WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Sunday, January 22, 2017

KASHFA YA RUZUKU YA CUF : Siri zaidi zavuja

Yabainika milioni 369 ziliingizwa katika akaunti halaliTokeo la picha la mutungiJaji Fransis Mutungi, Msajili wa Vyama vya siasa nchini Tanzania
  • L CUF Zanzibar watofautiana
  • L Habib Mnyaa apongeza uamuzi wa msajili
Na Meshack Katunzi.- JAMVI LA HABARI

SHILINGI milioni 369 zilizodaiwa kutoroshwa kutoka hazina na kwenda katika akaunti ya Chama cha CUF wilaya ya Temeke, Januari  5 na baadae kugawanywa  kwa watu mbalimbali, zinaelezwa ziliingizwa kihalali kwa kufuata sheria na taratibu zote za kiofisi kama ilivyoelekezwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jamvi la Habari linaweza kuthibitisha.

Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Kamati ya uongozi ya chama cha wananchi CUF ambaye ofisi ya  msajili wa vyama vya siasa haimtambui, Julius Mtatiro alikaririwa na vyombo kadhaa vya habari akilalamikia juu ya alichokiita kuchotwa kwa fedha za ruzuku za chama hicho kitendo alichokiita kupewa baraka na msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi.

Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili limezipata, zinaonyesha kuwa hakukuwa na tatizo lolote la kisheria, kimaadili wala kikanuni katika utoaji wa fedha hizo ambazo ni sehemu ya fedha za ruzuku ambazo CUF wanastahili kupata kutoka serikali kuu kwa shughuli za uendeshaji wa chama hicho.

Taarifa hizo zinasema zaidi kuwa sio kweli fedha hizo ziliingizwa katika akaunti ya wilaya ya Temeke isipokuwa kwa sasa, Temeke ni jina tu la akaunti hiyo kama ambavyo akaunti nyingine zinaitwa Holland, Vijana, Kijitonyama na kadharika, na kwamba akaunti hiyo ni halali na imehuishwa kwa kubadilishwa matumizi yake kutoka kuwa akaunti ya wilaya mpaka kuwa akaunti maalum ya taifa kwa kufuata vikao halali vya mashauriano ya chama hicho.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu aliye ndani ya serikali, anasema ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ilipata uthibitisho pasi na shaka kwamba  akaunti hiyo ni halali kwa kukipatia chama hicho ruzuku yao kama walivyoomba viongozi waandamizi wanaofahamika na kutambulika na msajili wa vyama.

‘’Unajua msajili hajajiingizia tu zile fedha, CUF wenyewe walileta maombi kuwa fedha zao kwa sasa ziingizwe katika akaunti namba fulani inayopatikana sehemu fulani, ndipo msajili alipofuatilia na kuwataka watimize masharti yote ya kikatiba ikiwemo kufuata vikao halali vya chama chao na kuwaingizia fedha hizo baada ya kuombwa muda mrefu kufanya hivyo’’. Kilisema chanzo chetu

‘’Ukweli ni kwamba Msajili anaifahamu CUF moja tu,  msajili yeye haifahamu kamati inayoongozwa na Mtatiro na wenzake, anachofahamu msajili wa vyama vya siasa kuwa kuna CUF, ambacho Mwenyekiti wake ni Profesa Ibrahim Lipumba, Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharrif Hamad, na manaibu wake Magdalena Sakaya na Nassoro Mazrui kila mmoja’’ kiliongeza chanzo chetu.
 Tokeo la picha la julius mtatiro 
Julius Mtatiro
Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili linazo zinaonyesha kuwa  kitendo cha Profesa Lipumba kumtambua na kuwa tayari kufanya kazi na Katibu Mkuu wa CUF,  Maalim Seif kimempa moyo msajili kuwa akuwapatia ruzuku kina Lipumba kutapelekea kazi za chama kizima kufanyika kwa kuwa mara kadhaa Lipumba amekaririwa na vyombo vya habari akimuita ofisini katibu mkuu wake kumpangia kazi za kufanya.

Tofauti na Katibu mkuu wa CUF Maalim Seif  ambaye ameendelea kusisitiza kutomtambua Mwenyekiti wake Lipumba bila kujali ukweli kwamba mamlaka iliyomchagua haikuwahi kurudhia kujiudhulu kwake.
‘’katika akili tu ya kawaida, mwenyekiti wa chama ndio kiongozi mkuu wa shughuli za kichama katika CUF, yeye anathibitisha anamtambua Katibu Mkuu wake na yupo tayari kushirikiana naye kufanya kazi, Katibu Mkuu yeye hataki kumtambua na anaendelea kuing’ang’ania Kamati ya Uongozi ambayo kisheria haitambuliki, unafikiri ili chama kiendelee kupewa ruzuku na kijiendeshe, nani angepewa ruzuku kama si Lipumba’’.  Alisema Chumi Kisyabo aliyeombwa na gazeti hili kutoa maoni yake.

‘’Kwa maoni yangu, kumpa ruzuku Lipumba ni kukifanya chama chao kiende mbele kwa kuwa Lipumba ndio kiongozi mkuu wa chama na anawatambua wasaidizi wake wote halali akiwemo Maalim Seif, na kumpa ruzuku Maalim Seif ni kukidumaza chama na kuchochea  mgogoro kutokana na msimamo wa wake wa kutomtambua, kwa hili namuona msajili wa vyama kama mtu aliyetumia akili nyingi sana kuutatua mgogoro huu’’. Alisema.
 Tokeo la picha la maalim seif 
Maalim Seif Sharrif Hamad

Sakata la ruzuku la chama hicho kimeendelea kuchukua nafasi katika vichwa vya habari mbalimbali ambapo jumapili ya Januari 15, 2017 anayejiita Mwenyekiti wa kamati ya uongozi wa chama hicho, Mtatiro alishiriki kwa njia ya simu mjadala kuhusu jambo hilo na Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma, Abdul  aliyekuwepo studio katika kituo cha Star Tv jijini Mwanza na wawili hao kushindana kwa hoja, katiba na uzoefu wao ndani ya chama hicho huku kambaya akimtuhumu mtatiro kuwa ni mpiga madili mzoefu.
‘’Namshangaa Julius(Mtatiro) leo analalamika sisi kuingiza  fedha hizi kwenye akaunti ya diwani wetu na anasema ni wizi, wakati yeye mwaka 2011 aliingiziwa milioni mia moja na nane (108) katika akaunti yake binafsi , sasa leo analalamika nini nay eye mwenyewe aliwahi kumuingizia diwani huyo huyo milioni 46’’?. Alisema Kambaya.

Katika majibu yake,  Mtatiro alikiri kuingiziwa na kusema ziliingizwa kwababu ya kampeni za uchaguzi mdogo igunga, japo akaunti ya wilaya hiyo ya igunga ilkikuwepo.
Katika hatua nyingine kiongozi mwandamizi wa chama hicho na mbunge maarufu mstaafu  wa Mkanyageni, Habib Mnyaa alipiga simu studio hizo na kusema yeye kama mwanachama na kiongozi mwandamizi wa chama hicho haoni shida kwa wao kuingiziwa fedha kwenye akaunti hiyo kwa kuwa ni akaunti halali ya chama na kwamba kuziingiza kwenye akaunti binafsi ya mtu ni jambo la chama ambalo halihusiani na msajili wa vyama.

‘’msajili hajaingiza fedha kwenye akaunti ya mtu binafsi, msajili ameingiza fedha kwenye akaunti ya chama, na kwa hivyo hakuna tatizo lolote kisheria, chama kimetumiaje hizo fedha ndio swala linaloweza kuibua mjadala, na hata hivyo mamlaka ya ubadhilifu sio ya mtatiro ni mamlaka ya CAG, hivyo hatuna haja ya kuwa na papara, tusubiri tuone matokeo ya msajili, kwenye hili Msajili hana makosa na ninampongeza sana kwa kweli’’. Alisikika Mnyaa.

No comments:

Post a Comment