WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, February 8, 2017

BAADA YA SOMALIA KUPATA RAIS MPYA: Mambo usiojua kuhusu rais mpya wa Somalia

Rais mpya wa Somalia Mohamed Abdullahi MohammedRais mpya wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohammed

 Rais mpya wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohammed anaitwa 'Farmajo' baada ya chakula cha Kitaliano cha Jibini
Inasemekana kwamba alipenda sana kula Jibini wakati alipokuwa kijana wakati wa ukoloni wa Italiano
Ana uraia wa nchi mbili za Marekani na Somalia na anajulikana kwa kampeni yake ya kupigania haki za kibinaadamu.
Amewahi kuhudumu kwa muda mfupi kama waziri mkuu mwaka 2011 lakini akajiuzulu baada ya miezi michache kufuatia migogoro kati yake na aliyekuwa rais Sheikh Sharrif hassa.

Hakuwa maarufu na wanasiasa wengine kwa kuwa alijionyesha kuwa mtu wa watu akipanda ndege za bei ya chini wakati alipokuwa akisafiri katika mataifa ya ughaibuni.
Miongoni mwa wagombea wote 20 ndiye aliyekuwa maarufu katika mtandao wa kijamii.
Wapinzani wake walikosolewa kwa kuungwa mkono na Kenya na hata Ethiopia.
Wafuasi wake wanapinga mataifa ya kigeni kuingilia kati utawala wa Somalia na wanataka kuona mabadiliko nchini humo.

No comments:

Post a Comment