WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, February 8, 2017

VITA DAWA ZA KULEVYA: MAKONDA AITIKISA NCHI - MBOWE, MANJI, GWAJIMA NA AZZAN WASABABISHA GANZI



Mbabe wa Vita  kama anavyoitwa na wengi, Paul Makonda, leo tarehe 08 february 2018 amesababisha mtikisiko wa aina yake baada ya kuwatamka washukiwa wa namna moja ama nyingine wa madawa ya kulevya na kuwataka waripoti kituo kikuu cha polisi siku ya ijumaa.
miongoni mwa waliotajwa ni pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, Mchungaji Josephat Gwajima, Iddi Azan na Yusuph Manji ambaye ni Mwenyekiti na Mfadhili wa timu ya Yanga wakituhumiwa kuhusika na dawa za kulevya

Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es salaam leo ameingia awamu ya pili ya kupambana na madawa ya kulevya na ametaja watu hao wanaotuhumiwa kuhusika na madawa ya kulevya kwa namna moja ama nyingine.

Makonda: ''Awamu ya pili ya kupambana na madawa ya kulevya tumeianza leo''.

Makonda: ''Nina orodha ya watu wengine ambao wanatakiwa kuripoti polisi siku ya Ijumaa''

Makonda: ''Tutapita nyumba kwa nyumba, kila nyumba inayohisiwa, tutaingia, nawashukuru wenyeviti wa mitaa''

Makonda: ''Hii vita tukishindwa, tumeshindwa wote, kuna watu wamekaa wanafikiri Makonda atashindwa''

Makonda: ''Leo nina majina 65, juzi ile walikuwa kumi na kitu, mtasikia mtikisiko kidogo. Nataka tukutane nao''.

Makonda: ''Wa kwanza ni mmiliki wa Slip Way, wenye klabu ya Yatch Klabu, Salehe wa MMI, Mwinyi Machapta''

Makonda:''Kuna dada yangu anaitwa Rose yuko China, kuna Mzee wangu anaitwa Kiboko anaishi Mbezi''

Makonda: ''Kila tunayemuita ajue tunamfahamu kuliko anavyofikiri. Kuna mtu anaitwa Hafidh anaishi Mbezi Mwisho''

Makonda: ''Kuna kaka yangu mpendwa mbunge mstaafu, Idd Azzan, naye namuhitaji''

Makonda: ''Kuna kaka yangu Aikael Mbowe Mbunge wa hai ambaye ni mkazi wa DSM, kuna Bossi Kizenga wa Bunju''

Makonda: ''Nassoro Selem wa Mabibo, kuna ndugu yangu Hussein Pamba Kali, pamoja na Mchungaji Gwajima''

Makonda: ''Pamoja na kaka yangu Yusuph Manji pia namuhitaji, Mmiliki wa Sea Clif pia namuhitaji''

Endelea kufuatilia ukurasa huu tukujuze mengi zaidihttps://i1.wp.com/www.darpost.com/wp-content/uploads/2016/04/paul-makonda.jpg?fit=1200%2C800Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda

No comments:

Post a Comment