WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Monday, December 19, 2016

Mkuu wa Jamii Forums: Maxence Melo apewa dhamana Dar es Salaam

Bw Maxence Melo
Mwanzilishi wa Jamii Forums Maxence Melo, ambaye amekuwa akizuiliwa na maafisa wa polisi nchini Tanzania tangu Jumanne wiki iliyopita, amepewa dhamana na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Masharti ya dhamana ni wadhamini wawili ambao wote walisaini bondi ya shilingi milioni 5 za Tanzania na kwamba Maxenxe hatatoka nje ya Dar es Salaam pasipo kibali cha mahakama.
Bw Melo alishtakiwa kwa makosa matatu Ijumaa.
Makosa hayo ni kuendesha na kumiliki tovuti ambayo haijasajiliwa nchini Tanzania, na kuzuia uchunguzi wa polisi kwa mujibu wa Sheria ya Makosa Kimtandao.
Hakuweza kuwasilisha ombi la kuachiliwa kwa dhamana Ijumaa na alizuiliwa gereza la Keko wikendi.
Kesi itasikilizwa tena tarehe 29 Desemba.

No comments:

Post a Comment