WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Saturday, October 1, 2016

Maganda ya chungwa yampatia shilingi milioni 100

http://ichef.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/5DF3/production/_91415042_orangepeels.jpg

Msichana wa miaka 16 nchini Afrika Kusini amejishindia zawadi ya maonyesho ya Google kwa kutumia maganda ya chungwa kutengeza kifaa kinachosaidia udongo kuhifadhi maji.
Kiara Nirghin aliwashinda wanafunzi wengine duniani kwa kujipatia ufadhili wa masomo wenye thamani ya dola 50,000 kwa ''kukabiliana na kiangazi kupitia chungwa''.
Kazi yake inajiri kufuatia kiangazi ambacho kinaendelea kuathiri Afrika Kusini.

Kiangazi hicho ambacho ni kibaya zaidi kuwahi kutokea tangu 1982 kimeathiri mimea huku mifugo ikifariki.
Kwa sasa anatumai kwamba mbinu hiyo inaweza kuwasaidia wakulima kuhifadhi fedha pamoja na mimea.

No comments:

Post a Comment