WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, November 30, 2016

Trump kutangaza baraza lake la mawaziri

Donald Trump

Rais mteule wa Marekani Donald Trump anajiandaa kutangaza mawaziri zaidi watakaohudumia utawala wake.
Ripoti zinasema kwamba Trump atamteua mshirika wake wa kibiashara wa zamani Steven Mnuchin kama waziri wa fedha.
Wawili hao walikuwa wanamiliki Goldman Sachs, kampuni ambayo Trump aliikashifu wakati wa kampeni zake.
Pia ameshiriki mazungumzo na Mitt Romney, ambaye anakisiwa kuwa mwaniaji wa wadhfa wa waziri wa mambo ya kigeni.
Donald Trump afanya uteuzi wa mapema
Bwana Romney aliyewania urais kwa tiketi ya chama cha Republican mwaka 2012, kwa wakati mmoja alimwita Trump mtu muongo.
BBC

No comments:

Post a Comment