WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, September 29, 2016

BILIONI 415 ZAPOTEA UDOM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjh-n1dokVEqJIGXG_qIQaQu4ii198wS4WDbB7Mbxz6oA0rEk-Z1hPn3dGiAvmjj7lUbfyC-betA5omxnDpUIPOBzJ2KUGv66_zbcbYeEV9UIyegI77L8v-teTa53UzaU8TmYqUTgmW50go/s1600/1.jpg 


na mwandishi wetu.

Ni kama Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, anakibarua kizito kunusuru upotevu unaoweza kujitokeza wa usimamizi wa mali za chuo kikuu cha Dodoma  zenye thamani ya  zaidi ya shilingi bilioni 400  taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali,CAG ya mwaka 2014/2015 inaeleza.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa serikali kupitia mashirika ya mifuko ya hifadhi za jamii ilijenga chuo hicho kikuu kikubwa kuliko vyote katika ukanda huu wa afrika mashariki kwa mkataba wa ujenzi,ubunifu, umiliki na uendeshaji wa pamoja na kwamba baada ya kukamilika mali za chuo hicho zilitakiwa kumilikiwa na mashirika hayo ndani ya miaka kumi lakini mpaka taarifa hiyo inatoka jambo hilo halikuwa limefanyika.

‘’Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Pensheni kwa Wafanyakazi wa Umma (PSPF), Mfuko wa Pensheni kwa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF), Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) na Mfuko wa Pensheni wa PPF yalitumia jumla ya Shilingi bilioni 415.4 kujenga Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), chini ya makubaliano ya buni, jenga, endesha, na kisha hamisha miliki baada ya miaka kumi (10)’’.  Inasema sehemu ya taarifa hiyo ya CAG

Totauti na ilivyotarajiwa, taarifa hiyo inasema kwamba mpaka sasa majengo hayo hayajaingizwa kwenye kumbukumbu za  chuo hicho wala mashirika hayo na hivyo kuhatarisha upotevu wake,

‘’Majengo haya hayapo kwenye vitabu vya Chuo Kikuu cha Dodoma wala katika vitabu vya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii husika. Japokuwa Mlipaji Mkuu wa Serikali amejibu kuwa majengo haya yataingizwa kwenye vitabu vya Chuo Kikuu cha Dodoma katika mwaka wa fedha wa 2013/2014, bado UDOM imepewa Hati Yenye Mashaka kutokana na kutokuwepo kwa majengo hayo kwenye vitabu vyake.’’ Imeongeza taarifa hiyo
 Kufuatia uchunguzi huo, mdhibiti na mkaguzi mkuu huyo wa serikali anaendelea kusisitiza umuhimu wa majengo hayo kuingizwa kwenye vitabu vya chuo hicho cha UDOM kama alivyopendekeza awali ili kukiondolea chuo hicho shaka ya kuendelea kutopata hati safi.

Hayo yanatokea huku kukiwa na msuguano wa chinichini baina ya wafanyakazi wa taasisi mbalimbali hapa nchini na serikali juu ya swala la Fao la kujitoa ambapo serikali imebadili sharia ili kuzuia fao hilo.

Sambamba na hilo la fao la kujitoa, wachambuzi wa mambo wanasisitiza kuwa kuna haja ya serikali kusimamia sawa sawa faida zinazotakiwa kutokana na ujenzi wa chuo hicho kwa kuwa ujenzi wake umetokana na fedha za watanzania na hivyo wafanye kila linalowezekana kukamilisha umiliki huo wa mali ili kuhakiki ulinzi wa pesa zao.

‘’unajua kibiashara, UDOM ni uwekezaji wa pesa zetu, sasa na kila uwekezaji lazima uzalishe faida, na kama mpaka sasa hawajakamilisha umilikishaji wa mali hizo kwa mashirika yetu maana yake uwekezaji huo hautatulipa na pesa zetu zitapote bure, serikali inatakiwa ichukue hatua za makusudi kwenye hilo’’. Alisema Omari kihampa mwanachama wa moja ya mifuko ya hifadhi za taifa.

‘’bilioni 415 ni nyingi sana aisee, pamoja na kuipongeza serikali kujenga chuo kupitia fedha zetu lakini lazima fedha hizo zituhakikishie usalama wetu tukistahafu, kuacha kuendelea hivi ilivyo itakuwa ni kuzipoteza’’. Ananukuliwa Mariam Jamlisheed mtumishi wa wizara moja hapa nchini.

Gazeti hili linaendelea na jitihada za kuutafuta uongozi wa chuo hicho kuona mpaka sasa ni hatua gani wamechukua kuhusiana na suala hilo linalopelekea chuo cha Dodoma kukosa mmikili halali mpaka sasa

No comments:

Post a Comment