WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Saturday, October 15, 2016

MAKALA: WASOMI WETU MNATUCHANGANYA MNO

 
Prof. Kitila Mkumbo, Mwanazuoni Mashuhuri nchini Tanzania.
Siku za hivi karibuni kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kulikua na mjadala mkali sana kuhusu hali ya uchumi katika nchi yetu.Mjadala huu ulikolezwa zaidi na kauli ya Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Mh Freeman Mbowe kwamba kila mtanzania anadaiwa takribani milion moja kama sehemu ya mgawanyo wa deni la taifa(trilion 51),Inadaiwa uchumi wetu umedorora na rejea zikitolewa kama kuongeza kwa deni lataifa kwa miezi kumi toka trilion 49 mpka 51 na kitu(ongezeko la trilion 2).Kushuka kwa pato la taifa kwa robo ya kwanza ya mwaka 2016 toka 5.7% mpaka 5.5% (tofauti ya 0.2%).

Ni mjadala huu ulimuibua gavana wa bank kuu na baadhi ya wasomi na  " wachambuzi " wengine wa masuala ya kiuchumi kueleza namna ambavyo uchumi wetu ulivyo imara.Tatizo ni moja tu inatumika lugha ngumu kuelezea jambo jepesi.Wasomi wetu wanatumia misamiati migumu sana kubadilisha tunachokiona,tunachokihisi na tunachoishi.

Kwetu sisi tuliowengi hatuhitaji maelezo ya kisomi kutambua uwezo wa kifedha wa serikali,hatuhitaji ma-G.D.P,sijui micro na macro economy, viashiria vya ukuaji wa uchumi, na lugha nyingine ngumu ngumu.Kinachofanyika sasa ni sawa na kuelezwa uzuri wa maisha ya nyumbani kwako wakati wajua mara kenda unazolala na njaa.Sisi tusiosoma tuna maeneo matatu tu ambayo hutumia kutambua uwezo wa kifedha wa serikali yetu.(.1).HUDUMA ZA JAMII,(2) MASLAHI YA WATUMISHI WA UMMA,(3) MIUNDO MBINU.

                                                       HUDUMA ZA JAMII
Sisi tusiosoma hili ni eneo tunalotumia kutambua uwezo wa kifedha wa serikali yetu.Kudai serikali ina pesa huku tukitambua ubovu wa huduma za kijamii ni kutogmbanisha na serikali,
Mabadiliko makubwa ambayo yanaonekana kwenye eneo hili ni mabadiliko ya kiutendaji, hayana uhusiano wowote na uwezo wa kifedha wa serikali.Kwamba wakati huu walau kazi zinafanywa,tunaheshimiana kiasi na ipo nidhamu kwa watoa huduma,japo wengine wanasema ni nidhamu inayotokana na hofu,jambo la msingi ipo nidhamu.

Lakini changamoto za msingi zinazotokana na uwezo mdogo wa kifedha wa serikali zipo au zimeongezeka,ni kweli kwamba bado dawa na vifaa tiba havipo mahospitalini kama ambavyo ilivyokua wakati wa serikali ya awamu iliyopita.Wakati huu kuna kelele nyingi kwa sababu wezi wa milion 7 kwa dakika wamekamatwa,watumishi hewa wameondolewa,ujanja ujanja haupo banadarini,T.R.A wanavunja rekod za makusanyo kila mwezi,

Hata huu utamaduni mpya ulioibuka sasa wa kutumia harambee na michango kutatua matatizo ambayo moja kwa moja ni jukumu la serikali,unatufanya  tushindwe kuelewa mnachotueleza kuhusu uwezo wa kifedha wa serikali yetu.Tulipaswa kuiona nguvu ya serikali yetu kiuchumi kwenye tatizo la madawati,tulipaswa kuiona nguvu ya serikali yetu kifedha kwenye tetemeko la Bukoba.Hawa wafanyabiashara tuliowakwepa kutuchangia wakati wa kampeni ndo hawahawa tunawakusanya kuwaomba misaada!!

Kuona ni kuamini na bahati nzuri fedha sio hewa, wasomi wetu kuliko kutumia nguvu nyingi kuelezea ni bora mkatuacha tuone.


                                                      WATUMISHI WA UMMA.
Hili ni eneo lingine tunaloweza kuthibitsha uwezo wa serikali kifedha,Ukiacha ongezeko lilitokana na punguzo la kodi(PAYEE) la 2% mwaka huu watumishi hawakupata nyongeza ya mshahara ya kila mwaka (annual increament),kodi za nyumba zinapanda,nauli zinabadilika,ada za shule zimepanda mishahara imebaki kama ilivyo,hapa unawezaje kueleweka ukisema serikali ina pesa?

Mpaka sasa watumishi wengi wenye kustahili kupanda madaraja hawajapanda,wengine inadaiwa walipandishwa na wakashushwa.Kuna taarifa zisizothibitishwa kwamba serikali imeamua kuutumia mchakato wa uhakiki kama sababu ya kutopandisha madaraja,Taarifa hizi zinapewa nguvu na uweli kwamba uhakiki umechukua mda mrefu sana tena kwa kurudiwa rudiwa,Serikali ya awamu ya nne ilitumia sana neno "mchakato" kama sababu ya kupooza mambo magumu,serikali hii inaonekana kutumia mno neno "uhakiki" katika namna ile ile ile iliyotumiwa nenp mchakato na serikali ya awamu ya nne.

Serikali inakuaje na pesa ikashindwa kuajiri? walimu wametosha?vijana waliomaliza vyuo vikuu mwaka 2015 na 2016 wa taaluma mbalimabli zeney kuhitajika serikali wapo hawajajiriwa.

                                                      MIUNDOMBINU.
Walau ununuzi wa ndege mbili na ujenzi wa kiwanja cha ndege chato unaweza kuonekana kama moja ya mambo yenye kuonesha uwezo wetu kiedha,Lakini hizi ndege wanatumia wakina nani?Kwa nini isiwe barabara ya lami kule ifakara panapolimwa mpunga?Katika lundo la changamoto za miundo mbinu tukaamua kuanza na ndege?

Sehemu kubwa ya miradi na miundo mbinu tulioyonayo wakati huu ni matokeo ya serikali iliyopita.Serikali ya awamu ya tano bado kupitia miundo mbinu haijaweza kutuonesha ni kweli makusanyo ya kodi yameongezeka,ni kweli kulikua na pesa zinapotea kupitia watumishi hewa,ni kweli wanafunzi hewa na wanufaika hewa wa mikopo waleta hasara zipi.


Ieleweke hakuna anayetamani kuona serikali inashindwa au kufeli ,ikifeli serikali tumefeli wote,lakini haukuna sababu kutumia usomi wetu kiasi cha kutumia lugha ngumu kuelezea mambo mepesi.Uchumi wetu ukiwa sawasawa hutotohitaji tutangaziwe wala kusimuliwa,tutauona sokoni,tutauiona hospitalini,tutauona mshuleni,tutauona kwenye mishahara yetu,tutauona kwenye barabara tutauona,tutaouna,tutauona,tutauona hatutohitaji uchambuzi kama hu wa sasa


                       Imeandikwa na Noel Nguzo
                            simu 0719755055

No comments:

Post a Comment