Rais mteule wa Marekani, Donald
Trump, amepuuzilia mbali madai ya Korea Kaskazini kuwa imeunda Kombora
linaloweza kuwasilisha zana za nuklia hadi Marekani.
Bwana Trump alisema katika ujumbe wake kuwa "Haitawezekana." Tamko lake la haiwezekani, halikueleweka vizuri kwa sababu wachanganuzi hawajui iwapo alimaanisha kuwa Korea Kaskazini haina uwezo huo au alikuwa akiandaa hatua ya kujikinga.
Bwana Trump pia alishutumu Uchina kwa kushindwa kuthibiti mshirika wake
Korea Kaskazini na pia akalaumu Beijing kwa kupokea pesa kiasi kikubwa
cha pesa na mali kutoka Marekani
BBC
No comments:
Post a Comment