WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, October 19, 2016

MEYA BONIFACE : MRISHO GAMBO AMETUMWA NA MAGUFULI KUFANYA ALIYOYAFANYA

katika Ukurasa wake wa facebook, meya mstaafu wa kinondoni na meya mtarajiwa wa Ubungo, Boniface Jacob ameandika maoni yake kuhusiana na suala la mgogoro uliojitokeza mkoani arusha kati ya mkuu wa mkoa huo Mrisho gambo na mbunge wa arusha mjini Godbless lema. zaidi soma mwenyewe
 
SI MARA YA KWANZA SERIKALI YA MAGHUFULI KUKWAMISHA MIRADI ENEO LA WAPINZANI.

By Boniface Jacob

Maoni yangu ni kuwa  sijaona jipya juu ya kilichotokea jana Arusha mbele ya Mbunge Godbless Lema.
Hao wakuu wa mikoa na makuu wa wilaya, wamepewa "maagizo maalum" ya kukwamisha wapinzani katika maendeleo kwa kipindi cha miaka mitano,na atakaye kwamisha vizuri kama MRISHO GAMBO anapewa promotion.

Hao wakuu wa mikoa na wilaya "wanamafunzo maalum" ya kuwakosea heshima viongozi wa upinzani kwenye maeneo yao na yeyote atakayeonekana anawapa ushirikiano wapinzani uhamishwa eneo hilo haraka sana kama ilivyokuwa kwa  FELIX NTIBENDA ili aletwe kiboko ya wapinzani(mvurugaji)

Mimi simuoni MRISHO GAMBO kwenye tukio lile la jana bali namuona mheshimiwa Rais John Pombe Maghufuli kupitia mkuu wa mkoa,yaani MRISHO GAMBO amemkosha sana moyo mheshimiwa Rais,sitegemei kuona anakemewa bali anapewa nafasi nyingine ya juu zaidi(kavuruga vizuri)
Serikali haijali juu ya kukosa au kupoteza mradi wa billioni 9 kutoka kwa Bill and merinda gates foundation au Martenity Africa,nilishashuhudia kwa macho yangu wafadhili wameambiwa waondoe billioni 3.2 manispaa ya kinondoni kutoka kwenye barua rasmi ya serikali,(Naibu katibu mkuu ambaye sasa hivi ni katibu mkuu rasmi) sababu tuh ni kuwapa (kick) wapinzani.

Mheshimiwa Godbless Lema ameivua ngozi ya kondondoo serikali na kutuonyesha "chui serikali" alivyo,ili wananchi wasidanganyike tena wakisikia wanaambiwa hapa kazi tu,maendeleo hayana chama,mara tunajenga nyumba moja tusigombee fito,kauli hizi zote ni za kinafki.

1.Manispaa ya moshi(WAPINZANI) imekataliwa mradi wa ujenzi wa stendi na fedha ni zao wamekopa benki,waziri TAMISEMI kaagizwa asiwasainie wakati mradi kama huo umekubaliwa manispaa ya morogoro(CCM).

2.Manispaa ya bukoba (WAPINZANI) imekataliwa kujenga mradi wa stendi mpya ya mabasi billioni 5,waziri TAMISEMI amekatazwa kusaini,Mradi kama huo umekubaliwa Geita kujenga machinjio billioni 16(CCM).

3.Manispaa ya kinondoni imekataliwa kupewa ruhusa ya kuingiziwa mitambo yenye thamani ya billioni 3.2 ya uchakataji taka,mpaka walipe kodi,pia katibu mkuu TAMISEMI amegoma kutia saini barua ya kuruhusu mkopo wa billioni 14 wakati manispaa ya Temeke (CCM) wamesainiwa mkopo wa kiasi hichohicho cha billioni 14.

This is foreign aids and opposition's projects frustrations.

NASHUKURU KABLA SIJAFA
WATANZANIA WANAZIONA RANGI NA ROHO ZA VIONGOZI WA SERIKALI HII YA CCM

Na Boniface Jacob
Meya mstaafu kinondoni.

No comments:

Post a Comment