WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, December 22, 2016

MKAKATI KUTOKOMEZA UKATILI WA WANAWAKE NA WATOTO .


ummy
Ummy Mwalimu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Na Beatrice Lyimo- MAELEZO
SAWA  wa  kijinsia  unaweza  kupimika  kwa  mifano  ya kuwepo  kwa  fursa  sawa  au  matokeo  sawa.  Au  kwa  kifupi,  tunaweza  kusema  kuwa  ni  haki,  majukumu na fursa sawa kwa wanawake na wanaume.
Ukatili wa kijinsia ni tatizo ambalo linawanyima uhuru wanaume, wanawake na watoto kufurahia haki zao za msingi ambazo pia ni haki za binadamu.
Utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha kuwa mwanamke mmoja katika kila wanawake watatu katika maisha yake amewahi kufanyiwa ukatili wa kijinsia ama kimwili, kingono na kisaikolojia.
Ukatili wa kijinsia umegawanyika katika makundi mbalimbali ikiwemo ukatili wa kimwili, ukatili wa kisaikolojia, ukatili wa kingono, ukatili utokanao na mila na desturi, ukatili wa kiuchumi,    na ukatili wa kijinsia sehemu za kazi.
Zipo sababu mbalimbali zinazopelekea ukatili wa kijinsia ikiwemo, mifumo ya jamii isiyozingatia usawa baina ya wanawake na wanaume, wanawake kutokuwa na sauti na ushiriki kwenye vyombo vya maamuzi ndani ya jamii na mitazamo hasi ya wanajamii kwa wanawake, pamoja na mfumo dume kwenye jamii.
Sababu nyingine ni umasikini, kuanguka kwa mifumo ya kijamii inayolinda maslahi ya wanajamii, ukimya wa jamii kukemea matendo ya ukatili wa kijinsia, na kukosekana kwa utekelezaji wa sheria za kudhibiti vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Hvi karibuni Serikali ilizindua Mpango Kazi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (2017-22) unaolenga kushirikisha wadau mbalimbali kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto na hivyo kusaidia wahanga wa ukatili huo kupata huduma stahiki ili kudhibiti ukatili nchini
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema kuwa jamii ina jukumu kubwa la kuhakikisha ukatili wa wanawake na watoto unapigwa vita kwa vitendo
“Serikali inaikumbusha jamii kupambana na vitendo vya ukatili kwani ukatili unafanyika kuanzia ngazi ya familia hivyo ni jukumu la wananchi kutoa taarifa za ukatili wa wanawake na watoto ili vyombo vya dola viweze kuchukua hatua za kisheria”, alisema Waziri Ummy
Aidha Waziri Ummy aliongeza kuwa kumekuwepo na matukio mengi ya ukatili yanayosababishwa na mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na umaskini katika familia, mila na desturi potofu zenye athari katika jamii, malezi na makuzi mabovu na sheria kandamizi.
Naye Mwakilishi wa Asasi za Kiraia zinazoshughulika na utetezi wa haki za watoto (TCRF), Erick Guga alisema watoto ndiyo wahanga wakubwa wa ukatili huo hivyo ni wakati mwafaka kwa mpango kazi kuanza kazi ili kuwanusuru wanawake na watoto katika ukatili
“Mpango Kazi huu wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto nchini Tanzania utakuwa ndiyo dira kwa wadau wote wa masuala ya maendeleo ya wanawake na watoto hapa nchini hivyo ni vema Serikali kushirikiana na wadau kila inapohitajika”, alisema Bw. Guga.
Waziri wa Fedha na Mipango Philip Mpango alizitaka Wizara, Taasisi zote za Serikali, Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanazingatia Mpango huo kwa kutenga fedha katika bajeti zao ili kukidhi utekelezaji wa shughuli zilizopangwa.
“Hata hivyo nazitaka taasisi zote zilizo chini ya Wizara yangu kutokomeza ukaliti wa wanawake mahali pa kazi na nitawachukulia hatua wale watakaojihusisha na ukatili huo” alisema Waziri Mpango.
Alisema kuwa athari ya madhara ya kuendelea kwa ukatili dhidi ya wanawake na watoto ni kubwa kijamii na kiuchumi ambapo kwa mujibu wa takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 asilimia 51.3 ya wanawake nchini, watoto chini ya miaka 18 ya watanzania walifanyiwa ukatili.
Kwa upande wake  Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,Bunge, Kazi, vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama, alisema kuwa ofisi yake itatoa miongozo ya kisheria katika utekelezaji wa mpango huo.
Alisema kuwa suala la kutokomeza ukatili si la Serikali pekee bali kuwataka Sekta binafsi, asasi za kirai na wadau wa maendeleo kuungana
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria, Dkt. Harrison Mwakyembe alisema kuwa katika Wizara yake inaandaa mkakati wa kushirikisha wananchi kutoa maoni kuhusu sheria ya ndoa ya mwaka 1971, kufanya mapitio ya pitia sheria ya mtoto ili kuweza kutokomeza suala la ukatili katika jamii.
Naye Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga alisema kuwa, kabla ya kuandaliwa kwa Mpango Kazi huu, Tanzania ilikuwa na mipango kazi minane (8) ya kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Akifafanua zaidi Sihaba alisema kuwa mipango hiyo haikuwa na mfumo wa kutokana na madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika maendeleo ya nchi, wakuu wa nchi wanachama wa Umoa wa Mataifa waliazimia kwa pamoja kutokomeza ukatili huo kupitia utekelezaji wa lengo Na. 5 na 6 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ifikapo 2030.
“Tanzania ni kati ya nchi nne (4) za kwanza duniani na nchi pekee katika Afrika iliyowezeshwa kupitia jukumu lilioanzishwa la kusaidia nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuandaa mpango wa kuzuia na kuitikia afua za kudhibiti ukatili”, alisema Sihaba.
Mpango huo unatarajiwa kuwezesha na kuondoa ukatili dhidi ya wanawake kwa asilimia 50 kufikia mwaka 2021/2022; na kuondoa ukatili dhidi ya watoto kwa asilimia 50 kufikia mwaka  2021/2022, na hivyo kuleta mabadiliko makubwa kwa kuwa na familia salama, na jamii yenye utulivu.
Kazi zitakazotekelezwa na kila mdau kuanzia familia, jamii, halmashauri, mikoa, wizara, sekta binafsi, asasi za Kiraia na wabia wa maendeleo Mpango umeweka mfumo fungamanishi wa uratibu, ufuatiliaji na tathmini ambao utaratibiwa katika ngazi ya Taifa na Ofisi ya Waziri Mkuu, ngazi ya mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa, na ngazi ya halmashauri na Wakurugenzi Watendaj

No comments:

Post a Comment