WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Thursday, December 22, 2016

NIT YAKUSANYA MAPATO BILIONI 2 ZA ADA

PROF. MBARAWA: ANDAENI WATAALAMU WA KUTOSHA

mba1
Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Prof. Zakaria Mganilwa akitoa taarifa ya utendaji wa chuo hicho kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa katika uzinduzi wa Baraza la Chuo hicho, jijini Dar es Salaam.
mba2
Mwenyekiti mpya wa Baraza la Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Prof. Bavon Nchomba akifafanu jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa katika uzinduzi wa Baraza la Chuo hicho, jijini Dar es Salaam.
mba3
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wajumbe wa Baraza la Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), katika uzinduzi wa Baraza jipya la Chuo hicho, jijini Dar es Salaam.
mba4
Wafanyakazi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa katika uzinduzi wa Baraza jipya la Chuo hicho, jijini Dar es Salaam.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), kimetakiwa kuchangamkia fursa za kuandaa wataalam wa kada mbalimbali za usafirishaji wa anga ili kuinua sekta hiyo na kuiwezesha nchi kujulikana Kimataifa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa Baraza la Chuo hicho, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa kuzalisha wataalam pekee haitoshi bali ni jukumu la uongozi wa Baraza hilo kuhakikisha wanawasaidia wataalam hao kwa kuwaunganisha na mashirika makubwa ya usafirishaji lengo ni kuwajengea uwezo na kuwatambulisha kimataifa.

“Tayarisheni wataalamu na muwakutanishe na Wakurugenzi wakuu wa Makampuni kama Emirates, Qatar na Etihad ili kuwawezesha kupata fursa kirahisi na wao kuweza kuonekana kimataifa”, amesema Profesa Mbarawa.
Ameongeza kuwa Chuo kinahitaji kuchukua wafanyakazi kutoka Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), ili kutoa mafunzo kwao kwa ajili ya kuzalisha wataalam wenye ujuzi na uwezo wa kujenga miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Guage).

“Msipotumia fursa kama hizi za kuandaa wataalamu wa mbalimbali, tutakosa watalaamu wazawa wa miradi mikubwa na kuanza kulalamika kuwa Chuo kipo lakini hakithaminiki kumbe mwanzoni tulishindwa kujipanga”, amefafanua Waziri Prof. Mbarawa.

Prof. Mbarawa amelipongeza baraza lililopita kwa uwezo mkubwa wa kukusanya mapato ya ndani yatokanayo na ada za wanafunzi kutoka Bil. 2.1 kwa mwaka wa fedha 2011/2012 hadi kufikia Bil. 5.1 mwaka 2015/2016.

Aidha, Prof. Mbarawa ameutaka uongozi wa Chuo hicho kuweka mifumo imara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), ili kuweza kuwajengea mazingira mazuri kati ya Walimu na Wanafunzi.
Sambamba na hilo, ameutaka uongozi kupunguza idadi ya kozi zinazotolewa chuoni hapo na kuwa na kozi chache zenye tija na soko kimataifa ili kukifanya chuo hicho kuwa cha kipekee Afrika.
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa Baraza hilo Prof. Bavon Nchomba amemhakikishia Waziri huyo kushughulikia changamoto zote zinazoikabili chuo hicho kwa kuanzia na upunguzaji wa idadi za kozi zisizo na tija.

Naye, Mkuu wa chuo hicho Prof. Zakaria Mganilwa amesema chuo hicho kitaendelea kuandaa wataalamu mahiri na waliobobea katika Sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji na kuomba Serikali kuendelea kusaidia kuboresha miundombinu ya chuo hicho

No comments:

Post a Comment