WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Friday, February 3, 2017

BREAKING NEWS: ZITTO KABWE AIBUKIA UINGEREZA, ATETA NA KIONGOZI WA UPINZANI WA BUNGE LA UINGEREZA

  • Kuonekana kwake kwajibu Hofu na tuhuma za kujificha
  • akialika chama cha Labour katika mkutano mkuu wa Kidemokrasia wa ACT WAZALENDO
  • Labour yamthibitishia Kushiriki
Na Mwandishi wetu :  
 wakati kukiwa na sintofahamu ya kutoonekana hadharani kwa mbunge wa Kigoma mjini na kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO mheshimiwa Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto ambaye pia ametunukiwa heshima ya kiuongozi wa kimila wa kigoma kwa kuitwa MWAMI.
 Image may contain: 2 people, people standing and indoor
leo amevunja ukimya na kuiondoa taharuki hiyo iliyojengeka tangu tarehe 21 mwezi january mwaka huu alipotafutwa kukamatwa na polisi mkoani shinyanga wilaya ya kahama kwa kuonyesha picha zake akiwa nchini uingereza.

katika ukurasa wake wa facebook kiongozi huyo ameandika
 
''Leo asubuhi nimefanya mazungumzo na Kiongozi wa Chama cha Labour cha Uingereza Ndg. Jeremy Corbyn katika Ofisi ya Jimboni kwake Islington Kaskazini.
Tumezungumza kuhusu ujenzi wa Ujamaa duniani katikati ya wimbi la siasa Kali za mrengo wa kulia zinazoendelea sasa.
Image may contain: 2 people, people standing and shoes
Pia tumejadiliana wimbi la kubana uhuru wa mawazo na demokrasia Afrika na Tanzania hususan.
Nimempa rasmi mwaliko wa kuhudhuria mkutano wa kidemokrasia wa kuadhimisha miaka 50 ya Azimio la Arusha utakaofanyika jijini Arusha tarehe 25 Machi 2017. Chama cha Labour kimekubali kuhudhuria mkutano huo. Image may contain: 1 person
Ndg. Corbyn pia amenialika kwenye mkutano mkuu wa Labour ambapo Seneta Bernie Sanders atahudhuria pia''.

Zitto Kabwe

hivi karibuni mshauri wa chama hicho na mhadhiri mashuhuli nchini Tanzania Prof. Kitila mkumbo alitoka hadharani na kusema kuwa kiongozi Kabwe yupo salama na hajapotea taarifa iliyotanguliwa na ile ya kiongozi huyo kutokubali kukamatwa na polisi bila kufuata utaratibu wa kiuongozi taarifa ambayo ilisambazwa na naibu katibu mkuu wa chama hicho bwana Msafiri Abdulahman Mussa Bin Salim wa  Mtemelwa, Ipombo Nyamangalo Nkumba  Sesiamali Lwigalwike.

NB: PICHA MBALI MBALI ZINAMUONYESHA ZITTO KABWE AKIWA NA KIONGOZI HUYO WA CHAMA CHA LABOUR

No comments:

Post a Comment