WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, September 29, 2016

MHANDISI URAMBO MIKONONI MWA WAZIRI SIMBACHAWENE



http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/SIMBAW.jpg 
waziri wa TAMISEMI George Simbachawene
Na Mwandishi wetu
Waziri wan chi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa mheshimiwa George Simbachawene ametakiwa kuingilia kati tabia za baadhi ya watendaji wa halimashauri mbalimbali hapa nchini kutokana na watendaji hao kulalamikiwa kutokusimamia sharia katika masuala kadhaa hasa yanayohusu manunuzi na kusababisha mgogoro na mgongano wa kimaslahi kunakopelekea kudorora kwa utolewaji wa huduma za msingi za kijamii na maendeleo.
Akizungumza na gazeti hili mmoja wa watumishi wa wizara hiyo ameshauri kuwa ni vema suala hilo akaachiwa waziri mwenyewe kwa sababu yeye ndie msimamizi wa moja kwa moja wa wizara hiyo na kwamba maamuzi yake ndio huwa ya mwisho na akiamua kuchukua nidhamu kwa muhusika wala haitazuilika.
Kadharika madiwani kadhaa wa halimashauri ya wilaya urambo ambapo wiki iliyopita gazeti hili lilitipoti kuhusiana na kadhia ya mhandisi mkuu wa ujenzi wa wilaya hiyo kujihusisha na tabia zinazoendana ama kuonekana kukiuka taratibu za kimanunuzi na ukiukwaji wa sharia wa wazi.
‘’sisi kwenye kikao tutamjadili na kuliazimia swala lake, lakini pia tutamtaka waziri simbachawene amuwajibishe haraka iwezekanavyo, maana sina imani kama mkurugenzi anaweza kutengua nafasi yake’’. Alisema diwani mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa
‘’unajua huyu bwana alishawahi kufikishwa mpaka Takukuru kuhusiana na masuala hayahaya, lakini inaonyesha kwamba ama amenogewa ama amewazidi ujanja hao mambwana wa Takukuru, hivyo Simachawene anaweza kutusaidia kabisa kabisa kumalizana na huyu bwana’’, aliongeza diwani huyo
Hayo yanatokea wakati wiki iliyopita gazeti hili lilipoti kuhusiana na kuwepo kwa tafiti  zikimuonyesha Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuwa kiongozi anayependwa zaidi na wananchi wake hasa kutokana na tabia yake ya kusimamia sawa sawa sheria na kutumbua majipu kwa kuwaondoa wabadhilifu serikalini na katika taasisi mbalimbali za umma,baadhi ya wasaidizi wake katika ngazi za halimashauri wanaweza kumkwamisha kutokana kutokusoma alama za nyakati hasa katika kipindi hiki cha utawala wa awamu ya tano wenye kauli mbiu ya hapa kazi tu.
Tuhuma nzito za mgogoro wa kimaslahi zinamkabili  Mhandisi mkuu wa halimashauri ya wilaya urambo mkoani tabora bwana Makori Kisare zikimuhusisha na kujilipa mamilioni ya shilingi kupitia kampuni ambayo inahusishwa naye kuwa mbia ya  Mispa Constraction Co. Ltd yenye makao yake makuu mkoani mara.
Taarifa za uhakika ambazo gazeti limezipata zinasema kuwa mhandisi huyo wa wilaya amekuwa akiisababishia hasara serikali kwa kupokea kazi zilizofanywa chini ya kiwango kutokana na tabia yake ya kuitumia kampuni yake hiyo kuomba kazi ambazo yeye mwenyewe anashiriki kuziandaa na kuzitangaza na hatimaye kampuni yake hiyo kushinda zabuni hizo hivyo kuingia katika mgogoro wa kimaslahi.
Taarifa hizo zinasema kuwa kampuni yake hiyo  iliyosajiliwa tarehe 22 mwezi wa tisa mwaka 2010 ikiwa na namba ya usajili74055 ya sanduku la barua 669 musoma mkoani mara, mpaka sasa imekuwa ikifanya kazi katika maeneo kadhaa hapa nchini hasa katika halimashauri ambazo ama amewahi kufanya kazi au ana maswahiba zake wanaofanya kazi hapo, mifano ikiwa ni  halimashauri za urambo na Dodoma na
Jamvi la habari linaweza kuthibitisha kuwa, mhandisi huyo baada ya Kuteuliwa kuwa Mhandisi ujenzi Wilaya ya Urambo alianza jipatia kazi kupitia Kampuni hiyo kwa kutumia cheo chake cha ukuu wa Idara ya Ujenzi, jambo linalosababisha kukosekana kwa ufanisi na uwajibikaji kwa kuwa muwajibishaji ndie anayefanya kazi.
Baadhi ya miradi ambayo hata hivyo imeonyeshwa kufanywa chini ya kiwango ni  ule wa ujenzi wa mitaro uliopo  Urambo mjini wenye thamani ya Shilingi Milion Sabini na tano (75million) na kuendelea kujipatia kazi nyingine ya matengenezo ya Barabara kuelekea standi mpya yenye thamani ya Milion themanini na tano (85million).
Sambamba na hayo mhandisi huyo analalamikiwa na baadhi ya wasaidizi wa idara yake katika halimashauri hiyo kwa  kuipendelea wazi wazi kampuni yake huku akijua navunha utaratibu na taratibu za manunuzi zinazoelekeza kwamba inapokuwa walioomba kazi wengi wanasifa zinazofanana, basi aliyeomba kwa kiwango cha chini cha malipo ndiye atapaswa kupewa kazi hiyo, na kinyume chake ameamua kujipa kazi huku kampuni yake ikiwa imependekeza gharama kubwa.
Akizungumza kwa ombi la kutoandikwa gazetini mmoja wa watendaji wa ofisi hiyo amesema anashangaa kuona mabadiliko haya ya kiutendaji tangu kuingia kwa mkuu huyo mpya wa idara.
‘’Hebu fikiria, katika mradi wa  kazi ya utengenezaji wa Barabara na mitaro ya Urambo mjini (Majengo ya Tabora) ilitender kwa Shilingi milioni Miamoja na Tisini na Tisa (199million) na wakati nyingine zalitenda  kwa milion miamoja sabini na tatu (173million) na kwa milioni miamoja na themanini (180million), lakini aliamua kujipa yeye kazi hiyo licha ya kwamba gharama zake zipo juu’’. Alisema
‘’akikupenda bossi, au kama unakula naye vizuri wala hupati shida, ona alivyowapa kazi marafiki zake wa wengine Nebrix japo wameshindwa kufikia kiwango’’ aliongeza
Taarifa zinaonyesha kwamba  Mhandisi huyo anatuhumiwa kutokuzingatia sharia wala kanuni za manunuzi na kwamba mfano wa zabuni ya za Kuweka vifaa vya Maabara aliamuru apewe Nebrix Ltd  kazi ambayo kwa kiwango kikubwa imeshindwa kufainya  vema kwa kupasuka pasuka kwa mipira ya gas na maji ( Value for Money) lakini licha ya hayo aliendelea kuipatia kampuni ya hiyo miradi yote ya Wilaya ya Urambo huku wadadisi mambo wa halmashauri husika wakivujisha kwamba kampuni hiyo ilitumika kama daraja la yeye kujikwapulia fedha hizo, na hata wazabuni wengine walipo omba kazi hizo walikataliwa na akapewa mtu mmoja kwa Wilaya nzima.
Alipotafutwa na gazeti hili kupitia namba yake ya simu yake ya mkononi ambayo pia inaonekana kwenye taarifa za wasifu wa kampuni hiyo, mhandisi huyo amekanusha kuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo na kwamba alitoka huko miaka kadhaa nyuma na sasa sio tena muhusika.
‘’kuhusu mispa kama mispa kwanza sikuwa mmiliki, nilikuwa mshauri tu, mimi nilikuwa mmiliki wa kampuni nyingine kabisa ila mispa nilikuwa mshauri tu wa masuala mbalimbali na kwa sasa sina uhusiano nayo’’. Alinukuliwa bwana Makori.
Kupatikana kwa majibu hayo ya bwana makori kunaibua maswali kadhaa ikiwemo ya kwamba Mispa ilijua kwamba makori ndie mkuu wa idara ya ujenzi wa wilaya ya urambo na wakati anaipatia kazi alikuwa anajua au hajui kama ile ni kampuni anayodai kuwahi kuwa mshauri wake na kama alitangaza maslahi yake popote.
‘’Mkuu ameshawahi kubadilisha vipuli vizima vya magari ya serikari na kuviuza kwa bei ya chini  kwa rafiki zake na kuweka vipuli vibovu ambavyo baada ya siku chache hufa kabisa na kuandikia madokezo ili vinunuliwe vingine, tukio ambalo pia limewahi kutokea katika halimashauri jirani ya kaliua ambapo liliwahi kukamatwa fulushi likwa na Engine mbovu ya Land Cruizer amboyo ilikua ipo tayari kubadilishwa, hilo lilishuhudiwa na watumishi kazaa ila Mkurugenzi alie kuwepo ambae sasa amehamishiwa Jijini Arusha ambapo  aliamua kulizima suala hilo, huu ni kama ugonjwa wa kila halimashauri hapa nchini’’.
Malalamiko kama haya ya urambo, yanasemwa kuwa ndio tabia ya watendaji na watumishi wa serikali na mashirika ya umma wa maeneo mengi (gazeti hili linayo mifano mingi) na kwamba kazi nyingi zinazotangazwa hutangazwa tu kugelesha lakini kampuni zao wenyewe na ambazo nyingine hazina hata ofisi hupewa kazi hizo na kusababisha ufanisi wa chini ya kiwango.
Juhudi za kumtafuta mkuu wa mkoa wa tabora mheshimiwa Agrey Mwanri kulizungumzia suala hilo zinaendelea na na katika kumsaidi na kuunga mkono jitihada za Rais Dk. John Pombe Magufuli kurudisha nidhamu serikalini na kuwafikishia watanzania maendeleo kwa kuwapatia huduma zinazostahili kwa wakati bili upendeleo, gazeti hili litaendelea kuujulisha umma hatua kwa hatua kuhusiana na jambo hilo na mengine yanayofanana na hili..




No comments:

Post a Comment