WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Saturday, October 15, 2016

HUU NI UBINAFSI WA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU AU ATHARI ZA SIASA VYUONI?

Na Noel Nguzo.
 
Wahitimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam katika picha.
 
Mwaka 1966 chuo kikuu cha Dar-es-Salaam kulitokea mgomo mkubwa sana wa wanafunzi.Mgomo huo uliopelekea jmla ya wanafunzi 400 wa chuo hiko kufukuzwa kabla ya 392 katiki yao kurudishwa chuoni hapo uliongozwa na aliyekua kiongozi wa serikali ya wanafunzi wakati huo Samweli Sitta na marehemu Wilifred Mwabulambo.
Sababu za mgomo huo  unadaiwa kuwa wa kihistoria zilikua ni kupinga kujiunga na jeshi la kujenga taifa(J.K.T) na kukatwa mshahara,mishahara minono ya wanasiasa na viongozi wa serikali.

Mwaka 1989 chuo kikuu cha Dar-Es -Salaam ,kulitokea mgomo mwingine mkubwa uliongozwa na kiongozi wa serikali ya wanafunzi wa chuo hiko wakati huo Bw Matare Matiko.Katika mgomo huu sababu za wanafunzi kugoma zilikua ;-mauaji ya wafugaji wilayani Kilombero,adha inayotokana na dampo la uchafu la tabata,ubovu wa kivuko cha kigamboni kilichodaiwa kuharibika siku mbili baada ya kununuliwa.

Nchini Kenya mwishoni mwa mwezi septemba kulitokea mgomo katika chuo cha Multmedia University(M.M.U) chuo hiki kipo  kusini mwa Nairobi katika mji wa Ongata Rongai. Chuo  Multimedia University(M.M.U) kipo takribani kilometa 25 kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo.Sababu ya mgomo huo ni wanafunzi wa chuo hiko kuungana na wakazi wa mji wa Ongata Rongai kupinga undeshaji wa hovyo wa madereva wa matatu yanayofanya ruti ya Nairobi-Ongata Rongai.
Chuo Kikuu cha Dodoma.

Hiyo ni mifano ya migomo ya baadhi ya vyuo vya nchi nyingine na migomo ya baaadhi ya vyuo vya hapa nchini ambayo sababu za migomo hiyo ni changamoto za jamii nzima zinazozunguka vyuo hivyo.Mambo yanaonekana kua tofauti sana kwa wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini kwa wakati huu.

Kipindi hiki licha ya jamii nyingi kukumbwa na changamoto nyingi mno,wanafunzi wengi wa vyuo vikuu hawaonekeni kuguswa nazo.Sisemi migomo ni mizuri au changamoto zilizopo zitapata utatuzi ikiwa wanafunzi wa vyuo vikuu watagoma,ninachojaribu kukionesha ni sauti za wanafunzi wa vyuo vikuu katika changamoto za jamii za kitanzani.Leo ukisikia mgomo chuo flani basi tatizo ni mikopo tu.Migomo mingi ya wanafunzi wa wakati huu ni ile inayohusu maslahi yao wenyewe tu basi.

Katika kipindi cha miaka miwili 2007-2009 nchi yetu ilikumbwa na janga la mauji ya  watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).Inadaiwa kuanzia mwezi june 2007 mpaka februari 2009 jumla ya watu wenye ulemavu  wa ngozi 43 walidaiwa kuuwawa.Ukubwa wa tatizo ulisababisha tar 4/9/2008 Bunge la nchi za umoja wa ulaya kutoa tamko la kuridhia juhudi za serikali kuchukua za kupambana na mauji hayo.Hakuna serikali ya wanafunzi wala wanafunzi wenyewe kuonesha kuguswa na tatizo kiasi cha kupaza sauti zao sawasawa.

Nchi imepita kwenye matukio yenye kugusa maslahi mapana ya taifa kama vile Buzwagi,sakata la ukwapuaji wa bilioni 306 kwenye akount ya Escrow mwezi nov mwaka 2014,sakata la Epa,Richmond na hivi karibuni tetemeko la ardhi lililotokea Bukoba wilayani Kagera tarehe 10/9/2016 na kusababisha vifo vya watu 16 na wengine kadhaa kujeruhiwa.Hakuna sauti,pole wala mchango unaokaribiana na hadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu uliofanyika ilihali mpaka wafanya biashara wa kariako wameshiriki(wanaweza kujiteteta vyuo vilifngwa) lakini pesa za serikali za wanafunzi zipo muda wote.

Kasumba hii ya kuacha kujishughulisha na mambo ya msingi ya jumla jumla nje ya mambo yao binafsi imeanza kuwaathiri hata wao wenyewe kwa kuanza kubaguana.Itakumbukwa tarehe 28/mei/2016 zaidi ya wanafunzi 7000 waliokua wanasoma ualimu ngazi ya stashahada maalum ya sayansi walitimuliwa na serikali.Kama nguvu ya wanafunzi wa vyuo vikuu wanayoitumia kudai mikipo yao wangeitumia katika sakata lile serikali isingeweza kuwapa masaa 24 wanafunzi wale waondoke na wala kusingekua na mwanafunzi aliyelala stand kama ilivyoripotiwa.Kwakua haikua mkopo halikua jambo muhimu sana kwao.

Nimewahi kuambiwa kuna chuo kikuu flani mkoani Dodoma   kuna bango lenye rangi na jina la chama cha kimojawapo cha siasa nchini kwenye geti kuu la kuingilia chuoni hapo lakini chuo hikohiko hakina bango lenye kukitambulisha chuo hiko unapongia chuoni hapo kama ilivyo kwenye vyuo vingi duniani.Pamoja na tatizo hili wanafunzi hawaoni kama ni muhimu sana kuwepo kwa bango lenye jina la chuo kuliko nembo na jina la chama cha siasa.Wapo kimya kwa sababu sio mkopo.Tarehe 2/6/2016 rais Magufuli aliwapiga wanafunzi wa vyuo vikuu kuacha siasa mavyuoni,marufuku hii ni vyema ikaenda sambamba na uondoaji au ukomeshwaji wa alama,au uvaaji wa sare za vyama ndani au karibu na maeneo ya vyuo.Bango hili la lipo chuoni hapo  mpaka leo ni kwakua sio mkopo.

Kubwa kuliko yote ni  ushiriki wa wanafunzi wa vyuo vikuu katika zoezi la uchaguzi mkuu.Katika chaguzi kadhaa hasa za mwaka 2010 na mwaka 2015 wanafunzi wa vyuo vikuu wengi walishindwa kushiriki kwenye zoezi hili kwakua uchaguzli ulifanyika vyuo vikiwa vimefungwa wakati waliandikishwa mavyuono na ndipo wanalistahili kupigia kura.Husikii wakati huu wakifanya harakati za kuhakikisha tume ya uchaguzi inatatua taizo hili,wapo kimya kelele chache wanazopiga vipindi vya uchaguzi zinatosha kwakua uchaguzi kwao sio mikopo.

Itakumbukwa kwenye uchaguzi uliofanyika 31/10/2010 katika watu takribani milioni 19 na zaidi waliojiandikisha kupiga kura ni watu milioni tisa na kitu tu ndio waliojiotokeza huku uchaguzi uliofanyika 25/10/2015  watu zaidi ya mulioni 23 walijiandikisha lakini waliopiga kura ni watu watu wasiozidi milioni 16.Ni kweli kwamba sio wote wasiopiga kura ni wanafunzi wa vyuo vikuu lakini ni ukweli pia sehemu kubwa ya wasiopiga kura ni wanafunzi wa vyuo vikuu.Katika mazingira ya kawaida kama msomi wa chuo kikuu haoni tatizo la kutopiga kura kwenye uchaguzi mkuu nini unategemea kwa wananchi wa kawaida wanoamini katika usomi?
 

Kimsingi wanafunzi wa vyuo vikuu wa kipindi hiki kwa kiasi kikubwa kumezwa na siasa za vyama.Siasa zimeathiri mno wanafunzi wa vyuo vikuu kiasi hata kuchaguza viongozi wa serikali zao wakati mwingine kunatokana na vyama wanavyotoka wagombea.Jambo hufanya hata mambo makubwa yanayotokea katika taifa letu kupokelewa na wanafunzi kulingana na mitazamo ya vyama vyao au itikadi za vyama hivyo.Wakati mwingine inawezekana ni ubinafsi tu wa wasomi .

Inawezekana jibu la baadhi ya wanafunzi ni sheria za chuo zinavyowabana kushiriki kwenye matukio haya.Kuna baaadhi vya vyuo ni marufku mwanafunzi kuongea na chombo cha habari au kujitambulisha ni mwanafuzni wa chuo fulani katika baadhi ya masuala.Lakini mnona hakuna chuo kinachoruhusu migomo na bado mnagoma mikopo ikichelewa?

Kwa kipindi cha hivi karibuni wasomi wengi nchini,wanataaluma kwa kiasi kikubwa wameacha kujishuglisha na mambo ya juma yanayozikumba jamii zetu.Wengi wameacha usomi wao na kukimbilia kwenye siasa kama sehemu ya kukidhi mahitaji yao ya kisiasa.Majina mengi yanayotajwa ya mafisadi,wala rushwa ni ya wasomi.Kwakua walioko mavyuoni hujifunza kwa wasomi waliomaliza imawezakna wamerithi ubinafsi huu.

Mimi binafsi kuna wakati niliwahi  kukaa na baadhi ya wakazi wa mkoa mmoja wapo wenye vyuo vingi nikawauliza wananufaikaje na uwepo wa wingi wa vyuo katika mkoa wao?,walichonijibu faida zaidi ya kuongeza mzunguko awa fedha kwa kuruhusu biashara nyingi hakuna,wanapenda faida za kudumu kwakua wakiondoka tu basi na biashara hudorora.Ni wakati wetu sasa wanafunzi wa vyuo vikuu kushiriki kikamilifu katika changamoto mbalimbali zinazozikumba jamii zetu.

                                    Imeandikwa na Noel Nguzo.
                          mwanafunzi chuo kikuu cha Dodoma (UDOM)
                                            0719755066

No comments:

Post a Comment