo huo."

 http://ichef-1.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/57F4/production/_91461522_img_9684.jpg
Ni ndege iliyotengenezwa nchini Ufaransa na kununuliwa kwa kitita cha dolla milioni 200 za marekani.

Bw Mirenge, anasema safari za shirika la ndege la Rwandair zilikuwa zinajikita sana Afrika magharibi na kati na kwamba ndege hii sasa inakuja kuongeza uwezo wa kuvamia masoko ya Ulaya, Asia na kusini mwa Afrika.
Safari ya kwanza ya ndege hiyo inatarajiwa kufanyika wikendi ijayo tarehe 8 kuelekea mjini Dubai.
Shirika hilo sasa linalenga kusafirisha abiria laki 750 ifikapo mwishoni mwa mwaka

MULIKA TV SHOW : UFAHAMU UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM












Huu hapa uwanja wa Taifa wa Daresalaam.



ni kipindi kipya cha luninga kinachozungumzia masuala mbalimbali kwa undani. karibu ujionee

SIRI ZAIDI ZAVUJA KIBURI CHA PROF. LIPUMBA CUF HIKI HAPA






http://dar24.com/wp-content/uploads/2015/08/Lipumba-02.jpg
Mwenyekiti wa Taifa wa  CUF Profesa Ibrahim Lipumba .

kile kinachoonekana kumpa nguvu ya kuendelea kuwa mwenyekiti wa CUF licha ya songongombingo zinazoendeshwa dhidi yake ni kutokufuatwa kwa katiba ya chama hicho utafiti wa Jamvi la Habari umebaini.

pamoja na kutokufuatwa kwa ibara ya 171 ya chama hicho inayomuhitaji kiongozi kukubaliwa kujiuzulu kwake na mkutano ama kikao kilichomchagua, lakini pia ibara ya 77 (7) ya chama hicho inambeba zaidi na kuwanyima utetezi upande unaompinga.

soma mwenyewe hapa.

bara 77 (7)

NUKUU :
Maamuzi muhimu yatahesabiwa kuwa maamuzi halali ya Mkutano mkuu wa Taifa ikiwa zaidi ya theluthi mbili (2/3) ya wajumbe kutoka Tanzania Bara waliohudhuria. Na zaidi ya theluthi mbili (2/3) ya wajumbe kutoka Zanzibar waliohudhuria watayaunga mkono maamuzi hayo.
Ibara ya 77 (8)
NUKUU :
Kwa madhumuni ya Kifungu cha (7) cha Kifungu hiki maamuzi muhimu ni pamoja na :-
(a) Kuvunja Chama.
(b) Kubadilisha Jina la Chama.
(c) Kuunganisha Chama na Chama au vyama vya Siasa vingine.
(d) Kuwasimamisha , Kuwaachisha au Kuwafukuza uongozi na / au uwanachama viongozi wakuu wa kitaifa wa chama pamoja na viongozi wa kitaifa kama ilivyoainishwa ndani ya katiba hii.
(d) Kuwaachisha , Kuwafukuza uwanachama Rais na /au Makamu Rais wa Jamuhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar anayetokana na Chama.
(f) Kupitisha , Kurekebisha au Kubadilisha katiba hii au Kifungu chochote cha katiba hii.
(g) Kupitisha , Kurekebisha au Kubadilisha itikadi ya Chama.
(h) Mambo mengine yoyote ambayo Mkutano Mkuu wa Taifa kwa masharti yale yale ya Kifungu cha (7) cha kifungu hiki utaamuwa kuwa ni maamuzi muhimu.

BREAKING NEWS: MBOWE AVUNJA UKUTA RASMI, AMSHUTUMU LIPUMBA MGOGORO CUF, AMVAA MSAJILI WA VYAMA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJybtHVKNQr92fEISYPG5rC3CEftsoCs85PHbFPof6crt10MclrvdwBkcBGP8N2qjKPf3rqdTyw8hRoxMhln4Ifd9wDTwdIsBW-Y1G0p197qzpFyB-eQZIRa12Jc49sLchnzL1q3NjM41v/s640/mbowe.jpg
Mwanachama wa Chadema Ben Saa nane ameandika taarifa hizi katika mtandao wa Jamii forums.
 akiripoti mkutano wa Mbowe na waandishi wa habari uliofanyika leo tarehe 30.09.2016 katika makao makuu ya chama hicho kinondoni ufipa.

-Tayari Waandishi wa Habari wameketi
-Viongozi wakuu Wakiongozwa na Mhe.Freeman Mbowe wanaingia Ukumbini

Hotuba kwa Taifa itaanza hivi Punde

Saa 12:15 baada ya İtifaki kuzingatiwa, Mwenyekiti Taifa anaanza kuhutubia
Anawapa pongezi wanahabari kwa kufika kwa wingi .Anasema

- Jana kamati ndogo ya kamati kuu imekutana tena ili kufanya marejeo kuhusu yalipofika majadiliano ya Viongozi wa Dini na Rais baada ya kukiomba Chama kisitishe Operesheni UKUTA

-Hadi jana na hadi sasa viongozi wa Dini hawajaleta Taarifa yoyote kuhusu kama waliweza kukutana na Rais

-Sisi kama Chama Cha Siasa tumetekeleza wajibu wetu
-Tunawaheshimu viongozi wa Dini na Tutaendelea kuwaheshim
-Sasa kama chama cha Siasa tutaendelea sasa kutekeleza wajibu wetu

-Kazi ya siasa sio kazi ya siku moja.Tutaifanya kazi hii endelevu ya kupambana na Utawala kandamizi unaowaumiza wananchi kwa kukanyaga sheria na katiba na pia utawala unaokwepa wajibu wake lakini hautaki kukosolewa.

Maisha magumu kwa Watanzani lakini Mtawala asiye na Mbinu mbadala hataki wananchi wapaze sauti

-UKUTA ni Fikra. Yaani fikra za kupambana na ukandamizaji wa haki na demokrasia.Mapambano haya hayahusishi CHADEMA pekee.

Kwa muktadha huu tuna wajibu wa kufanya siasa ndani ya wigo uliowekwa nchini na pia kimataifa

-Tanzania sio kisiwa.Ndio maana chama kiliona Umuhimu wa kutuma ujumbe Mzito kwenye ziara maalumu nchi za Ulaya .Nchi za Ujerumani na Denmark kuendelea kuujulisha Ulimwengu juu ya ukandamizaji mkubwa wa haki za binadamu na Demokrasia kinyume na jinsi ambavyo serikali imekua ikijipamba kuwa ya amani na Utulivu

Hiyo ilikua ziara ya awamu ya kwanza
Bado Ujumbe Mwingine utatumwa kwenye nchi nyingine kama Uingereza,Marekani,Canada , Malaysia,Japan na hata ndani ya Umoja wa Afrika na kwenye mtangamano wa kikanda kama SADC na EAC

Tunataka utawala ujue mipaka yetu haiishii Namanga na Tunduma
Tutatumia Taasisi za kimataifa
Kurugenzi yetu ya Sheria inaendelea na kazi nzuri ya kutumia Mahakama za ndani na za kimataifa kupeleka mashauri yetu

-Viongozi wetu mbalimbali wanakabiliwa na kesi mbalimbali zinazoitwa kesi za Uchochezi

-Tumesikia Juzi polisi katika kujihalalishia uovu wao walipojua CCM sasa wanakaribia kuanza vikao vya ndani wanatangaza kuruhusu Mikutano ya ndani

-Sisi tunaandaa mikutano ya kisiasa nchi nzima
-Ukuta wa Oktoba Mosi utasogezwa mbele kwa Tarehe Maalumu
-Rais anatumia jeshi kupambana na Sisi lakini hakuweza kuwatumia kwenye Tetemeko Kagera na kuwaacha raia wetu wakiteseka
-Leo anatumia jeshi kuumiza Raia na vituko vingine eti kufagia na wengine kupanda Miti

-Rais aliyekwepa mikutano ya kimataifa kwa kisingizio cha Tetemeko la Ardhi Kagera hakufika,Hakupeleka jeshi ila alikaa İkulu akisubiri Ripoti

MİGOGORO İNAYOPANDİKİZWA
-Prof.Lipumba amekituhumu CHADEMA kuhusika na migogoro ndani ya CUF
Sikusudii kumjadili Lipumba.Maana sitaki kumpa nafasi na umuhimu aliokuwa nao zamani
He's politically İrrelevant.

CHADEMA kitashirikiana na chama chochote chenye dhamira ya dhati
CUF tunaheshimu maamuzi yao ya vikao halali

-Natoa Rai kwa Wanachama wa CHADEMA nchi Nzima kupuuza kauli za Prof.Lipumba na tuache kumpa ushirikiano wowote kwa kuwa ni msaliti wa mageuzi anayetafuta kuangamiza Upinzani

MSAJİLİ WA VYAMA VYA SİASA



-Jaji Mutungi amechochea mgogoro CUF na hatuna sababu za kumuheshimu
-Atambue kuwa tutasimama na CUF na ajue yeye sio Msajili wa kwanza.

Mbinu zake na Watawala zitashindwa
-Serikali inatumia nguvu kubwa sana na taasisi nyingine kununuliwa

-Kwa mfano TWAWEZA .Upo ushahidi kuwa walipewa pesa na serikali kupika Utafiti siku moja kabla ya UKUTA kwa bahati mbaya hawakupika kwa kiwango cha kuifanya ripoti ionekane kuwa na sifa za kiutafiti

-Kwa hiyo ndugu wanahabari sisi kama Chama tumebadilisha Tarehe ya kuanza Kufanya maandamano na mikutano

Sasa wale walojiandaa kushambulia na kuua watu wasubiri
Sisi tunabadili mbinu tukihusisha mbinu za kimapambano na kidiplomasia

-Mmeona matokeo ya Mbinu hizi sasa Jumuiya ya Kimataifa imeanza kuona ukandamizaji wa Demokrasia nchini na Udikteta Uchwara ulioshamiri

Tulipowapa Muda viongozi wa Dini wao watawala walidhani tumelala kumbe tumevuka mipaka na kuingia anga za kimataifa

-Sasa serikali inahaha na kutapatapa baada ya kushitakiwa kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa
Sasa tutaendelea kufanya vikao vya kimkakati nchi nzima na pia mikutano
Tutaendelea kuhabarishana kadiri tunavyopiga hatua katika maandalizi na Mikakati yetu ambayo haitawapa fursa watawala kujipanga

Asanteni


Mwisho:Sasa Mwenyekiti Taifa na Viongozi wakuu anaongea na Baadhi ya Vyombo vya Habari vya Kimataifa kisha ataelekea kwenye kikao nyeti cha Ndani,Kikao cha Kimkakati

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHAMIA RASMI DODOMA


Thursday, September 29, 2016

TULIWAHI ANDIKA : LIPUMBA SEIF NGOMA NZITO

BILIONI 415 ZAPOTEA UDOM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjh-n1dokVEqJIGXG_qIQaQu4ii198wS4WDbB7Mbxz6oA0rEk-Z1hPn3dGiAvmjj7lUbfyC-betA5omxnDpUIPOBzJ2KUGv66_zbcbYeEV9UIyegI77L8v-teTa53UzaU8TmYqUTgmW50go/s1600/1.jpg 


na mwandishi wetu.

Ni kama Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, anakibarua kizito kunusuru upotevu unaoweza kujitokeza wa usimamizi wa mali za chuo kikuu cha Dodoma  zenye thamani ya  zaidi ya shilingi bilioni 400  taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali,CAG ya mwaka 2014/2015 inaeleza.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa serikali kupitia mashirika ya mifuko ya hifadhi za jamii ilijenga chuo hicho kikuu kikubwa kuliko vyote katika ukanda huu wa afrika mashariki kwa mkataba wa ujenzi,ubunifu, umiliki na uendeshaji wa pamoja na kwamba baada ya kukamilika mali za chuo hicho zilitakiwa kumilikiwa na mashirika hayo ndani ya miaka kumi lakini mpaka taarifa hiyo inatoka jambo hilo halikuwa limefanyika.

‘’Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Pensheni kwa Wafanyakazi wa Umma (PSPF), Mfuko wa Pensheni kwa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF), Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) na Mfuko wa Pensheni wa PPF yalitumia jumla ya Shilingi bilioni 415.4 kujenga Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), chini ya makubaliano ya buni, jenga, endesha, na kisha hamisha miliki baada ya miaka kumi (10)’’.  Inasema sehemu ya taarifa hiyo ya CAG

Totauti na ilivyotarajiwa, taarifa hiyo inasema kwamba mpaka sasa majengo hayo hayajaingizwa kwenye kumbukumbu za  chuo hicho wala mashirika hayo na hivyo kuhatarisha upotevu wake,

‘’Majengo haya hayapo kwenye vitabu vya Chuo Kikuu cha Dodoma wala katika vitabu vya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii husika. Japokuwa Mlipaji Mkuu wa Serikali amejibu kuwa majengo haya yataingizwa kwenye vitabu vya Chuo Kikuu cha Dodoma katika mwaka wa fedha wa 2013/2014, bado UDOM imepewa Hati Yenye Mashaka kutokana na kutokuwepo kwa majengo hayo kwenye vitabu vyake.’’ Imeongeza taarifa hiyo
 Kufuatia uchunguzi huo, mdhibiti na mkaguzi mkuu huyo wa serikali anaendelea kusisitiza umuhimu wa majengo hayo kuingizwa kwenye vitabu vya chuo hicho cha UDOM kama alivyopendekeza awali ili kukiondolea chuo hicho shaka ya kuendelea kutopata hati safi.

Hayo yanatokea huku kukiwa na msuguano wa chinichini baina ya wafanyakazi wa taasisi mbalimbali hapa nchini na serikali juu ya swala la Fao la kujitoa ambapo serikali imebadili sharia ili kuzuia fao hilo.

Sambamba na hilo la fao la kujitoa, wachambuzi wa mambo wanasisitiza kuwa kuna haja ya serikali kusimamia sawa sawa faida zinazotakiwa kutokana na ujenzi wa chuo hicho kwa kuwa ujenzi wake umetokana na fedha za watanzania na hivyo wafanye kila linalowezekana kukamilisha umiliki huo wa mali ili kuhakiki ulinzi wa pesa zao.

‘’unajua kibiashara, UDOM ni uwekezaji wa pesa zetu, sasa na kila uwekezaji lazima uzalishe faida, na kama mpaka sasa hawajakamilisha umilikishaji wa mali hizo kwa mashirika yetu maana yake uwekezaji huo hautatulipa na pesa zetu zitapote bure, serikali inatakiwa ichukue hatua za makusudi kwenye hilo’’. Alisema Omari kihampa mwanachama wa moja ya mifuko ya hifadhi za taifa.

‘’bilioni 415 ni nyingi sana aisee, pamoja na kuipongeza serikali kujenga chuo kupitia fedha zetu lakini lazima fedha hizo zituhakikishie usalama wetu tukistahafu, kuacha kuendelea hivi ilivyo itakuwa ni kuzipoteza’’. Ananukuliwa Mariam Jamlisheed mtumishi wa wizara moja hapa nchini.

Gazeti hili linaendelea na jitihada za kuutafuta uongozi wa chuo hicho kuona mpaka sasa ni hatua gani wamechukua kuhusiana na suala hilo linalopelekea chuo cha Dodoma kukosa mmikili halali mpaka sasa

MHANDISI URAMBO MIKONONI MWA WAZIRI SIMBACHAWENE



http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/SIMBAW.jpg 
waziri wa TAMISEMI George Simbachawene
Na Mwandishi wetu
Waziri wan chi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa mheshimiwa George Simbachawene ametakiwa kuingilia kati tabia za baadhi ya watendaji wa halimashauri mbalimbali hapa nchini kutokana na watendaji hao kulalamikiwa kutokusimamia sharia katika masuala kadhaa hasa yanayohusu manunuzi na kusababisha mgogoro na mgongano wa kimaslahi kunakopelekea kudorora kwa utolewaji wa huduma za msingi za kijamii na maendeleo.
Akizungumza na gazeti hili mmoja wa watumishi wa wizara hiyo ameshauri kuwa ni vema suala hilo akaachiwa waziri mwenyewe kwa sababu yeye ndie msimamizi wa moja kwa moja wa wizara hiyo na kwamba maamuzi yake ndio huwa ya mwisho na akiamua kuchukua nidhamu kwa muhusika wala haitazuilika.
Kadharika madiwani kadhaa wa halimashauri ya wilaya urambo ambapo wiki iliyopita gazeti hili lilitipoti kuhusiana na kadhia ya mhandisi mkuu wa ujenzi wa wilaya hiyo kujihusisha na tabia zinazoendana ama kuonekana kukiuka taratibu za kimanunuzi na ukiukwaji wa sharia wa wazi.
‘’sisi kwenye kikao tutamjadili na kuliazimia swala lake, lakini pia tutamtaka waziri simbachawene amuwajibishe haraka iwezekanavyo, maana sina imani kama mkurugenzi anaweza kutengua nafasi yake’’. Alisema diwani mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa
‘’unajua huyu bwana alishawahi kufikishwa mpaka Takukuru kuhusiana na masuala hayahaya, lakini inaonyesha kwamba ama amenogewa ama amewazidi ujanja hao mambwana wa Takukuru, hivyo Simachawene anaweza kutusaidia kabisa kabisa kumalizana na huyu bwana’’, aliongeza diwani huyo
Hayo yanatokea wakati wiki iliyopita gazeti hili lilipoti kuhusiana na kuwepo kwa tafiti  zikimuonyesha Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuwa kiongozi anayependwa zaidi na wananchi wake hasa kutokana na tabia yake ya kusimamia sawa sawa sheria na kutumbua majipu kwa kuwaondoa wabadhilifu serikalini na katika taasisi mbalimbali za umma,baadhi ya wasaidizi wake katika ngazi za halimashauri wanaweza kumkwamisha kutokana kutokusoma alama za nyakati hasa katika kipindi hiki cha utawala wa awamu ya tano wenye kauli mbiu ya hapa kazi tu.
Tuhuma nzito za mgogoro wa kimaslahi zinamkabili  Mhandisi mkuu wa halimashauri ya wilaya urambo mkoani tabora bwana Makori Kisare zikimuhusisha na kujilipa mamilioni ya shilingi kupitia kampuni ambayo inahusishwa naye kuwa mbia ya  Mispa Constraction Co. Ltd yenye makao yake makuu mkoani mara.
Taarifa za uhakika ambazo gazeti limezipata zinasema kuwa mhandisi huyo wa wilaya amekuwa akiisababishia hasara serikali kwa kupokea kazi zilizofanywa chini ya kiwango kutokana na tabia yake ya kuitumia kampuni yake hiyo kuomba kazi ambazo yeye mwenyewe anashiriki kuziandaa na kuzitangaza na hatimaye kampuni yake hiyo kushinda zabuni hizo hivyo kuingia katika mgogoro wa kimaslahi.
Taarifa hizo zinasema kuwa kampuni yake hiyo  iliyosajiliwa tarehe 22 mwezi wa tisa mwaka 2010 ikiwa na namba ya usajili74055 ya sanduku la barua 669 musoma mkoani mara, mpaka sasa imekuwa ikifanya kazi katika maeneo kadhaa hapa nchini hasa katika halimashauri ambazo ama amewahi kufanya kazi au ana maswahiba zake wanaofanya kazi hapo, mifano ikiwa ni  halimashauri za urambo na Dodoma na
Jamvi la habari linaweza kuthibitisha kuwa, mhandisi huyo baada ya Kuteuliwa kuwa Mhandisi ujenzi Wilaya ya Urambo alianza jipatia kazi kupitia Kampuni hiyo kwa kutumia cheo chake cha ukuu wa Idara ya Ujenzi, jambo linalosababisha kukosekana kwa ufanisi na uwajibikaji kwa kuwa muwajibishaji ndie anayefanya kazi.
Baadhi ya miradi ambayo hata hivyo imeonyeshwa kufanywa chini ya kiwango ni  ule wa ujenzi wa mitaro uliopo  Urambo mjini wenye thamani ya Shilingi Milion Sabini na tano (75million) na kuendelea kujipatia kazi nyingine ya matengenezo ya Barabara kuelekea standi mpya yenye thamani ya Milion themanini na tano (85million).
Sambamba na hayo mhandisi huyo analalamikiwa na baadhi ya wasaidizi wa idara yake katika halimashauri hiyo kwa  kuipendelea wazi wazi kampuni yake huku akijua navunha utaratibu na taratibu za manunuzi zinazoelekeza kwamba inapokuwa walioomba kazi wengi wanasifa zinazofanana, basi aliyeomba kwa kiwango cha chini cha malipo ndiye atapaswa kupewa kazi hiyo, na kinyume chake ameamua kujipa kazi huku kampuni yake ikiwa imependekeza gharama kubwa.
Akizungumza kwa ombi la kutoandikwa gazetini mmoja wa watendaji wa ofisi hiyo amesema anashangaa kuona mabadiliko haya ya kiutendaji tangu kuingia kwa mkuu huyo mpya wa idara.
‘’Hebu fikiria, katika mradi wa  kazi ya utengenezaji wa Barabara na mitaro ya Urambo mjini (Majengo ya Tabora) ilitender kwa Shilingi milioni Miamoja na Tisini na Tisa (199million) na wakati nyingine zalitenda  kwa milion miamoja sabini na tatu (173million) na kwa milioni miamoja na themanini (180million), lakini aliamua kujipa yeye kazi hiyo licha ya kwamba gharama zake zipo juu’’. Alisema
‘’akikupenda bossi, au kama unakula naye vizuri wala hupati shida, ona alivyowapa kazi marafiki zake wa wengine Nebrix japo wameshindwa kufikia kiwango’’ aliongeza
Taarifa zinaonyesha kwamba  Mhandisi huyo anatuhumiwa kutokuzingatia sharia wala kanuni za manunuzi na kwamba mfano wa zabuni ya za Kuweka vifaa vya Maabara aliamuru apewe Nebrix Ltd  kazi ambayo kwa kiwango kikubwa imeshindwa kufainya  vema kwa kupasuka pasuka kwa mipira ya gas na maji ( Value for Money) lakini licha ya hayo aliendelea kuipatia kampuni ya hiyo miradi yote ya Wilaya ya Urambo huku wadadisi mambo wa halmashauri husika wakivujisha kwamba kampuni hiyo ilitumika kama daraja la yeye kujikwapulia fedha hizo, na hata wazabuni wengine walipo omba kazi hizo walikataliwa na akapewa mtu mmoja kwa Wilaya nzima.
Alipotafutwa na gazeti hili kupitia namba yake ya simu yake ya mkononi ambayo pia inaonekana kwenye taarifa za wasifu wa kampuni hiyo, mhandisi huyo amekanusha kuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo na kwamba alitoka huko miaka kadhaa nyuma na sasa sio tena muhusika.
‘’kuhusu mispa kama mispa kwanza sikuwa mmiliki, nilikuwa mshauri tu, mimi nilikuwa mmiliki wa kampuni nyingine kabisa ila mispa nilikuwa mshauri tu wa masuala mbalimbali na kwa sasa sina uhusiano nayo’’. Alinukuliwa bwana Makori.
Kupatikana kwa majibu hayo ya bwana makori kunaibua maswali kadhaa ikiwemo ya kwamba Mispa ilijua kwamba makori ndie mkuu wa idara ya ujenzi wa wilaya ya urambo na wakati anaipatia kazi alikuwa anajua au hajui kama ile ni kampuni anayodai kuwahi kuwa mshauri wake na kama alitangaza maslahi yake popote.
‘’Mkuu ameshawahi kubadilisha vipuli vizima vya magari ya serikari na kuviuza kwa bei ya chini  kwa rafiki zake na kuweka vipuli vibovu ambavyo baada ya siku chache hufa kabisa na kuandikia madokezo ili vinunuliwe vingine, tukio ambalo pia limewahi kutokea katika halimashauri jirani ya kaliua ambapo liliwahi kukamatwa fulushi likwa na Engine mbovu ya Land Cruizer amboyo ilikua ipo tayari kubadilishwa, hilo lilishuhudiwa na watumishi kazaa ila Mkurugenzi alie kuwepo ambae sasa amehamishiwa Jijini Arusha ambapo  aliamua kulizima suala hilo, huu ni kama ugonjwa wa kila halimashauri hapa nchini’’.
Malalamiko kama haya ya urambo, yanasemwa kuwa ndio tabia ya watendaji na watumishi wa serikali na mashirika ya umma wa maeneo mengi (gazeti hili linayo mifano mingi) na kwamba kazi nyingi zinazotangazwa hutangazwa tu kugelesha lakini kampuni zao wenyewe na ambazo nyingine hazina hata ofisi hupewa kazi hizo na kusababisha ufanisi wa chini ya kiwango.
Juhudi za kumtafuta mkuu wa mkoa wa tabora mheshimiwa Agrey Mwanri kulizungumzia suala hilo zinaendelea na na katika kumsaidi na kuunga mkono jitihada za Rais Dk. John Pombe Magufuli kurudisha nidhamu serikalini na kuwafikishia watanzania maendeleo kwa kuwapatia huduma zinazostahili kwa wakati bili upendeleo, gazeti hili litaendelea kuujulisha umma hatua kwa hatua kuhusiana na jambo hilo na mengine yanayofanana na hili..




Uingereza yawachangia wana Kagera bilioni sita

http://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/12F5D/production/_91416677_1.jpg
 Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Sarah Catherine Cooke, akimkabidhi Rais John Magufuli mchango wa Shilingi Bilioni 6 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa miundombinu ya shule zilizopata madhara kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea katika Mkoa wa Kagera.


Uingereza imetoa mchango wa Shilingi Bilioni 6 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa miundombinu ya shule zilizopata madhara kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea katika Mkoa wa Kagera tarehe 10 Septemba, 2016.

Mchango wa fedha hizo umewasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Balozi wa Uingereza hapa nchini Mhe. Sarah Catherine Cooke, Ikulu Jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya Balozi huyo kuwasilisha hati zake za utambulisho.
Balozi Sarah Catherine Cooke amemueleza Rais Magufuli kuwa pamoja na kutoa mchango wa fedha hizo Waziri Mkuu wa Uingereza Mhe. Theresa May anatoa pole kwa Serikali ya Tanzania na kwa familia zote zilizopatwa na madhara ya tetemeko hilo na kwamba Uingereza imeona ishirikiane na Tanzania katika kukabiliana na madhara hayo.

"Uingereza imeguswa sana na maafa yaliyowakumba wananchi kufuatia tetemeko lililotokea Kagera, tunapenda kuona wananchi wanasaidiwa na wanafunzi wanaendelea na masomo" amesema Balozi Sarah Catherine Cooke.

Kwa Upande wake Rais Magufuli amemshukuru Waziri Mkuu wa Uingereza kwa mchango huo ambao utasaidia juhudi za Serikali za kuhakikisha inarejesha miundombinu iliyoharibika zikiwemo shule.
"Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke naomba unifikishie shukrani zangu za dhati kwa Waziri Mkuu wa Uingereza Mhe. Theresa May na umueleze kuwa kwa niaba ya watanzania hususani waliopatwa na madhara ya tetemeko la ardhi tumeguswa sana na moyo wake wa upendo kwetu" amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli na Balozi Sarah Catherine Cooke pia wamezungumzia uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Uingereza ambapo Rais Magufuli ametoa wito kwa Balozi huyo kuendelea kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji wa Uingereza kuongeza uwekezaji wao hapa nchini na kwamba Tanzania itaendeleza na kukuza uhusiano huo.

"Uingereza ni rafiki na ndugu wa kweli na wa kihistoria kwa Tanzania, tunatambua kuwa nchi yenu ni mdau mkubwa na muhimu wa maendeleo yetu, hivyo tusingependa kupoteza rafiki na ndugu yetu, tuendelee kushirikiana kwa manufaa ya wananchi.

"Natambua kuwa Uingereza ina utaalamu mkubwa katika masuala ya gesi hivyo nawakaribisha waje wawekeze katika sekta ya gesi" amesisitiza Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli amesema Serikali itahakikisha fedha zote zinazotolewa kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na madhara ya maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera zinafikishwa kwa walengwa na ameonya kuwa watakaothubutu kuiba fedha hizo watashughulikiwa.

Dkt. Magufuli amebainisha kuwa baada ya kutengua uteuzi na kuchukua hatua nyingine dhidi ya aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Amantius Msole na Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba Bw. Steven Makonda pamoja na kumsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw. Simbaufoo Swai, amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei awachukulie hatua watumishi wa Benki hiyo walioshirikiana na watumishi hao kufanya njama za kuanzisha akaunti nyingine ya benki yenye jina linalofanana na akaunti rasmi ya "Kamati ya Maafa Kagera" kwa lengo la kujipatia fedha"

Yaya Toure: Ahofia Uamuzi wa Fifa kuwaumiza wachezaji

http://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/11986/production/_91407027_96b94309-5fb2-4470-b1ca-3d3bf59de84b.jpg

 BBC
Kiungo wa Manchester City, Yaya Toure amesema wachezaji na mashabiki wanaweza kuumia kufuatia hatua ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuvunja kikosi kazi kilichoundwa kwa ajili ya kupambana na vitendo vya ubaguzi wa rangi katika soka.
Toure mwenye umri wa miaka 33, alikuwa mmoja wa wajumbe katika kikosi kazi hicho kilichoundwa mwaka 2013 kusaidia kutokomeza ubaguzi.
Katibu mkuu wa FIFA, Fatma Samba Diouf Samoura amesema kikosi kazi hicho kilikuwa na kazi maalumu ambayo tayari wameimaliza.
Hata hivyo, hatua hiyo imekosolewa vikali na wadau mbalimbali, akiwemo Toure ambaye alifanyiwa vitendo vya kibaguzi na mashabiki wa CSKA Moscow Octoba mwaka 2013.
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ivory Coast amesema hatua hiyo ya FIFA itaweza kuwaumiza mashabiki na wachezaji kama mipango sahihi isipowekwa.

HIVI NDIVYO ARSENAL INAVYOTAKATA

http://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/4241/production/_91416961_theo-walcott-arsenal-aston-villa.jpg


Michuano ya klab bingwa barani ulaya inaendelea katika hatua ya makundi ambapo Usiku wa kuamkia leo michezo michezo nane ilipigwa katika viwanja tofauti. 

Arsenal ikiwa nyumbani ilibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Basel ya nchini uswizi, magoli yote yaliwekwa kimyani na Theo Walcott.

PSG ikiwa ugenini iliibuka na ushindi mnono wa 3-1 dhidi ya Ludogorets Razgrad ya nchini Bulgaria.
Besiktas imeenda sare ya 1-1 dhidi ya Dynamo Kyiv. Huku SSC Napoli ikiibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya Benfica.

Borussia Moenchengladbach nayo ikiwa nyumabi imekubali kichapo cha 2-1 dhidi ya Barcelona. Na mchezo wa kushangaza wa funga nikufunge ulikuwa kati ya Celtic na Manchester City, ambazo zilienda sare ya 3-3.

Atletico Madrid nayo ikiwa nyumbani iliibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Bayern Munich. Na FC Rostov ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 2-2 dhidi ya PSV Eindhoven

Bei ya mafuta duniani yaanza kupanda

 Tokeo la picha la MAFUTA
Bei ya mafuta duniani imeanza kupanda baada ya muungano wa mataifa yanayozalisha mafuta kwa wingi, Opec, kukubaliana kupunguza uzalishaji wa mafuta kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka minane.
Habari za kufikiwa kwa makubaliano hayo zimesababisha kupanda kwa bei ya mafuta ghafi kwa karibu asilimia 6.

Wanachama wa Opec wamekuwa wakilaumiana kusababisha mdororo wa bei ya mafuta kutoka nana wao kushindwa kuchukua msimamo mmoja wa kudhibiti bei.
Wanachama wa Opec wamekuwa wakikutana Algeria.

"Opec imechukua uamuzi wa kipekee leo," waziri wa mafuta wa Iran Bijan Zanganeh amesema.
Mafuta ghafi ya Brent, yanayotumiwa kama kigezo cha amfuta kimataifa, yalipanda bei na kufikia karibu asilimia 6 hadi $49 kila pipa baada ya tangazo hilo kutolewa.

Mawaziri wa mafuta wa nchi wanachama wamesema maelezo ya kina kuhusu mwafaka wa sasa yatajadiliwa kwenye mkutano mwingine Novemba.

Uzalishaji wa mafuta utapunguzwa hadi mapipa 700,000 kwa siku, ingawa upunguzaji wa uzalishaji hautakuwa sawa miongoni mwa wanachama.
Iran itaruhusiwa kuongeza uzalishaji wake.

Kulikuwa na suitafahamu awali baina ya Iran na mpinzani wake Mashariki ya Kati Saudi Arabia, jambo ambalo lilikuwa limezuia kupatikana kwa mwafaka.


Wazalishaji wadogo wa mafuta walipigania kupunguzwa kwa uzalishaji baada ya mafuta kushuka bei kutoka $110 miaka miwili iliyopita.
Waziri wa mafuta wa Nigeria Ibe Kachikwu, taifa lililoathirika sana, alisema huo ni "mkataba mzuri sana".
Waziri wa kawi wa Algeria Algerian Noureddine Bouarfaa amesema uamuzi huo huo ulifikiwa kwa kauli moja.
Waziri wa kawi wa Qatar Mohammed Bin Saleh Al-Sada ambaye ndiye rais wa sasa wa Opec amesema uzalishaji sasa utakuwa kati ya mapipa 33.2 milioni na 33 milioni kwa siku.
Uzalishaji wa sasa unakadiriwa kuwa mapipa 33.3 milioni kwa siku.

BBC SWAHILI

Upinzani Sudan Kusini waapa kuangusha utawala wa Kiir

http://gdb.voanews.com/6868A570-13E1-4F60-AC9C-13DA97F8B543_w987_r1_s.jpg  Kundi la upinzani huko nchini Sudan Kusini ambalo limeapa kuuangusha utawala wa Rais Kiir

Maafisa wa kundi la South Sudan Democratic Movement Cobra Faction ambalo zamani liliongozwa na David Yau Yau kwa mara nyingine wameapa kufanya vita dhidi ya serikali ya Rais Salva Kiir kwa sababu wanaishutumu haijatekeleza kwa upande wake matakwa ya mkataba wa amani uliotiwa saini mwaka 2014.
Yau Yau alitia saini mkataba wa amani na Rais Kiir mwezi mei mwaka 2014 ambao ulitoa njia ya kutambua eneo la Greater Pibor kuwa na mamlaka yake yenyewe.


Wakati huo huo Yau Yau aliteuliwa kuwa naibu waziri wa ulinzi lakini baadhi ya viongozi wengine wa SSDM-Cobra Faction wanasema utawala wa Kiir ulipuuza mikataba mingine yote ya majimbo.
Kiongozi mpya wa kundi la SSDM-Cobra Faction ni Luteni Jenerali Khalid Botrus Bora ambapo msemaji wake Kernoy Philip Kadal alifanya mkutano na waandishi wa habari mjini Nairobi nchini Kenya hapo Jumanne na kusema kundi litaungana na wanamgambo wengine katika juhudi za kuuangusha utawala wa Kiir.

MAKALA : Ukodishaji wa Ndege Usiokuwa na Faida - RIPOTI YA CAG



Ukaguzi umebaini kuwa tarehe 9 Oktoba, 2007, Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ilisaini mkataba wa ukodishaji wa ndege (Airbus namba A320-214 yenye usajili namba MSN630) kutoka Kampuni ya Wallis Trading Co. Ltd. Hata hivyo, mkataba wa kukodi haukufuata utaratibu muhimu na rasmi wa uendeshaji wa kampuni. 

Kwa mujibu wa taratibu hizi, Kitengo cha Ufundi ndani ya Kampuni kinawajibika kufanya uchunguzi wa ubora na kupata maelezo yote ya ndege kabla ya kuingia katika makubaliano yoyote ya kukodisha. Kwa upande mwingine, 

TCAA pia ni inawajibika kuchunguza na kukagua ndege ilikuhakikisha kwamba inaendana na viwango vya sayansi na ufundi wa vyombo vya anga vya kimataifa kabla ya kusajili ndege husika katika nchi. 

Nilibaini kuwa vitengo vyote viwili vya ufundi cha Kampuni ya Ndege Tanzania na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania lifanya uchunguzi wao kati ya tarehe 14 na 22 Januari, 2008 wakati mkataba wa kukodi ulikuwa umekwisha kusainiwa. 

Matokeo ya ukaguzi yalionyesha kuwa ndege haikufikia viwango vinavyohitajika hivyo Mamlaka ya Usafiri wa Anga ilimpa maelekezo mkodishaji kurekebisha mapungufu yaliyoonekana kabla ya kukabidhi ndege hiyo kwa Kampuni ya Ndege Tanzania. 

Aidha, nilibaini kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali mnamo tarehe 8 Oktoba, 2007 aliishauri Kampuni kupitia barua yake yenye kumbukumbu no.JC/I.30/308/3 lakini ushauri wake haukuzingatiwa wakati mkataba wa kukodi ndege unasainiwa. 

Ili kutimiza matakwa ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga kufuatia ukaguzi wao waliofanya, kampuni ya Wallis Trading Co LTD ilifanya matengenezo yaliyoelekezwa mwezi Februari, mwaka 2008. Hata hivyo, Mkodishaji hakukabidhi ndege kwa Kampuni ya Ndege Tanzania mpaka ilipofika mwezi Mei, mwaka 2008 baada tu ya Serikali kutoa barua ya dhamana ya thamani ya Dola za Marekani milioni 60 tarehe 2 Aprili mwaka 2008. 

ATCL ilikuwa ikigharamika kodi ya mwezi ya Dola za Marekani 370,000 kiasi kwamba kati ya Oktoba mwaka 2007 na Mei mwaka 2008 Kampuni ilikuwa ikidaiwa limbikizo la kodi la kiasi cha Dola za Marekani 2,590,000 kabla ya ndege kukabidhiwa rasmi kwa Kampuni ya Ndege Tanzania. Ndege ilifanya kazi kwa muda wa miezi sita hadi mwezi Novemba mwaka 2008. 

Ilipofika mwezi Disemba mwaka 2008 ndege ilitupelekwa katika Kampuni ya Ndege ya Mauritius kwa uchunguzi mkubwa wa kiufundi ambapo ilikaa hadi mwezi wa Juni mwaka 2009. Mwezi Julai mwaka 2009 ndege ilihamishiwa kwenye Kampuni ya Ndege ya Ufaransa kwa uchunguzi wa C+12. 

Makadirio za matengenezo yaliyofanyika yalikuwa Dola za Marekani 593,560 dhidi ya gharama halisi ambapo iliongezeka kufikia Dola za Marekani 3,099,495 baada ya matengenezo ya kina kufanyika. Mmiliki alitoa dhamana ya kuchangia Dola za Marekani 300,000 tu na gharama nyingine kubebwa na Kampuni ya Ndege Tanzania. 

Matengenezo yalikamilika mwezi Oktoba mwaka 2010 lakini ndege haikuweza kurudishwa Tanzania kutokana na Kampuni ya Ndege Tanzania kushindwa kulipa gharama husika. Ndege ilikaa Ufaransa kwa kipindi chote cha mkataba wa kukodi hadi tarehe 17 Oktoba 2011 mpaka mkataba ulipositishwa. 

Wakati mkataba wa kukodi unasitishwa, gharama za kukodi kwa muda wa miezi 43 ambayo ndege hiyo ilikuwa chini ya matengenezo zilifikia Dola za Marekani 15,910,000. 

Jumla ya gharama ikijumuishwa na ada ya kila mwezi ya kukodi na gharama nyingine kama vile riba ilifikia Dola za Marekani 42,459,316. (sawa na Bilioni 90)

NI MTIKISIKO



 ·     


           Katika kila watu 10 , 7 kati yao wanalalamika njaa
·        Kampuni zafunga Ofisi, zapunguza wafanyakazi
·        Vijana sasa wageukia Kilimo, Ufugaji
·        Serikali yasisitiza hali ni  shwari

Na. mwandishi wetu,
Mabadiliko makubwa ya kimfumo wa utawala katika serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli yanayoendana na kubana matumizi, kurudisha nidhamu serikalini, kufuta na kuondoa wafanyakazi hewa na kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya viwanda yenye uchumi wa kati yanaonyesha kuambatana na maumivu makali kwa wananchi wa kada mbalimbali yanayotokana na kinachoitwa kukaukiwa fedha mifukoni kunakotokana na kubanwa matumizi huko.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti unaonyesha kwamba, tangu mkakati wa kubana matumizi ushike kasi, hali ya maisha ya watu mmoja mmoja imekuwa ikibadilika kwa kasi kubwa huku nidhamu ya fedha ikionekana kutamalaki tofauti na hapo awali.
Sambamba na malalamiko hayo, taarifa zinaonyesha kupungua ama kudorora kwa mzunguko wa fedha katika maeneo mbalimbali ya nchi hususani jijini Dar es salaam kunakotokana na watu wengi wenye kipato kikubwa kijihami na kuamua kubana matumizi huku wakisikilizia hali ya uchumi kutengemaa, sambamba na kubana huko matumizi kwa kutokutumia pesa na kuiondoa katika mzunguko, pia wafanyabiashara wengi waliokuwa wametoa ajira kwa vijana na watu wazima wamepunguza idadi ya wafanyakazi kati ya asilimia 40 mpaka 60 ya wafanyakazi waliokuwa wamewaajiri ili kuendana na mabadiliko hayo ya kiuchumi.
Mmoja wa wamiliki wa kampuni inayojihusisha na huduma za hoteli hapa nchini ambaye ameombwa jina lake lisitajwe Gazetini, amesema kampuni  yake haina namna zaidi ya kupunguza wafanyakazi na kuitaka serikali iangalie upya na haraka njia bora ya kubadili mfumo wa kiuchumi bila kuathiri shughuli na maisha ya kila siku ya wananchi wake.
‘’kwa sasa ninaedesha kampuni kwa hasara kubwa, tena hasara imekuwa ikiongezeka kila siku tangu mwezi wa tatu, kiasi kwamba hata wafanyakazi ninawalipa Mishahara kutoka kwenye vyanzo vingine vya mapato ambavyo navyo vimekata kwa sasa, hivyo hakuna jinsi ndio maana nimeamua kuwapunguza tu ndugu yangu’’. Alisema
‘’wewe mwenyewe fikiria, tunalipa Ankara za maji, umeme, usafi na mishahara kwa gharama kubwa sana tofauti na tunachokipata, hali hii inatuumiza sana’’. Aliongeza
Utafiti zaidi uliofanywa na gazeti hili unaonyesha kuwa katika kila watu 10 waliohojiwa juu ya hali ya sasa ya kimaisha na kiuchumi, watu saba kati yao wamekuwa wakilalamika mabadiliko haya kuwakuta kabla ya wao kujiandaa na kwamba wanalia njaa.
‘’kwa hali hii, bora nichukue zangu malipo yangu ya pensheni nikajiajiri kwa kilimo aisee, nikifuga zangu kuku wa nyama na mayai hata wa milioni tatu naamini ipo siku watanilip tu’’. Alisema Godwin Mnyembela wa kinyerezi Dar es salaam.
Mwengine aliyepata kuzungumza na gazeti hili bwana Gilbert Mgube amesema kuwa kwa hali hii inavyokwenda inawahitaji vijana kutuliza akili zaidi kuliko kupapatika na sehemu sahihi ya kutulizia akili wakati wa kuangalia namna bora zaidi ya kuendana na kasi hii ni kilimo.
‘’wapo wanaolalamika kuhusu kilimo kutokulipa, lakini sio sawa na kutokupata kabisa, uzurinwa kilimo hakikukati moja kwa moja, utakosa kikubwa lakini kidogo utapata, na ikiwa utazingatia matakwa ya ukulima wa kisasa haiwezi kukukata kabisa na lazima ikulipe, japo changamoto ya soko imezidi kuwa kubwa kwa sasa, lakini hakuna kukata tamaa’’. Alisema Mgube
Hivi karibuni kumeripotiwa kufanyiwa mabadiliko kwa makampuni kadhaa ya hoteli na kufungwa, kuuzwa ama kubadili matumizi ili kuendana na hali ya sasa ya ubanaji wa matumizi.
Hoteli maarufu jijini arusha za Snow Crest na Mount Meru zilizokuwa zikisifika kwa ubora na uendeshaji wake sasa zimetangazwa kuuzwa huku jijini Dar es Salaam hotel maarufu ya land mark iliyopo ubungo riverside ikibadili matumizi kutoka kuwa hotel mpaka hostel kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo vikuu.
Hali hii inakuja huku kukiwa na  taarifa za Benki Kuu zilizopo kwenye tovuti yake (Quarterly Economic Review na Monthly Economic Review) kwa robo ya mwisho ya mwaka 2015 (Oktoba - Desemba 2015 ) zinaonesha kuwa kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa ilikuwa 9%. Katika robo ya kwanza ya mwaka 2016 (Januari - Machi 2016) kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa ilishuka hadi kufikia 5.5%. Kiuchumi, hii inamaanisha kuwa ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika kipindi cha miezi 6 umepungua kwa 4%.
Taarifa hizo zinaonyesha kuwa  Shughuli za uchumi zinazohusu wananchi masikini zimeshuka kutoka kasi ya ukuaji ya 10.20% robo ya mwisho ya mwaka 2015 mpaka 2.7% katika robo ya kwanza ya mwaka 2016, ikiwa ni punguzo la 8% ndani ya kipindi kisichozidi miezi sita, sambamba na hayo, Ukuaji wa sekta ya ujenzi katika robo ya mwisho ya mwaka 2015 ilikuwa 13.8% lakini ukuaji wa sekta hii katika robo ya kwanza ya mwaka 2016 ilikuwa ni 4.30%, ikiwa ni tofauti ya takribani -10%. Hii ni kwa sababu uwekezaji katika sekta hii umeanza kushuka.
 Taarifa hizo zinaonyesha zaidi kuwa Kasi ya ukuaji wa sekta ya usafirishaji imeporomoka kutoka kukua kwa 14.50% robo ya mwisho ya 2015 mpaka kukua kwa 7.9% robo ya kwanza ya 2016, ikiwa ni kuporomoka kwa 7%.
Taarifa hizi  za kushuka kwa uchumi zinaenda sambamba na malalamiko ya kupungua kwa shehena ya mizigo katika bandari ya Dar es salaam kunakodaiwa kutokana na kuongezeka kwa gharama za tozo za kodi tofauti na hapo awali.
Tofauti na malalamiko hayo ya kupungua kwa mizigo kunakodaiwa na serikali kupitia mamlaka ya mapato nchini  Tra kupandisha tozo hizo, taarifa iliyosambazwa na viongozi wa Tra mitandaoni inawaondoa hofu watanzania na kwamba kodi sio sababu ya mizigo kupungua.
Taarifa hiyo inakiri kuwa ni ukweli uliowazi kuwa kwa kiasi fulani mizigo imepungua kwa wastani wa asilimia 9-30 kutegemea na nchi, ambapo  mizigo mingi iliyokuwa inapita bandari ya Dar kwa kisingizio inaenda Kongo siyo kweli ilikuwa inaenda Kongo badala yake ilikuwa wana itumia  humu nchini.
Taarifa hiyo inazitaja sababu nyingine kuwa ni Kudorora kwa bei ya shaba Zambia,Uchaguzi mkuu wa  Zambia na kuimarika kwa  Msumbuji kiasi kwamba bandari ya Beira imeanza kufanyakazi vizuri.
Sababu nyingine ni Kuanza kutumika kwa utaratibu wa Single Custom Territory ambapo mizigo inalipiwa ktk bandari ya Dar kabla ya kusafirishwa kwenda Kongo ambapo inawanyima wafanyabiashara kule Kongo kukwepa kodi .

Sambamba na hayo sehemu ya taarifa hiyo inaonyesha kwamba hata katika  utafiti tulioufanya hata Bandari ya Mombasa mizigo imepungua, na kusema kuwa kupungua kwa mizigo katika bandari ya Dar hakujazuia kuongezeka kwa mapato na badala yake mapato yanayotokana na bandari yameongezeka maradufu tofauti na hapo awali
‘’Wakati meli zikiwa zimepingua katika bandari ya  Dar,  Mapato yatokanayo na Forodha mwaka 2015 yalikuwa wastani wa Shilingi Bilioni 200-300  kwa mwezi. Lakini tangu Disemba 2015 - August 2016 wastani wa mapato ya Forodha kwa mwezi ni Kati ya shilingi bilioni 400-550. Facts hizi zipo Mwananchi yeyote anaweza kuzipata kwenye tovuti yetu ya TRA Taarifa za Mapato kila mwezi.’’ Inasema taarifa ya mamlaka hiyo ya serikali
Wakati TRA wakisema hayo, hivi karibuni Gavana wa benki kuu ya Tanzania Professa Beno Ndulu ameuhakikishia umma kwamba hali ya uchumi wan chi ni shwari na kwamba kila kitu kipo sawa na kinachotokea sasa kiuchumi ni kuondoka ama kupungua kwa fedha za ujanaujanja mitaani na kubaki kwa fedha zinazotokana na shughuli rasmi.



HONGERA TENA MAGUFULI - MCHANGE


Jana wakati unazindua na kukabidhi ndege mbili 'mpya' ATCL nimekusikiliza kwa Makini mno Rais MAGUFULI,
nimefurahishwa zaidi na Dhamira yako ya kutaka kulifikisha taifa sehemu fulani.
Ulipotangaza Kununua ndege mbili kubwa ambapo moja kubwa na nyingine kubwa zaidi ni kama ulikuwa unausemea moyo wangu.
Mimi na watanzania wengine wengi wetu ni wajasiriamali wadogo.
Tunapojichanga changa tukipata vidola elf 5 tunakimbilia china kuchuuza na kuleta vibiashara hapa nyumbani kuganga njaa.
Mimi ni Muafrika zaidi, siamini katika mashirika ya ndege ya kiarabu kama emirates au Qatar, Wala ya kizungu
Kwa sababu hiyo mara zote ninaposafiri kimataifa hasa kuelekea China au Hong Kong Mimi husafiri na Ethiopian Airlines.
Nachukuliwa DSM mpaka Bolle International Airport Addis Ababa.  Kusubiri ndege ya kunipeleka kituo cha mwisho.
Pale nakutana na watu wa mataifa mbali mbali ya Africa hasa Africa magharibi.
Wakenya wenzetu wako sensitive Sana na utaifa wao 9/10 husafiri kwa ndege yao Kenya Airways - KQ.
Mara zote nikiwa Bolle kuanzia nashuka mpaka na connect ndege nasononekaga Sana.  Hakuna walichotuzidi kimuonekano, lakini wao wamewekeza Sawa Sawa katika ndege.  Mpaka unaona wivu.
Jana MAGU umegusa ndoto yangu, ndoto ya Mimi kutoka moja kwa moja nyumbani,  kwenda Airport na nikipaa, nikitua nipo China au popote nitakapokuwa ninaenda.  Hongera Sana.
Ndoto hii na itimie hata kesho Baba,  ndoto ya watu wa Malawi,  Zambia,  Congo,  Uganda, Burundi na kwengineko kuacha kwenda umbali mrefu mpaka Addis au Joburg kuunganisha badala yake Kuja Dar,  Shukrani Sana.
Ndoto ya kuwa na ndege ambayo wasafiri wake watasoma vitabu vya kitanzania wakiwa angani,  watatazama miziki ya kitanzania wakiwa angani,  watakula chakula cha kitanzania na watazungumza lugha ya kitanzania - hii si ndoto ya kubezwa hata kidogo.
Ndoto ambayo itanifanya nisisafiri tena masaa 19 kufika China Bali masaa nane na nusu tu mpaka tisa Sawa na ndugu yangu aendae Arusha kwa Basi akitokea Dar - ndoto nzuri Sana hii.
Hii ni Ndoto itakayonisaidia zaidi kupunguza gharama za Usafiri mpaka asilimia 40 ya ninazolipa Sasa kwenda ughaibuni.
Ndoto hii itanisaidia kuhakikisha usalama wa mizigo yangu, maana hatari ya kupotea au kuchelewa kutokana na connections itakuwa imepungua mno kwa kuwa ni moja kwa moja.
Ndoto itakayowafanya watalii Kuja moja kwa moja Tanzania Kuona vivutio vyetu,  hakukuwa na haja ya mtalii kupitia Kenya halafu Kuja mikumi Kuona simba ambao angeweza kuwaona Tsavoy Kenya.
Hii ni ndoto itakayonifanya nijivunie zaidi kuwa mtanzania maana kwa wasiojua, moja Kati ya kielelezo chepesi cha taifa kimataifa ni shirika la ndege.
Hongera Sana kwa Dhamira hii,  Hongera tena kwa kututia moyo na matumaini yaliyopotezwa na serikali ambayo wewe mwenyewe pia ulikuwemo kwa zaidi ya miaka 20 lakini si haba unatusitiri Sasa.
MUNGU AKUTIE NGUVU INSHAALLAH.
Ndimi
Habib Mchange