WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Tuesday, October 11, 2016

CUF CHINI YA LIPUMBA NI SAWA NA UKAWA BILA CUF,


wenyeviti wenza wa UKAWA freeman Mbowe wa CHADEMA Kushoto, Prof. Ibrahim Lipumba wa CUF katikati na James Mbatia wa NCCR-MAGEUZI kulia .

 Anaandika NJANO TANO

Tunakumbushana tu, tufanye siasa ndani ya nchi yetu, vyama vyetu kwa kuongozwa na haja ya kutaka kuleta mabadiliko katika jamii ya kitanzania na si kwa lengo la kutibu njaa ambayo twajua tiba yake ni kifo tu,,,, chakula ni dawa tu ya kutuliza maaumivu....

Ni njaa pekeee ndio inayo fanya wasomi na watu wenye akili timamu kukanyaga misimamo yao bila kuzingatia taratibu au miiko waliyojiwekea wenyewe!!!! njaa mbayaaa sana!!!!

Ni njaa pekeee,,, ndiyo inayo wafanya watu wamkumbatie Lowassa mwenye kashfa ya Ufisadi na kuhonga au kununua watu na KUMKANDAMIZA kabwela Lipumba ambaye pamoja na makosa yake(kama anayo) watu wanahangaika kumtoa katika uenyekiti kwa kutumia nguvu ya fedha za Rushwa wanazo zipata kutoka kwa Lowassa badala ya nguvu ya kikatiba na kanuni walizo jiwekea...

Tunajua,,, CUF chini ya Lipumba ni sawa kabisa na UKAWA bila CUF, na yule mwenye uchu na uroho wa kuwa rais hawezi kukubali hata kidogo kuona Lipumba anaendelea kuwa mwenyekitiii......wa CUF.
Lipumba kavunja rekodi, naeza kusema, tumezoea vyama vyetu kumfukuza kama mbwa mtu wanaye muona tatizo ua kirusi, na huyo mtu kufukuzika na kwisha kisiasa kabisa!!!

Lipumba sasa unakwenda huu mwezi wa tatu nafikiri,,, bado wanasumbuana na hao wanao jiita chama, huku hao wajitao chama wakitamba haikuwahi kutokea mtu akashindana na chama alafu ashinde,,,,,,
Kwa mambo yanavyo endelea, na mgogoro usivyo tabirika, binafsi nina shaka na hao wanao jiita chama na wanao muita Lipumba kirusi. Tumezoea virus katika vyama vyetu kutimuliwa siku moja tu,,, na kisha kwenda kupotelea kwa msajili au mahakaman kama kikimbilia huko..... mifano ipo,,,,

Lakini kirusi Lipumba aidha kimekuwa sugu kinachoweza kumuua CUF, au Lipumba si Kirus bali yeye chini ya CUF anapambana kirusi,,,,.. nani chama hasa chama kati ya Julius Sunday Mtatiro na Lipumba??? Nani anashindana na CUF kati ya hao???

Sijui,, lakini KUBADILIKA kwa msimamo wa Mtatiro juu ya kashfa zinazo mkabili Lowassa, na ukizingatia kulikuwa na njaa kanisani iliyopelekea wachungaji kumuunga mkono Lowassa, na hivyo basi dhahiri njaa ile sasa iko UKAWA, na njaa hiyo ndio anayo pambana nayo Lipumba.

Vyovyote iwavyo,,, Lipumba andelee kuwa mwenyekiti au mumtoe kwa kutumia nguvu ya fedha ya Lowassa, bado Lipumba atabaki kuwa MSHINDI tu, sababu anacho kisimamia kina mashiko, lakini unachokisimaia Mtatiro hakina mashiko hata kidogo.


No comments:

Post a Comment