WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, November 30, 2016

DC KIGOMA:AWAJIBU MADIWANI WA ACT WAZALENDO - ''NISIPOFANYA KAZI YA CCM NIFANYE KAZI YA NANI?''

Mkuu wa wilaya ya Kigoma Bwana Samson Anga amethibitisha kwamba ni kweli anafanya kazi ya CCM katika kutimiza majukumu yake ya kila siku akijibu shutuma zilizotolewa na mwenyekiti wa Madiwani Mkoa wa Kigoma bwana Yunus Ruhomvya ambaye pia ni diwani wa Manispaa ya Kigoma Ujiji.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh9K3Hv6dJWlZ2kJyRTe-3_NZXW-IuJShPZWza7Kqxfu8TUZ2nPnaCFtXKFlcpTR_jUeu4BOfIs-EghevjObNtUb8fMtAOgXe29XLm8g2mv3us8s1ZOHLrjABr4B6NVk34D0KAllDyWpmWe/s1600/DSC_0259.JPG
 picha ya maktaba inamuonyesha  Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma, Charles Pallangyo (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Samson Anga.

juzi JAMVI LA HABARI liliripoti juu ya kauli ya mwenyekiti huyo wa madiwani akisema kuwa mkuu wa wilaya na ofisi yake wanakwamisha maendeleo ya manispaa hiyo kwa kufanya kazi za CCM badala ya kufanya kazi ya kiserikali na hivyo kuwakwamisha.

''Ngoja nikujibu ..wewe kwa mtazamo wako ulitegemea mimi nifanye kazi za nani?, kwa mtazamo wako wewe,...kawaulize mlitaka afanye kazi za nani?, nyinyi mlitaka afanye kazi za nani, nenda kawaulize?''. alijibu DC Anga.
                                           
Rashid Yunus Ruhomvya.
Mwenyekiti wa Madiwani wa chama cha ACT WAZALENDO mkoani kigoma

''naomba ukawaulize hao wanaolalamika kwamba  mimi nafanya kazi za CCM, Kawaulize walitaka nifanye kaze za nani?, unategemea nisipofanya kazi za CCM nifanye kazi za nani?.'' aliongeza DC huyo.

No comments:

Post a Comment