WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Friday, February 17, 2017

TUNDU LISSU AMVAA MWAKYEMBE SAKATA TLS


Tokeo la picha la tundu lisu
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt Harrison Mwakyembe jana alisema kuwa atakifuta Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society (TLS)) kwa madai kuwa kimesahau misingi yake na kuanza kufanya kazi kama chama cha siasa.

Waziri Mwakyembe alisema kuwa, kama wanataka kufanykazi kama chama cha siasa, basi yeye ataongea na msajili wa vyama vya siasa nchini ili cha hicho kipya kisajiliwe.

Kufuatia kauli hiyo, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Mbunge wa Singida Mashariki na mgombea Urais wa TLS, Tundu Lissu ameandika waraka huu kwenda kwa wanasheria wenzake.

Mawakili wenzangu. Mimi binafsi sijashangazwa na kauli ya Dkt. Mwakyembe kwamba ataifuta TLS kama itajiingiza katika harakati za kisiasa. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa serikali ya Tanzania kutoa vitisho vya kuifuta TLS.

Waziri Mkuu hayati Edward Sokoine aliwahi kutishia hivyo katika kilele cha vita dhidi ya wahujumu uchumi miaka ya mwanzo ya ’80. Na hata kabla ya hapo katika miaka ya ’60 na ’70 watangulizi wa Sokoine walijaribu kufanya hivyo hivyo. In fact, kuanzishwa kwa Tanzania Legal Corporation kipindi hicho kulikuwa driven in part na jitihada za kuondoa the private bar.

Vitisho dhidi ya TLS vilirudi miaka ya ’90 wakati wa Lyatonga Mrema. Kitu kimoja kiko common katika vitisho hivyo vyote. Vitisho hivi vimetolewa kila wakati TLS na private bar wanapo-assert their independence na wanapoanza kutetea utawala wa sheria na kupinga state lawlessness and impunity of the rulers.

Mawakili wakiwa kimya na TLS ikiwa mfukoni mwa serikali na wasipohoji matumizi mabaya ya madaraka basi wanakuwa darlings wa serikali.

Kuna kitu kingine ambacho ni common katika vitisho hivi. Havijawahi kufanikiwa na havitafanikiwa. Sheikh Abeid Amani Karume alipiga marufuku private legal practice mara baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya ’64. Tanzania ya leo sio Zanzibar ya miaka ya ’60 na ’70, hatutakubali udikteta wa aina ya Karume au wa aina nyingine yoyote kwenye Tanzania ya leo.

Inaelekea Dkt. Mwakyembe hafahamu au anajisahaulisha jinsi ambavyo TLS na mawakili binafsi walivyo embedded kwenye mfumo wetu wa kikatiba na kisheria. Simply put, ukifuta TLS maana yake ni kwamba hakuna wakili binafsi hata mmoja nchi nzima. Mfumo mzima wa kimahakama unategemea uwepo wa mawakili na kwa hiyo uwepo wa TLS. Mahakama karibu zote zitashindwa kufanya kazi kusipokuwa na mawakili binafsi. The same applies to various tribunals and other judicial and quasi judicial bodies.

Aidha, kuna taasisi nyingi zilizoundwa na Katiba yetu kama vile Judicial Service Commission na Law Reform Commission ambazo zinakuwa properly constituted kukiwa na uwakilishi wa TLS. Kuna taasisi nyingine nyingi ambazo zimeanzishwa na sheria za kawaida ambazo composition yake inakamilika kukiwa na representation ya TLS. Hiyo legal, constitutional and political upheaval itakayotokana na kufutwa kwa TLS will be unprecedented and unimaginable kwa mtu mwenye akili timamu.

Dkt. Mwakyembe ana akili timamu. He must be joking. Hawezi kufuta TLS. Anachotaka kufanya ni kuwatisha mawakili ili wachague watu wale wale wa miaka yote kuongoza TLS. Anatutisha ili tuendelee na status quo katika uongozi wa TLS. Hataki tufanye mabadiliko yanayohitajika ili TLS yetu isichukue nafasi yake stahiki katika kuamua mustakbala wa nchi yetu na wa taaluma yetu.

Nawataka viongozi na wanachama wa TLS wamkemee Dkt. Mwakyembe in the strongest possible terms. Nawataka wagombea wenzangu wa nafasi mbali mbali za uongozi katika TLS wajitokeze hadharani na kulaani kauli ya Dkt. Mwakyembe in no uncertain terms. Wakinyamaza tutawajua wako upande wa nani: status quo au mabadiliko. And I’ll ask you all to vote accordingly.

 Tundu Lissu

No comments:

Post a Comment