WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Tuesday, October 11, 2016

MTATIRO AUMBULIWA NA NUKUU ZAKE

Ukiwa Muongo shurti uwe na kumbukumbu ndivyo wasemavyo waswahili, lakini pia ili kuwa na msimamo lazima uweke akiba ya maneno wanaongeza waswahili hao hao.

maneno hayo ya wahenga yanaonyesha kuwa mwiba mchungu kwa Mwanachama wa chama cha wananchi CUF Julius Mtatiro baada ya wanasiasa kadhaa mitandaoni kusambaza nukuu zake akiwabeza waliokuwa wanamuunga mkono Edward Lowassa wakati yupo CCM na kuwahusisha na kununuliwa na kwamba anawashangaa kwanini viongozi wa dini wamekubali kununuliwa kirahisi hivyo huku akiamini ukiwa na pesa tanzania unaweza fanya lolote.

NUKUU YAKE HII HAPA CHINI


NJAA HADI KWENYE NYUMBA ZA IBADA!!!!

Wachungaji wa makanisa mbalimbali ya Kikristo wakiandamana muda huu kwenda nyumbani kwa Edward Lowassa kumshinikiza achukue fomu ya kugombea Urais.

I hope mapadre hawamo humo! Mungu atuepushie!
Yani kanchi ketu haka kanaendeshwa kwa ujanja ujanja na wiziwizi tu.

Mtu akiwa na hela zake basi anafanya jambo lolote tu, Duh!

Julius S. Mtatiro
23.03.2015

2 comments:

  1. Nafikiri Unapokuwa unatoa maoni, katika suala fulani, unaouhuru wa kulizungumza unavyoliona na kama lilivyo. Sio kweli kuwa maoni yako ndio intellectual and objective opinion ambayo utahukumiwa nayo katika dunia ya kitaaluma. Katika hili mtatiro alitoa maoni yake na nina imani yalishawishiwa sana na utashi wa ushindi katika uchaguzi, ndio maana ukitafuta maoni yake baada ya Mzee Kupiga about turn utaona alichozungumza ni kinatofautiana na yeye.

    ReplyDelete