WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Tuesday, November 15, 2016

BREAKING NEWS: HIVI NDIVYO WAZIRI KIGWANGALA ALIVYOKAMATA POMBE BANDIA







BREAKING NEWS:
WAZIRI KIGWANGALA AKAMATA VIWANDA FEKI VYA POMBE.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla, ambaye anaongoza timu ya Serikali yenye wataalamu na wanausalama, kusaka viroba feki na pombe nyingine haramu, amekamata shehena kubwa ya bidhaa hizo feki na haramu kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kukifuma kiwanda bubu kinachotengeneza konyagi   na Smirnoff feki maeneo ya Sinza. 

Kiwanda hicho kinatengeneza vinywaji hivyo kwa kutumia 'spirit' ambayo inachanganywa na 'gongo'; spirit, gongo, chupa tupu na zilizojazwa, vizibo, vifungashio vimekamatwa. 

Polisi inawashikilia watu wawili ambao inasemekana wanafanya kazi pamoja na bwana Yusuf Abdul Kalambo, ambaye anatafutwa na polisi mpaka sasa.
JAMVI LA HABARI LITAWAJUZA ZAIDI.

No comments:

Post a Comment