WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, November 17, 2016

BREAKING NEWS: MBEYA, TUNDUMA ZADAIWA KUWA SOKO LA VIROBA, POMBE FEKI


 


Wakati  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla, akiendelea na usimamizi wa Operesheni Maalum ya kufuatilia na kuufumua mtandao wa Viroba na Pombe feki na haramu nchini. Mchana wa jana  amelazimika kukifunga kiwanda cha Afro American kinachozalisha viroba aina ya Zed, Dollars na vinginevyo ambavyo vimekutwa havina vibali vya TFDA na havina usajili wa TFDA, havina Batch Number ya kutambua uhalali wa uzalishaji wake, havina tarehe ya kuzalishwa na wala ya ku-expire. 

Hivyo ni ngumu kutambua ubora wake na idadi yake halisi kwa maksudi ya kulipa kodi ya serikali. 

Wenye kiwanda hawatunzi rekodi za uzalishaji na wamekiri kuwa mitambo yao haina uwezo wa kuweka batch number. Jana akiendesha operesheni hii maalum, Dkt. Kigwangalla alibaini uwepo wa bidhaa hizi sokoni na hivyo aliagiza wataalamu wafuatilie kinyume nyume kujua zinakotoka. Upelelezi umewafikisha hapa.

mmoja wa watoa taarifa wetu ametujuza kuwa mizigo hiyo husafirishwa usiku wa manane kupelekwa mbeya na tunduma kwa mauzo.

''Hivi viroba hauzi Dar kabisa. Anapeleka Mbeya Na Tunduma tu! Kila siku usiku wa manane anasafirisha gari mbili za tani 10 kila moja''. amesema msiri wetu

No comments:

Post a Comment