WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, October 12, 2016

BREAKING NEWS: TANZIA CUF YAPATA MSIBA MZITO

marehemu  Ashura Mustapha enzi za uhai wake.

INNAA LILLAAHI WA INNAA ILAYHI RAAJI'UUN!
Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi na Mkutano Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa, Mheshimiwa Ashura Mustapha (pichani), amefariki dunia, leo asubuhi, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa siku chache zilizopita!
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Habari wa CUFm Taifa, Mheshimiwa Abdul Kambaya, msiba wa marehemu upo Mburahati eneo la Kwa Jongo, wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho mchana, inshaaAllaah.
Ee Mwenyezi Mungu Muumba wa vyote, nakuomba idhini yako umghufirie, umrehemu na umpe makazi mema ya peponi dada yetu mpendwa, Mheshimiwa Ashura Mustapha. AMIN.

No comments:

Post a Comment