WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Saturday, November 26, 2016

BREAKING NEWS:- MADIWANI ACT WAZALENDO WAWAVAA MKUU WA MKOA, WILAYA KIGOMA


 Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Hussein Ruhava Kushoto akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo hilo Zitto Kabwe katika picha ya maktaba

 Rashid Ruhomvya.
Mwenyekiti wa Madiwani wa chama cha ACT WAZALENDO mkoani kigoma
 Hussein Ruhava Mstahiki meya Manispaa ya kigoma ujiji akiongea na wananchi.
Hussein Ruhava Mstahiki meya Manispaa ya kigoma ujiji akiongea na wananchi.

Na. Mwandishi Wetu, Kigoma
Mwenyekiti wa Madiwani wa Chama cha ACT WAZALENDO mkoani ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya Elimu,Uchumi na Afya katika Halimashauri ya manispaa ya Kigoma Ujiji ambayo inaongozwa na chama hicho mheshimiwa Rashid Ruhomya, leo amewashtaki kwa wananchi wa Manispaa hiyo Mkuu wa wilaya ya Kigoma mheshimiwa Samson Anga kuwa anampotosha mkuu wa mkoa na mkurugenzi mtendaji wa halimashauri hiyo kwa kujikita katika kuitetea CCM na kuacha kufuata maamuzi halali ya halimashauri.

akiwahutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi katika mkutano ulioitishwa katika kata ya Kigoma mjini uwanja maarufu wa Kigoma Sinema kuzungumzia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama chao kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu wachaguliwe..

''kwa kipindi kirefu sasa Mkuu wa wilaya amekuwa akifanya kazi ya CCM, sisi baraza la madiwani tunapanga mipango ya maendeleo, tunaipitisha halafu yeye anakaa na wana CCM wenzake wanazuia utekelezaji''. alisema Ruhomvya.

''mpaka hivi sasa, baada ya mkuu wa wilaya kumvuruga mkurugenzi, na kuzuia mipango ya maendeleo, 
sisi baraza la madiwani tumempigia Kura ya kutokuwa na imani mkurugenzi wa Manispaa na tumeamua kumng'oa ili akakae na CCM wenzake''. aliongeza
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh9K3Hv6dJWlZ2kJyRTe-3_NZXW-IuJShPZWza7Kqxfu8TUZ2nPnaCFtXKFlcpTR_jUeu4BOfIs-EghevjObNtUb8fMtAOgXe29XLm8g2mv3us8s1ZOHLrjABr4B6NVk34D0KAllDyWpmWe/s1600/DSC_0259.JPG
picha ya maktaba inamuonyesha  Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma, Charles Pallangyo (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Samson Anga.

''Manispaa ni Serikali inayojitegea (is an aotonomous), maamuzi yake hakuna mamlaka ya kuyatengua, si mkuu wa wilaya wala mkuu wa mkoa, sasa namshanga huyu mkuu wa wilaya wakuja hapa anataka kutuharabia mipango yetu ya maendeleo. nawahakikishia ndugu zangu wa kigoma tutawapigania kufa na kupona na tutamshinda. maslahi ya wana kigoma lazima tuyaweke mbele kuliko vyama vyetu''. aliongeza Ruhomvya

naye Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Hussein Ruhava amewahakikishia wananchi hao kuendelea kuwatumikia kwa moyo mkunjufu na nguvu zote na kusisitiza hawatakatishwa tamaa.

''mkuu wa mkoa ameunda kamati maalum kushughulikia mradi wa Mgebuka Square, hiyo haituzuii sisi kuendelea na mradi huo, mkandarasi anaendelea kuweka Pavements na tunahakika mradi hautasimama''. alisisitiza Meya Rugava


No comments:

Post a Comment