WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Tuesday, November 8, 2016

BREAKING NEWS: TUHUMA NZITO ZA UFISADI HIFADHI YA SELOUS ZANASWA

Na Mwandishi Wetu

UFISADI mkubwa umefichuliwa katika pori la akiba la serious Kanda ya Kusini Mashariki Liwale, baada ya mhifadhi wa pori hiyo kuhusishwa na ufisadi mkubwa wa mamiilioni ya shilingi, kuchukua kadi za benki za watumishi pamoja na kutengeneza watumishi hewa.
http://tanzaniatourismonline.com/wp-content/uploads/2016/01/Maghembe12.jpg
 Profesa. Jumanne Maghembe Waziri wa Maliasili na Utalii wizara inayosimamia Hifadhi za Taifa na mapori ya Akiba.

Taarifa iliyopatikana kutoka kwenye pori hilo, ilieleza kuwa Mhifadhi Mkuu, Salum Ramadhan Kulunge amekuwa akifanya malipo hewa pamoja na kuwalipa watumishi ambao hawajashirikishwa doria pamoja kutumia gari la serikali yenye namba  T. 753 AFA na STL 2497 kubeba mbao zilizokamatwa.

Ilisema miongoni mwa watumishi wanaoingizwa majina yao katika orodha ya watumishi wanaokwenda doria ni pamoja na Chiku Kwilasa, ambaye amekuwa akilipwa fedha bila kufanya kazi zozote huku hata jina lake likiwa halipo kwenye kitabu cha ukaguzi wa silaha na mahudhurio ofisini.

Nyaraka zingine zilionyesha kuwa mhifadhi huyo, amekuwa akiajiri watumishi hewa huku pia baadhi yao akiwa yeye ndie anashikiria kadi zao za benki, kwa kutoa fedha mbalimbali, ambapo baadhi ya nyaraka zilionyesha zaidi milioni 20 zilichukuliwa katika kipindi cha miezi minne.

JAMVI LA HABAR
Ii lilibahatika kupata majina ya watumishi kadhaa ambao zilionyesha akaunti zao ziliingizwa fedha na kutolewa na kampuni mbalimbali zinahusiana na mambo ya utalii kwenye pori hilo.

Mmoja wa watumishi hao, aliyekataa jina lake kuwekwa gazetini, alisema wameshafikisha kilio chao Wizara ya Maliasili na Utalii kueleza tatizo hilo, ambalo kwa namna moja au nyingine hakuna msaada waliopata.

"Mimi hapa sina kadi ya benki, lakini kuna hela zaidi ya milioni sita iliingizwa katika akaunti yangu na taasisi ya uwindaji ya TAWISA, na baadae ilitolewa bila hata mimi kujua, na nilipogundua baada ya kwenda benki kuomba taarifa za benki ndio nikagundua kuna kiasi kikubwa cha fedha kinaingia na kutoka,''alisema.

Aidha, alisema kuna mbao huwa tunazikamata kwa watu wanaoingia ndani ya hifadhi, ambapo huwa anazibeba na kuzipakia kwenye magari ya serikali namba hizi T. 753 AFA na STL 2497 na kuzisafirisha kwenda kuziuza.

Pia, taarifa zaidi zilieleza mkuu huyo, amekuwa hawalipi watumishi kutopata stahiki za malipo pindi wanapofanya kazi pamoja na kutoa adhabu kwa watumishi zisizofuata sheria na kanuni za utumishi wa umma.

Taarifa hiyo, ilisema kiongozi huyo, anawatimua kazi watumishi huku akishindwa kuwapa nafasi za kujitetea huku akizuia watumishi kutekeleza wajibu wao huku akiwa ni miongoni mwa vinara wanaodaiwa kuiba mbao zinazokamatwa zilizovuna kinyume na taratibu.

Hata hivyo, tulipowasiliana  na Salum alisema hawezi kusema chochote lakini tuhuma zote anazijua na kuzifahamu na hivi sasa hawezi kutoa tamko kwa kuwa Wizara inafanya uchunguzi wa suala hilo ili wachukue hatua.

"Nakuomba usitoe taarifa hadi uchunguzi utoke, yote nayafahamu hayo, nimeshatoa utetezi wangu,''alisema na kuomba aachwe.

Hivyo, alisema hawezi kueleza chochote kuhusiana na jambo hilo kwa kuwa anaamini itasababisha tafsiri tofauti kuhusiana na jambo hilo, ambalo limeonekana kuleta mambo mengi kuhusiana na swali hilo.

No comments:

Post a Comment