WADHAMINI WETU

WADHAMINI WETU

Wednesday, December 7, 2016

Wasaliti wote sasa kunyongwa

Watu 15 wamehukumiwa kunyongwa kwa kushirikiana na IranMaandamano dhidi ya Saudi Arabia Iran

Mahakama moja nchini Saudi Arabia imewapa hukumu ya kifo watu 15 kwa kuwa majasusi wa Iran.
Watu hao ni miongoni mwa 32 ambao wanatoka madhehebu ya Ki-Shia, akiwemo raia mmoja wa Iran na Afghanistan.
Wakuu wa mashtaka wamewalaumu kwa kufanya njama ya mapinduzi ambapo pia wametuhumiwa kwa kuwa na mtandao wa ujasusi kwa ushirikiano na Iran na kutoa taarifa muhimu kuhusu jeshi.
Taharuki imeendelea kati ya Saudi Arabia inayofuata madhehebu ya Ki-Sunni na Iran inayofuata imani ya Shia.
Ufalme wa Saudia ulikata uhusiano wa kidoplomasia na Iran baada ya waandamanaji kuvamia ubalozi wake mjini Tehran kulalamikia kunyongwa kwa muhubiri maarufu wa Kishia raia wa Saudi Arabia Sheikh Nimr al-Nimr.
 Kifo chake kilizua maandamano nchini IranSheikh Nimr al-Nimr. alinyongwa na utawala wa Saudia

Saudia ilisisitiza kwamba Nimr alikua na makosa ya ugaidi, lakini kiongozi mkuu wa Iran akasema alinyongwa kwa kuukosoa ufalme.
Dola hizi mbili pia zinaunga mkono makundi pinzani katika vita nchini Yemen.
Raia Wa-Shia ni asili mia 10 pekee nchini Saudi Arabia na wamekua wakilalamikia kubaguliwa katika elimu ya umma, uhuru wa kuabudu, nafasi za kazi na hata masuala ya haki.

No comments:

Post a Comment