WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Friday, October 21, 2016

BREAKING NEWS: UKATA WALITANDA BUNGE, LAKAUKIWA FEDHA LASHINDWA KUTOA PHOTOCOPY

hali ya ukata wa kifedha inayolikabili taifa sasa imehamia katika Ofisi za Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania  amefichua Mbunge wa Kigoma mjini na kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO Zitto Kabwe , kiasi cha kushindwa kutoa photocopy nakala za mapendekezo ya muswada wa sheria ya habari.
 Spika wa Bunge Job Ndugai.
mbunge huyo ameyasema hayo katika andiko lake alilokuwa akimjibu waziri wa habari vijana utamaduni sanaa na michezo Nape nauye aliyeandika andiko la kumtak aache unafiki kuhusiana na msimamo wake katika muswada huo.
hapa chini ni sehemu ya maandiko ya mbunge huyo kijana kutoka kigoma.
Kanuni za Bunge ( kanuni ya 84 ) zinataka kwamba Muswada ukishasomwa Kwa mara ya kwanza Bunge lifanye MATANGAZO Kwa umma ili kuhakikisha kuwa umma unaelewa maudhui ya muswada na kuwezesha Wananchi kutoa maoni Yao. 
                                                         Wabunge wakiwa kazini Bungeni.

Muswada huu kwanza Bunge halikutoa matangazo yeyote ( Kwa Taarifa tu Ni kwamba Hata Kamati ya Bunge ilishindwa kutoa photocopy nakala za uchambuzi wa muswada kutoka Kwa wanasheria wa Bunge Kwa sababu Bunge halina Fedha. Bunge halina Fedha kutoa photocopy ya nyaraka za Wabunge kufanyia Kazi ). 
Wadau wote waliokuja mbele ya Kamati ya Bunge walitamka dhahiri kwamba wamepewa Taarifa ya kutokea mbele ya Kamati Siku 2 kabla ya vikao Na hivyo wameomba muda zaidi wa kutoa maoni Yao. Labda Ni kutokana Na uchanga wa shughuli za Bunge, 
                                                         Mbunge wa kigoma mjini Zitto Kabwe
Waziri anajenga Hoja kwamba Ushiriki ulianzia kabla. Mtu yeyote anayejua namna Bunge linafanya Kazi atakwambia muswada Ni muswada pale ambapo umechapishwa kwenye gazeti la Serikali Na kusomwa mara ya kwanza Bungeni. 

limenukuliwa andiko hilo la Zitto Kabwe

No comments:

Post a Comment